Pages

Showing posts with label Iringa. Show all posts
Showing posts with label Iringa. Show all posts

Monday, November 19, 2012

Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera na Uratibu wa Bunge, Wiliam Lukuvi Amjulia Hali Paroko wa Kanisa Katoliki Parokia ya Isimani mkoani Iringa baada ya Kuvamiwa na Majambazi


Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera na Uratibu wa Bunge, Wiliam Lukuvi (Katikati) akimjulia hali Paroko wa Kanisa Katoliki Parokia ya Isimani mkoani Iringa, Angelo Burgio wakati alipomtembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa jana. Picha na Mpiga Picha wetu.  
---
 
Geofrey Nyang’oro na Pius Kadinde Iringa

IDADI ya watu wanaotuhumiwa kuhusika na ujambazi katika matukio mawili tofauti kwenye Parokia za Kanisa Katoliki za Kihsesa na Isimani mkoani Iringa imeongezeka na kufikia nane huku mmoja wa watu waliokamatwa akiwa ni Dereva wa Paroko wa Parokia ya Isimani, Padri Angelo Burgio.
Tukio hilo ambalo lilisababisha mapadri wawili wa Parokia ya Isimani ambao ni Paroko wa Kanisa hilo Padri Burgio na msaidizi wake Padri Herman Myala na mlinzi wa Parokia ya Kihesa, Batholomeo Nzigilwa kujeruhiwa na kulazwa katika hosptali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa lilitokea usiku wa Novemba 15 na 16 mwaka huu.

Akitaja orodha hiyo mpya huku akisisitiza kuwa msako wa kuwatafuta watuhumiwa wengine unaendelea Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda alisema miongoni mwa watuhumiwa waliokamatwa ni pamoja na Dereva wa Paroko huyo ambaye hivi karibuni ndiye aliyemsindikiza kwenda kuchukua fedha Benki.
“Idadi ya watuhumiwa hadi sasa imefikia 8 na kati ya watuhumiwa wanne waliokamtwa jana katika msako unaoendelea hivi sasa mmoja wao ni Dereva Baba Paroko na ndiye aliyempeleka hivi karibuni kwenda Iringa Mjini kuchukua fedha,” alisema Kamuhanda.Kwa habari zaidi bofya na Endelea......>>>>>

Friday, October 19, 2012

Wakazi Wa Iringa, Waendelea Kutoa Maoni Kuhusu Katiba Mpya

Heny Mkenja, akijaza fomu maalumu ya maoni ya katiba mpya 
Baadhi ya wakazi wa Iringa ,kata ya Mivinjeni wakifatilia maoni ya wenzao kwa makini
Christina Mgongolwa, mkazi wa kata ya mivinjeni amependekeza kwamba katika katiba mpya ijayo,somo la maarifa ya nyumbani lipewe mhimu wake

Thursday, September 6, 2012

CCM YATOA TAMKO MAUAJI YA KUTISHA MWANDISHI WA HABARI MKOANI IRINGA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
Itakumbukwa tarehe 02/09/2012 katika operesheni za Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) mkoani Iringa kulitokea vurugu zilizosababisha kuuawa kwa mwanahabari mzoefu Ndg. Daudi Mwangosi na kujeruhiwa vibaya kwa askari watatu wa kuzuia fujo.

Chama Cha Mapinduzi kimepokea kwa masikitiko makubwa sana taarifa za kifo hicho na kujeruhiwa kwa askari hao. CCM inachukua nafasi hii kutoa pole kwa wafiwa, wanahabari nchini na wote walioguswa na msiba huu kwa namna moja au nyingine.

Tunatoa wito kwa vyombo na tume mbalimbali zilizoundwa kuchunguza swala hili, vichunguze kwa umakini na weledi mkubwa ili kubaini yote - ikiwemo chanzo cha vurugu zilizotokea na mazingira ya kifo cha ndugu yetu Daudi Mwangosi.

Pamoja na wito wetu wa kuchunguzwa suala hili kwa umakini na weledi mkubwa, pia tunatoa rai kwamba uchunguzi huu ufanyike kwa kutumia muda mfupi ili ukweli uweze kubainika mapema na hatua zinazostahili ziweze kuchukuliwa haraka iwezekanavyo.

Vilevile CCM inasikitishwa sana na mfululizo wa matukio ya watu kupoteza maisha au kujeruhiwa katika mikutano na operesheni mbalimbali zinazoendeshwa na CHADEMA nchini hasa zile zilizofanyika kwa kukaidi amri halali za vyombo vya ulinzi na usalama.

Kutaja matukio baadhi tu ni pamoja na lile la kuuwawa kwa kada wa CCM Mkoani Singida, kuuawa kwa Ndg. Ally Hassan mjini Morogoro, kuuawa kwa Ndg. Daudi Mwangosi Mjini Iringa hivi majuzi,kujeruhiwa kwa askari polisi Iringa na matukio mengine mengi ambayo yametokea wakati wenzetu wa CHADEMA wakiendesha operesheni zao mbalimbali nchini.

Matukio haya si mazuri kutokea kwenye shughuli za Chama cha siasa. Kwakweli ni aibu, inayohitaji uwajibikaji,hata kama ni wa kisiasa. Inapotokea shughuli za chama chako zinasababisha kupotea kwa maisha ya watu kila unapozifanya na bado usitake kuwajibika, inahitaji roho ngumu na ujasiri wa aina yake.

Inakuwa mbaya zaidi pale vifo hivi vinaposababishwa na Chama hicho kutotii amri halali zilizotolewa kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi inayovipa pia uhalali vyama vya siasa kuwepo na kuendesha shughuli zake kwa mujibu wa sheria.

Laiti Chama hicho kingesubiri siku chache zilizobakia kabla ya Sensa kuisha kabla ya kuendelea na mikutano yake ni dhahiri mauaji haya yasingetokea. Lakini kauli za kukebehi na uamuzi wa kukaidi amri ya Jeshi la Polisi na kusema "tupo tayari kwa lolote" ni ishara kwamba Chama hiki kiliandaa na kujiandaa na fujo zilizotokea.

Tunatoa wito kwa vyama vya siasa na wanasiasa kwa ujumla kujenga utamaduni wa kuheshimu utawala wa sheria. Amani na utulivu vulivyopo nchini ni kazi nzuri iliyojengwa kwa muda mrefu na waasisi wetu kwa kujenga utamaduni wa kuzingatia utawala wa sheria.

Imetolewa na;
Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Katibu wa NEC-Itikadi na Uenezi Taifa.

Monday, September 3, 2012

MWILI WA ALIYEKUWA KATIBU WA CCM MKOA WA MOROGORO ASHA KIPANGULA WAWASILI MKOANI IRINGA KWA MAZISHI

Vijana wa CCM wakibeba jeneza lenye mwili wa marehemu Asha Kipangula
Jeneza likiingizwa nyumbani kwa marehemu mjini Iringa
Naibu Katibu Mkuu wa CCM, John Chiligati akiagana na baadhi ya waombolezaji kabla ya mwili wa aliyekuwa Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro Mayr Chipangula, kuondoka Hospitali ya Taiafa Muhimbili Dar es Salaam,jana asubuhi kupelekwa Iringa kwa ajili ya maziko.
Msafara wa kuupeleka mkoani Iringa mwili wa marahemu Asha Kipangula ukiwasili Ofisi ya CCM mkoa wa Morogoro jana, ukitokea Dar es Salaam, ambapo kwenye ofisi hiyo ulisimamishwa kwa muda kutoa fursa kwa wana-CCM na waombolezaji wenmgine kuaga
Muombolezaji akiangua kilio nyumbani kwa marehemu mjini Iringa
Mmoja wa viongozi wa CCM akilia kwa huzuni baada ya mwili kufika Morogoro jana
Katibu wa CCM, Mary Chatanda akiangua kilio mwili wa marehemu Asha Chipangula ulipofikishwa nyumbani kwao Iringa jana jioni
Sheikh Mohammed Kairo akiongoza dua, mwili wa marehemu Asha Kipangula uliowasili mjini Morogoro jana
Nape akizungumza na baadhi ya waombolezaji mjini Morogoro. Aliyesimama ni Kada wa CCM, Asas
Kiongozi wa msafara, LKatibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itiladi na Uenezi CCM, Nape Nnauye akijadiliana na baadhi ya viongozi mwili ulipowasili mjini Morogoro. Baadhi ya viongozi hao ni Kaimu Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro Sixtus Mapunda.Picha na Bashir Nkromo

Sunday, September 2, 2012

Safari ya Mwisho ya Daud Mwangosi









Vurugu Baina ya Wafuasi wa Chadema na Polisi katika kijiji cha Nyololo, Mufindi

Hapa polisi wakiwataka wafuasi wa Chadema kutawanyika eneo la tukio ofisi za Chadema Nyololo Mufindi
Mmoja wa askari wa kutuliza ghasia ffu akipita mbele ya ofisi za Chadema Nyololomuda mfupi baada ya kupiga bomu la machozi
Daud Mwangosi kulia enzi za uhai dakika 20 kabla ya kuuwawa kwake
Sehemu ya wafuasi wa chadema wakiwa kwenye ofisi za Chadema Nyololo
Mwili wa mwanahabari Daud Mwangosi ukiwa chini
Sehemu ya magari matano ya Chadema yaliyoharibiwa vibaya kwenye vurugu hizo.Picha zote na Habari na Mdau Francis Godwin-Iringa

Taarifa Ya Jeshi la Polisi Kabla ya Vurugu Baina ya Wafuasi wa Chadema katika kijiji cha Nyololo, Mufindi,Iringa

JESHI la polisi mkoa wa Iringa limesema limezuia mikutano ya vyama vya siasa kwa vyama vyote na sio kwa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) pekee hivyo laonya vyama vyote kutii sheria bila shuruti.

Hata hivyo jeshi hilo la Polisi limesema kuwa halifanyi kazi kwa matakwa ya chama chochote cha siasa na kuwa si kweli kama wanavyodai viongozi wa Chadema kuwa jeshi la polisi linatumiwa na chama cha mapinduzi (CCM) kuzuia mikutano hiyo.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Michael Kamuanda ametoa kauli hiyo leo ofisini kwake alipozungumza na waandisha wa habari kuhusu zuio la mkutano wa Chadema uliopangwa kuanza leo katika wilaya ya Mufindi.

" Nawatangazia wanasiasa na vyama vyote vya siasa pamoja na wananchi wa mkoa wa Iringa kuwa hakutakuwa na mikutano ya kisiasa kutokana na shughuli za sensa zinazoendelea ....hivyo basi nawaomba wananchi wote kutoshiriki mikutano yoyote ya kisiasa itakayoitishwa na wanasiasa "alisisitiza

Kuwa mikutano hiyo imezuiliwa kwa kipindi hiki cha sensa kilichoongezwa hadi hapo tamko litakapotolewa tena na msajili wa vyama vya siasa John Tendwa kama alivyokwisha kutoa tamko la kuzuia shughuli hizo za vyama vya siasa kwa kipindi hiki cha sensa.

"Wananchi wote wa mkoa wa Iringa mnaombwa kutii sheria bila shuruti hii ni amri ....nawaombeni sana wananchi kutodanganywa na wanasiasa kwa kuvunja sheria "aliongeza kamanda huyo wa polisi.

Hata hivyo alisema kuwa kimsingi zoezi la sensa lilipaswa kuhitimishwa Septemba mosi mwaka huu ila kutokana na serikali kuongeza muda wa zoezi hilo bado jeshi hilo la polisi linazingatia maagizo ya Msajili wa vyama vya siasa kama alivyoyatoa kwa jeshi hilo.

Kamanda Kamuanda alisema kuwa jeshi hilo la polisi wala msajili wa vyama vya siasa hajazuia vyama vya siasa kuendelea na vikao vyao vya ndani kwa kipindi hiki na kuwa hata Chadema wakiwa mkoani Iringa wameendelea kufanya vikao vyao vya ndani katika kata mbali mbali za mkoa wa Iringa na hakuna mtu aliyewazuia kuendelea kufanya hivyo.

Friday, August 31, 2012

Dkt Slaa akutana na waandishi wa Habari Mkoani Iringa

katibu mkuu wa Chadema Dkt Slaa akionyesha baadhi ya vielelezo kwa wanahabari leo mjini Iringa
Dkt Slaa akiwa katika mkutano wake na wanahabari mkoa wa Iringa katika ukumbi wa Hoteli ya M.R

Katibu mkuu huyo wa Chadema Taifa Dkt Slaa ameibua mambo mazito juu ya waziri Sitta na serikali yake katika mkutano huo na kueleza mikakati mbali mbali ya Chadema .

KAMANDA UVCCM IRINGA AWAPA SOMO VIJANA IRINGA VIJIJINI

kamanda wa UVCCM wilaya ya Iringa vijijini Arif Abri akifungua mkutano wa uchaguzi wa UVCCM wilaya ya Iringa vijijini leo
Wajumbe wakiwa wamependeza kwa sare zilizotolewa na kamanda huyo na mbunge Lukuvi na Mgimwa
Waandishi wakipewa kadi za CCM Leo


CHANGAMOTO imetolewa kwa vijana wa Chama cha mapinduzi ( UVCCM) wilaya ya Iringa vijijini mkoani Iringa kufanya kazi kwa kujituma zaidi badala ya kuendelea kulalamika vijiweni bila kufanya kazi.

Changamoto hiyo imetolewa Leo katika ukumbi wa Sekondari ya Mwembetogwa mjini Iringa na mgeni rasmi katika mkutano mkuu wa uchaguzi wa UVCCM ambaye pia ni kamanda wa UVCCM wilaya ya Iringa vijijini Arif Abri .

Abri amesema kuwa hivi sasa imejitokeza tabia ya vijana kulalamika juu ya hali ngumu ya maisha hata kuhoji juu ya maisha bora huku sehemu kubwa ya vijana hao wakiendelea kushinda vijiweni jambo ambalo ni kinyume na harakati za kujitafutia maisha bora kwa kila mtanzania.

Hata hivyo amewataka vijana hao kuendelea kujishuguulisha na shughuli za Uzalishaji mali ikiwa ni pamoja na kujiunga katika vikundi vya kiuchumi ili kuiwezesha serikali kuweza kuwasaidia mikopo yenye masharti nafuu.

Abri amesema kuwa vijana ambao ni tegemeo kubwa katika Taifa bado wanalojukumu kubwa la kuendelea kuwavuta vijana wenzao ambao wanakimbilia vyama vya upinzani.

wakati huo huo Abri amewapongeza wanahabari watano mkoani Iringa ambao wamejiunga na UVCCM wilaya ya Iringa vijijini.

Katibu wa UVCCM wilaya ya Iringa vijijini Frank Kibiki aliwataja wanahabari walioniunga na CCM kuwa ni meneja wa IT Ebony Fm Eliud Kalokola , Flora Kamaghe kutoka gazeti la Uhuru, Zuhura Zukheli kutoka radio Qibra ten ,Wiliam Muro kutoka gazeti la kwanza jamii na NEEMA Mgulanga mwanahabari wa kujitegemea .

MWISHO

Mwenyekiti mpya UVCCM Iringa vijijini ni Benitho Kayugwa

Mwenyekiti mpya UVCCM Iringa vijijini Benitho Kayugwa akieleza mikakati yake baada ya kutangazwa mshindi

Vijana wa UVCCM Iringa vijijini wakiwa wamembeba mwenyekiwa wao mpya

Haya ndio matokeo ya uchaguzi UVCCM Iringa vijijini


Hata hivyo kutokana na kukatika ghafla kwa umeme kutokana na Hitirafu iliyotokea Ipogolo mwenyekiti huyo alijikuta akikabidhiwa kiti hicho gizani .

Huku akiendelea kuwahutubia vijana kwa kutumia mwanga wa tochi za simu za mikononi kabla ya katibu wa mbunge jimbo la Isimani Thomas Malenga kujitolea kukimbia nyumbani kwake kuchukua taa

Sunday, July 29, 2012

Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati (CCM) asaidia timu ya Taswa Iringa

Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati (CCM) ameisaidia jezi seti moja timu ya waandishi wa habari za michezo Tanzania (TASWA) mkoa wa Iringa kama njia ya kuiunga mkono timu hiyo katika kuhamasisha michezo mkoani Iringa.

Akikabidhi msaada huo leo kwa mwenyekiti wa TASWA mkoa wa Iringa Bw.Francis Godwin ,mbunge Kabati alisema kuwa amelazimika kutoa msaada huo kama sehemu ya kuunga mkono unzishwaji wa timu hiyo .
Kwani alisema suala la michezo lime katika ilani ya uchaguzi wa CCM hivyo akiwa kama mbunge ameguswa na mkakati wa wanahabari mkoa wa Iringa katika kuhamasisha michezo na kuwa miongoni mwa wadau wa kweli wa michezo ambao wamekuwa wakiandika habari za michezo ila pia na wao wenyewe kuonyesha mfano katika michezo kwa kuwa na timu yao.

Mbunge Kabati alitoa wito kwa wabunge wengine na wadau wa michezo katika mkoa wa Iringa kujitokeza kuisaidia timu hiyo vifaa vya michezo pamoja na misaada mbali mbali pale inapohitajika ili kuiwezesha kuwa timu bora katika mkoa wa Iringa.

Popular Posts