Pages

Showing posts with label Kigoma. Show all posts
Showing posts with label Kigoma. Show all posts

Monday, November 19, 2012

ZIARA YA VIONGOZI WA CUF MKOANI KIGOMA


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimiana na wanachama wa CCM na CUF mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kigoma kuanza ziara ya siku mbili ya kichama Mkoani humo.
  Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad akiwahutubia wafuasi na wapenzi wa chama hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika Wilayani Kasulu, Mkoa wa Kigoma.
 Mwenyekiti wa CUF Taifa Prof. Ibrahim Lipumba akiwahutubia wafuasi na wapenzi wa chama hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika Wilayani Kasulu, Mkoa wa Kigoma.
--
 
Tanzania inahitaji mabadiliko kwa kuwekeza katika kilimo cha kisasa sambamba na kutoa elimu na huduma bora kwa wakulima ili waweze kuendeleza kilimo chenye tija.
 
Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi CUF Profesa Ibrahim Lipumba alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma.
 
Amesema Tanzania imebarikiwa kuwa na ardhi yenye rutba inayokubali kuotesha mazao mbali mbali, lakini bado hakujakuwepo na mikakati imara ya kuendeleza kilimo, jambo ambalo linapaswa kufanyiwa kazi kwa maslahi ya wananchi.

Prof. Lipumba amefahamisha kuwa Mkoa wa Kigoma ni miongoni mwa Mikoa inayoweza kufanya vizuri katika kilimo kutokana na kuwepo kwa maziwa na mito ya kudumu ambayo inaweza kutumika kwa kilimo cha mboga mboga na umwagiliaji, na kusaidia kukuza kipato cha wakulima.
 
Sambamba na hilo Prof. Lipumba amewataka wakulima kutilia mkazo mazao ya nafaka yakiwemo mahindi na maharage, kutoka na kuongezeka kwa bei ya mazao hayo katika soko la dunia.
 
Mwenyekiti huyo wa CUF Taifa pia amesisitiza haja ya kuwepo kwa mikakati ya makusudi ya kuongeza ajira kwa vijana ili kuwanusuru kujiingiza katika vitendo viovu.
 
“Ukosefu wa ajira unatisha, na ikiwa vijana hawana ajira wanaweza kushawishika kufanya jambo lolote ambalo linaweza kuliletea madhara Taifa”, alifafanua Prof. Lipumba.
 
Akizungumzia kuhusu mchakato wa katiba, Prof. Lipumba ametaka katiba mpya ijayo itamke wazi kuwa maliasili za Tanzania na mali ya Watanzania na iweke itaratibu ambao Watanzania wataweza kunufaika na rasilimali hizo.
 
Amesema iwapo wananchi watanufaika moja kwa moja na rasilimali zao za nchi wataweza kuzilinda na kuziendeleza, lakini vyenginevyo rasilimali hizo zinaweza kuleta maafa badala ya neema kama zilivyo baadhi ya nchi za Afrika zikiwemo Nigeria na Equatorial Guinea.
 
Kwa mujibu wa Prof. Lipumba Tanzania ina utajiri wa rasilimali mbali mbali zikiwemo madini, mafuta na gesi asilia ambapo katika siku za hivi karibuni Kampuni moja ya Norway iligundua gesi yenye futi za ujazo trilioni 5 katika kisima kimoja pekee, ambapo jumla inakisiwa kuwepo na gesi trilioni 30 futi za ujazo.
 
Amesema rasilimaji zipo nyingi lakini zinahitaji kuwepo na uongozi wenye dira utakaozingatia mgawanyo wa rasilimali hizo kwa wananchi na kuimarisha miundombinu ya kiuchumi.
 
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad amesema CUF kitasimamia sera yake ya haki na usawa, ili kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata haki zake za msingi zikiwemo za kisiasa, kiuchumi na huduma za jamii.
 
Amesema tatizo kubwa la Tanzania ni mipango duni ya kiuchumi, na kuwashauri wananchi kukiunga mkono chama hicho ili kiweze kurekebisha kasoro zilizopo na kuimarisha uchumi wa nchi.
 
Kabla ya mkutano huo, Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, aliupongeza uongozi wa Mkoa huo kutokana na ushirikiano mzuri wanaoutoa kwa vyama vya siasa, na kwamba kufanya hivyo ni kuonesha ukomavu wa kisiasa.
 
Katika uwanja wa ndege wa Kigoma Maalim Seif alipokelewa na viongozi wa mkoa huo pamoja na wafuasi wa CUF na Chama Cha Mapinduzi.
 
Mkutano huo ni sehemu ya Operesheni mchakamchaka hadi 2015 iliyozinduliwa na chama hicho kwa ajili ya kutembelea mikoa mbali mbali ya Tanzania kutoa uelewa kwa wananchi ili hatimaye waweze kujiunga na chama hicho.

 
Na 
Hassan Hamad 
Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar

Tuesday, July 24, 2012

Nisihusishwe na Matamshi na Makanusho wa Wabunge walokuwa Kigoma

Katika gazeti la Mwananchi la tarehe 23 Julai 2012, kulikuwa na habari yenye kusomeka ‘Wabunge wamsafishia Zitto njia ya Urais 2015′. Habari hii imeleta mjadala mara baada ya kutoka na kusomwa. Mjadala umekuzwa zaidi baada ya Wabunge ndugu Halima Mdee na ndugu Joshua Nassari kukanusha maneno waliyonukuliwa kuyasema. Napenda kusema masuala yafuatayo.

Moja, Waheshimiwa Wabunge Halima Mdee, Joshua Nassari, Kangi Lugola, Esther Bulaya, Deo Filikunjombe, Raya Ibrahim, Amina Mwidau na David Kafulila walihudhuria tamasha la vijana wa Kigoma All Stars kwa kualikwa na Mratibu wa kundi hilo Mwasiti Almasi.

Wabunge wengine walialikwa lakini hawakutokea wakiwemo Joseph Mbilinyi, David Silinde, Amos Makala, Vicky Kamata na Peter Serukamba. Wabunge hawa hawakualikwa na mimi bali nilisaidia ‘logistics’ tu. Lengo la kushauriana na Vijana wa Kigoma All Stars kuwaalika wabunge kutoka vyama mbalimbali lilikuwa ni kuonyesha umoja na mshikamano wa nchi bila kujali vyama vya siasa.

Wabunge wote walioalikwa waliambiwa hii ni shughuli ya muziki na wala sikufanya mazungumzo nao yeyote ya awali au kuwaambia au kukubaliana nini cha kuzungumza au hapana. Tamasha lilikuwa la muziki na halikuhusika kabisa na siasa. Ni bahati mbaya sana kuwa kuna matamshi ya kisiasa yalitamkwa katika shughuli ile.

Waheshimiwa wote walipewa nafasi ya kusalimia na wote walizungumza. Wabunge waliozungumza kwa muda mrefu kidogo ni ndugu Halima Mdee, Joshua Nassari, Deo Filikunjombe na Kangi Lugola.

Hotuba za Wabunge wote zilirekodiwa kwenye video neno kwa neno na video hizo zitawekwa wazi kwenye blogu yangu kama sehemu ya documentary ya tamasha lile la kihistoria.

Pili, sikuhusika kwa namna yeyote ile na kuandikwa kwa habari hii iliyozusha mjadala. Wala sikujua kama habari hii ingeandikwa maana katika ziara ile sikuita mwandishi hata mmoja maana nilitaka liwe tukio la Kigoma tu. Mimi kama mlezi wa KigomaAllStars na vijana wenyewe tulijikita katika ‘shukrani Kigoma’ kwa watu wa Kigoma.

Kama mwandishi kaandika ambayo wabunge hawa hawakuyasema basi itaonekana kwenye videos hizo. Wabunge wenyewe wanajua kwenye nafsi zao nini walisema Kigoma na kipi kiliwasukuma kusema walioyasema Kigoma.

Nisingependa kuhusishwa kwa njia yeyote ile na matamshi yao, habari iliyowanukuu na hata makanusho yao. Maana mwisho wa siku ukweli ndio utasimama.

Suala la Urais lisitupotezee muda kwani kuna mambo mengi sana ya kujadili kuhusu nchi yetu. Taharuki ambazo watu wanazipata masuala ya urais yanapotajwa zinashangaza sana.

Chama changu bado hakijatangaza rasmi mchakato wa kupata mgombea Urais. Hivi sasa chama hakina mgombea Urais mpaka hapo mchakato utakapotangazwa ambapo wanachama wataruhusiwa kuomba kupeperusha bendera ya chama. Mwanachama wa chama chetu atakaye kubalika na jamii na wajumbe wa mkutano wa uteuzi ndiye atakuwa mgombea wetu. Kwa sasa hayupo na hivyo tusipoteze muda kujadili jambo hili.

Mzee Thabiti Kombo alituachia usia tunapokuwa tunazungumza. Alisema ‘weka akiba’ sio akiba ya fedha, bali ya akiba ya maneno. Tuweke akiba ya maneno. Tusimalize yote.

Monday, July 23, 2012

MKUTANO WA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA KIGOMA

Waziri wa Nchi Ofsi ya Rais, Mahusiano, Steven Wasira akihutubia kwenye mkutano wa CCM uliofanyika, jana , Julai 22, 2012, kwenye Uwanja wa Community Centre, Mwanga mjini Kigoma.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala wa Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI,) Aggrey Mwanri akihutubia, kwenye mkutano wa CCM uliofanyika, jana , Julai 22, 2012, kwenye Uwanja wa Community Centre, Mwanga mjini Kigoma.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye akihutubia, kwenye mkutano wa CCM uliofanyika, jana , Julai 22, 2012, kwenye Uwanja wa Community Centre, Mwanga mjini Kigoma.
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Charles Tzeba akihutubia kwenye mkutano wa CCM uliofanyika, jana , Julai 22, 2012, kwenye Uwanja wa Community Centre, Mwanga mjini Kigoma.
Viongozi.
Mamia ya wananchi waliofurika kwenye mkutano wa CCM katika Uwanja wa Community Centre, Mwanga mkoani Kigoma
Wazee kwenye mkutano wa CCM, Uwanjwa wa Community Cetre Mwanga Kigoma
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye akituzwa na Mbunge wa Kigoma Mjini, Peter Serukamba alipocharaza gita, kwenye mkutano wa CCM, Uwanja wa Communiy Cetre, Mwanga Kigoma
Habibu Ally wa kikundi cha Ujiji cha Sebene akicharaza kinanda akiwa chali wakati wa mkutano huo

Thursday, July 19, 2012

LekaDutigite Kigoma All Stars Concert Yadatisha

Mambo ya LekaDutigite Kigoma All Stars Concert
Mwanamuziki Machachari Diamond akidatisha Mashabiki
Wadau wakigoma wakisifia Burudani
Watu Kibao
Mheshimiwa Ziitto Kabwe akiongea
MbungewaKawe(Chadema)HalimaMdee(kushoto)akiwajukwaaninaMbungewaVitiMaalumCCM,Ester Bulaya.
Mheshimiwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA)Zitto Kabwe akiwa na Mashabiki
Mdau Akiwa Mwenye Furaha ndani ya Kigoma All Stars Concert
Waheshimiwa Wabunge Wakiwa kwenye Steji
Wasanii Wakikolezaaa burudani
Mdau Akishowlove ndano ya Kigoma LekaDutigite Kigoma All Stars Concert.Picha zote na Habari zimeletwa hapa na Mh, Zitto Kabwe-Mbunge wa kigoma kaskazini(CHADEMA)

Friday, June 8, 2012

MTOTO ALIYEUWAWA KWA BOMU KIGOMA

MTOTO OBEDI MANASE (8) MAREHEMU ALIYELIPUKIWA NA BOMU PICHA NA PARDON MBWATE WA JESHI LA POLISI KIGOMA
---
Na Mohammed Mhina na Pardon Mbwate-Jeshi la Polisi
Mwanafunzi mmoja wa darasa la kwanza katika shule ya msingi ya Kigadye wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma, Abeid Manase(8), amefariki dunia hapo hapo na wengine wanne kujeruhiwa vibaya baada ya kulipukiwa na bomu la kutupwa kwa mkono walilokuwa wakilichezea.
Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma ACP Fraisser Kashai, amewataja watoto waliojeruhiwa na bomu hilo kuwa ni wanafunzi wawili wa darasa la kwanza Tuju Seluke(7) aliyejeruhiwa tumboni na Sarah Manase(6) aliyejeruhiwa kwenye paja na mguu kulia. wote wanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya msingi Kigadye wilayani Kasulu.
Kamanda huyo amewata wengine waliojeruhiwa kuwa ni watoto wadogo wenye umri wa miaka minne kila mmoja ambao walikuwa wakichezea bomu hilo kwa pamoja ambao ni Enjord Seluke aliyejeruhiwa kwenye sikio la upande wa kushoto na Isaka Yohana aliyejeruhiwa kwenye jicho la upande wa kushoto.
Kamanda Kashai amesema majeruhi hao wote wamelazwa katika hospitali ya Misheni iliyopo katika kijiji cha Shunge wilauani Kasulu kwa matibabu zaidi na hali zao zimeelezwa kuwa zinaendelea vizuri.
Kamanda Kashai amesema jana majira ya saa 11.00 jioni, huko katika kijiji cha Kigadye, watoto hao walikuwa wakilichezea bomu hilo la kutupa kwa mkono na ndipo lilipowalipukia na kumuua mwenzao na wengine hao wane wakajeruhiwa.
Bomu hilo lilikuwa limefichwa katika moja ya bustani nyumbani kwa Bw. Ayoub James Luvahovi mkazi wa kijiji cha Kidae na likimbia mara baada ya tukio hilo na Polisi wanamsaka.
Katika tukio linguine Kamanda Kashai amesema huko Kasulu, watu wenye silahawamemjeruhi kwa kumpiga risasi tumboni mfanyabiashara mmoja Bi. Deothera Malusha(23) na baadaye kumpora shilingi 150,000 pamoja na simu yake ya mkononi aina ya Nokia yenye thamani ya shilingi 55,000.
Amesema baada ya uporaji huwo, majambazi hayo yalikimbia na kutokomea katika msituni na majeruhi amelazwa kwenye Hospitali ya wilaya ya kasulu mkoni Kigoma na hali yake bado sio nzuri.
Wakati huo huo, Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma linawashikilia watuhamiaji haramu 52 kwa makosa ya kuingia na kuishi nchini bila ya kibali.
Kamanda Kashai amesema kuwa wayuhumiwa hao walikamatwa katika maeneo mbalimbali walipokuwa wakifanya shughuli za uvuvi mkoani humo.

Sunday, June 3, 2012

POLISI MKOANI KIGOMA WAOKOA WATATU WANAOTUHUMIWA KWA UCHUWI

BAADHI YA WANANCHI WAKISHANGAA BAADA YA FAINES KUZINDULIWA NA MTOTO MWENYE MIAKA KUMI ALIYEKABIDHIWA MIKOBA NA MAMA YAKE.
BIBI NA MJUKUU WAKE WANAOSADIKIWA NI WACHAWI WAKIWA KATIKA GARI LA POLISI.
FAINES AKIPAKIWA KATIKA GARI YA POLISI.
FAINES ZAWADI-BINTI ALIYEFARIKI KWA MUDA NA KUREJESHWA DUNIANI AKIWA AMESHIKILIWA NA NDUGU ZAKE.
---
Jeshi la Polisi mkoani Kigoma limefanikiwa kuwaokoa watu watatu waliokuwa wamezingirwa na kundi la wananchi wakitaka kuwaua kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya ushirikina.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma SSP Joseph Konyo, aliwataja watu hao waliokolewa kuwa ni Evania Sephanga(50), mkazi wa wilaya ya Kibondo, Bruno January(46), mkazi wa kijiji cha Nyamhoza na mtoto mmoja mwenye umri wa miaka kumi na mkazi wa kijiji cha Nyamhoza Kigoma mjini ambaye jina lake linahifadhiwa.
Kamanda Konyo amesema kuwa wiki iliyopita majira ya saa tisa mchana, watu hao walizingirwa na kundi hilo kwa madai kuwa walimroga na kumuua msichana mmoja aitwaye Faines Zawadi(20) mkazi wa kijiji hicho cha Nyamhoza ambaye siku moja kabla ya kifo chake alionekana kama mtu aliyechanganyikiwa na kuwa kama kichaa.

Alisema katika tukio hilo, bibi kizee mmoja ambaye alikuwa mshirika wa kundi la waliodaiwa kuwa wachawi, alifanikiwa kutoroka katika mazingira ya kutatanisha alipojifanya kuwa anakwenda kujisaidia.
Kamanda Konyo amemtaja bibi huyo aliyefanikiwa kutoroka kuwa ni Bibi Editha Dosiyo mkazi wa kijiji hicho ambaye baadaye alipatikana na kuhojiwa kabla ya kukabidhiwa kwa Idara ya ustawi wa jamii baada ya kuonekana kuwa maisha yake yangekuwa hatarini.

Amesema baada ya Polisi kupata taarifa za tukio hilo, walikimbia na kwenda kuwaokoa kutoka katika mikono ya kundi la wananchi lakini wakiwa wameshaadhibu ingawa ilikuwa haijawa kwa kiasi kikubwa.

Habari zinasema kuwa, baadhi ya wananchi walipata taarifa kutoka kwa mtoto aliyeokolewa akisema kuwa baadhi ya watoto waliofariki kijijini hapo, akiwataja (majina tunayahifadhi) alikuwa akiwaona nyumbani kwao nyakati za usiku wakiosha vyombo na baadaye kupewa chakula.

Siku ya tukio hilo, baadhi ya wananchi walisema kuwa kabla ya bibi huyo kutoweka alimnong’oneza jambo mjukuu wake ili amfanyie mareheme ikiwa ni pamoja na kumruka mara saba kisha bibi huyo alitoweka akijifanya anakwenda kujisaidia.
Walisema mara baada ya bibi huyo kutoweka, mtoto huyo wa kiume ambaye ni miongoni mwa waliozingirwa wakitaka kuuawa, aliamza kutekeleza maagizo ya bibi huyo na alipomaliza kitendo cha kumruka kwa mara ya saba, msichana yuyo ambaye alikuwa ni marehemu alizinduka na kuomba uji.

Wamesema msichana huyo ambaye alikuwa mfu, alipewa uji na kunywa kisha akapelekwa hospitalini ambako hadi sasa hali yake inasemekana kuwa inaendelea vizuri.

Hata hivyo Kamanda Konyo ametoa wito kwa wananchi kuacha kuchukua sheria mkononi na badala yake watoe taarifa Polisi kwa kila jambo wanaloliona kuwa linaweza kuleta uvunjifu wa amani ili hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya wahusika.

Mwezi uliopita watu wawili mke na mume, waliuawa na kundi la watu wenye hasira kisha miili yao kuchomwa kwa moto mkoani Kigoma baada wa kutuhumiwa kuwa walikuwa ni wachawi.

Na
Pardon Mbwate na Felister Chubwa,
Polisi -Kigoma

Popular Posts