IDADI ya watu wanaotuhumiwa kuhusika na ujambazi katika matukio mawili tofauti kwenye Parokia za Kanisa Katoliki za Kihsesa na Isimani mkoani Iringa imeongezeka na kufikia nane huku mmoja wa watu waliokamatwa akiwa ni Dereva wa Paroko wa Parokia ya Isimani, Padri Angelo Burgio.
Translate - Tafsiri
Labels
- Tamko kwa Umma - Press Release
- All Photos - Picha
- CCM CHAMA CHA MAPINDUZI
- Zanzibar
- IKULU - STATE HOUSE
- Sports - Michezo
- CHADEMA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO
- Dodoma
- Editorial Opinion - Maoni Tahariri
- Tanzania
- Dar es salaam
- Habari za Kimataifa - International News
- Burudani - Entertainment
- Bungeni
- Katiba - Constitution
- Dini - Religion
- Mbeya
- SMZ Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
- Vodacom
- Hotuba - Speech
- Arusha
- Iringa
- Tanzia - Msiba - Mazishi
- Afya - Health
- Ofisi ya Waziri Mkuu
- Singida
- Ajali - Accident
- Development Reports
- Morogoro
- Open Letters - Barua za Wazi
- Urembo - Beauty
- Kenya
- CUF Chama cha Wananchi
- Maonyesho ya Sabasaba
- Ofisi ya Makamu wa Rais
- Huduma za Usafiri - Transport Services
- Tanga
- Business Finance Money
- Masuala ya Elimu - Education
- Miundombinu -Infrastructure
- Mtwara
- Rukwa
- UVCCM
- Habari za Mahakamani
- Kilimanjaro
- Serengeti Breweries Limited
- Tourism - Utalii
- Habari za Nyumbani - Local News
- Jakaya Mrisho Kikwete
- Kagame Cup - Kombe la Kagame
- Katavi
- Lindi
- Nishati - Madini - Mining - Energy
- UN United Nations - Umoja Mataifa
- Yanga
- African Union - Umoja wa Afrika
- Bagamoyo
- Agriculture - Kilimo
- Azam FootBall Club
- Balozi na Ofisi za Balozi
- Baraza la Wawakilishi
- Human Rights - Haki za Binadamu
- Jeshi la Polisi Tanzania
- Kigoma
- Maonyesho ya Nane Nane
- Simba Sports Club
- Tabora
- East African Community
- HARUSI - WEDDINGS
- Kagera
- Mwanza
- Pemba
- Shinyanga
- Sumbawanga
- TFF Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania
- Videos - Multimedia
- Wizara ya Mambo ya Nje Na Ushirikiano wa Kimataifa
- Wizara ya Nishati na Madini
- Afdb African Development Bank
- Airtel Tanzania
- Benki - Fedha - Uchumi
- Fiesta 2012
- GEITA
- Mafuta - Oil Issues
- Uganda
- Wizara ya Maliasili na Utalii
- BAJETI 2012 - 2013
- Burundi
- Climate Change - Mabadiliko ya Tabia Nchi
- FASHION - MITINDO - MAVAZI
- ICT Information and communications technology
- Kambi ya Upinzani
- London Olympic Games 2012
- Mambo ya Zamani - Archives
- Maonyesho ya Biashara - Trade Shows
- Mara
- Mobile - Telecoms
- NHIF National Health Insurance Fund
- Peace and Security
- Rwanda
- Sayansi na Tekinolojia
- Wizara ya Elimu na Ufundi
- Wizara ya Mambo ya Ndani
- Wizara ya Uchukuzi
- Zambia
- BOT Bank of Tanzania Benki Kuu ya Tanzania
- Events - Matukio
- Habari za Majimboni
- Mahojiano - Interview
- Makala - Articles
- Malawi
- Mkoa wa Pwani
- Musoma
- NJOMBE
- National Parks - Mbuga za Wanyama
- Ruvuma
- SONGEA
- Shirika la Nyumba laTaifa - NHC
- TBL Tanzania Breweries Limited
- Taifa Stars - Timu ya Taifa
- UDAKU UMBEYA GOSIP
- US EMBASSY - UBALOZI WA MAREKANI
- University of Dar es salaam - Chuo Kikuu cha Dar es salaam
- ABG African Barrick Gold
- BAKWATA
- Banks - Benki
- Environment - Mazingira
- Ilala
- Kilimo Kwanza
- Land and Land Grabbing Issues - Ardhi
- Love Relationships - Mapenzi Mahusiano
- MIKUTANO
- Mabondia - Boxing
- Manyara
- Miradi ya Maendeleo
- Misaada - Donations
- Mombasa
- NCCR MAGEUZI
- Nairobi
- People - Watu
- Picha ya Wiki - Photo of the Week
- Precision Air
- Procurement
- Ripoti Maalumu
- SANAA - ARTS
- Sensa ya Makazi na Watu 2012
- Sheria - Law
- Somalia
- South Africa
- South Sudan - Sudani Kusini
- Takwimu - Statistics
- Tigo
- Travel - Safari
- Ugaidi - Terrorism
- Ulinzi na Usalama - Security and Defence
- Wizara ya Afrika Mashariki
- Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
- Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo
- Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Teknologia
- Wizara ya Viwanda na Biashara
- Zimbabwe
Blog List
Monday, November 19, 2012
Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera na Uratibu wa Bunge, Wiliam Lukuvi Amjulia Hali Paroko wa Kanisa Katoliki Parokia ya Isimani mkoani Iringa baada ya Kuvamiwa na Majambazi
IDADI ya watu wanaotuhumiwa kuhusika na ujambazi katika matukio mawili tofauti kwenye Parokia za Kanisa Katoliki za Kihsesa na Isimani mkoani Iringa imeongezeka na kufikia nane huku mmoja wa watu waliokamatwa akiwa ni Dereva wa Paroko wa Parokia ya Isimani, Padri Angelo Burgio.
Friday, October 19, 2012
Wakazi Wa Iringa, Waendelea Kutoa Maoni Kuhusu Katiba Mpya
Thursday, September 6, 2012
CCM YATOA TAMKO MAUAJI YA KUTISHA MWANDISHI WA HABARI MKOANI IRINGA
Itakumbukwa tarehe 02/09/2012 katika operesheni za Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) mkoani Iringa kulitokea vurugu zilizosababisha kuuawa kwa mwanahabari mzoefu Ndg. Daudi Mwangosi na kujeruhiwa vibaya kwa askari watatu wa kuzuia fujo.
Chama Cha Mapinduzi kimepokea kwa masikitiko makubwa sana taarifa za kifo hicho na kujeruhiwa kwa askari hao. CCM inachukua nafasi hii kutoa pole kwa wafiwa, wanahabari nchini na wote walioguswa na msiba huu kwa namna moja au nyingine.
Tunatoa wito kwa vyombo na tume mbalimbali zilizoundwa kuchunguza swala hili, vichunguze kwa umakini na weledi mkubwa ili kubaini yote - ikiwemo chanzo cha vurugu zilizotokea na mazingira ya kifo cha ndugu yetu Daudi Mwangosi.
Pamoja na wito wetu wa kuchunguzwa suala hili kwa umakini na weledi mkubwa, pia tunatoa rai kwamba uchunguzi huu ufanyike kwa kutumia muda mfupi ili ukweli uweze kubainika mapema na hatua zinazostahili ziweze kuchukuliwa haraka iwezekanavyo.
Vilevile CCM inasikitishwa sana na mfululizo wa matukio ya watu kupoteza maisha au kujeruhiwa katika mikutano na operesheni mbalimbali zinazoendeshwa na CHADEMA nchini hasa zile zilizofanyika kwa kukaidi amri halali za vyombo vya ulinzi na usalama.
Kutaja matukio baadhi tu ni pamoja na lile la kuuwawa kwa kada wa CCM Mkoani Singida, kuuawa kwa Ndg. Ally Hassan mjini Morogoro, kuuawa kwa Ndg. Daudi Mwangosi Mjini Iringa hivi majuzi,kujeruhiwa kwa askari polisi Iringa na matukio mengine mengi ambayo yametokea wakati wenzetu wa CHADEMA wakiendesha operesheni zao mbalimbali nchini.
Matukio haya si mazuri kutokea kwenye shughuli za Chama cha siasa. Kwakweli ni aibu, inayohitaji uwajibikaji,hata kama ni wa kisiasa. Inapotokea shughuli za chama chako zinasababisha kupotea kwa maisha ya watu kila unapozifanya na bado usitake kuwajibika, inahitaji roho ngumu na ujasiri wa aina yake.
Inakuwa mbaya zaidi pale vifo hivi vinaposababishwa na Chama hicho kutotii amri halali zilizotolewa kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi inayovipa pia uhalali vyama vya siasa kuwepo na kuendesha shughuli zake kwa mujibu wa sheria.
Laiti Chama hicho kingesubiri siku chache zilizobakia kabla ya Sensa kuisha kabla ya kuendelea na mikutano yake ni dhahiri mauaji haya yasingetokea. Lakini kauli za kukebehi na uamuzi wa kukaidi amri ya Jeshi la Polisi na kusema "tupo tayari kwa lolote" ni ishara kwamba Chama hiki kiliandaa na kujiandaa na fujo zilizotokea.
Tunatoa wito kwa vyama vya siasa na wanasiasa kwa ujumla kujenga utamaduni wa kuheshimu utawala wa sheria. Amani na utulivu vulivyopo nchini ni kazi nzuri iliyojengwa kwa muda mrefu na waasisi wetu kwa kujenga utamaduni wa kuzingatia utawala wa sheria.
Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Katibu wa NEC-Itikadi na Uenezi Taifa.
Monday, September 3, 2012
MWILI WA ALIYEKUWA KATIBU WA CCM MKOA WA MOROGORO ASHA KIPANGULA WAWASILI MKOANI IRINGA KWA MAZISHI










Sunday, September 2, 2012
Vurugu Baina ya Wafuasi wa Chadema na Polisi katika kijiji cha Nyololo, Mufindi
Taarifa Ya Jeshi la Polisi Kabla ya Vurugu Baina ya Wafuasi wa Chadema katika kijiji cha Nyololo, Mufindi,Iringa
Hata hivyo jeshi hilo la Polisi limesema kuwa halifanyi kazi kwa matakwa ya chama chochote cha siasa na kuwa si kweli kama wanavyodai viongozi wa Chadema kuwa jeshi la polisi linatumiwa na chama cha mapinduzi (CCM) kuzuia mikutano hiyo.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa Michael Kamuanda ametoa kauli hiyo leo ofisini kwake alipozungumza na waandisha wa habari kuhusu zuio la mkutano wa Chadema uliopangwa kuanza leo katika wilaya ya Mufindi.
" Nawatangazia wanasiasa na vyama vyote vya siasa pamoja na wananchi wa mkoa wa Iringa kuwa hakutakuwa na mikutano ya kisiasa kutokana na shughuli za sensa zinazoendelea ....hivyo basi nawaomba wananchi wote kutoshiriki mikutano yoyote ya kisiasa itakayoitishwa na wanasiasa "alisisitiza
Kuwa mikutano hiyo imezuiliwa kwa kipindi hiki cha sensa kilichoongezwa hadi hapo tamko litakapotolewa tena na msajili wa vyama vya siasa John Tendwa kama alivyokwisha kutoa tamko la kuzuia shughuli hizo za vyama vya siasa kwa kipindi hiki cha sensa.
"Wananchi wote wa mkoa wa Iringa mnaombwa kutii sheria bila shuruti hii ni amri ....nawaombeni sana wananchi kutodanganywa na wanasiasa kwa kuvunja sheria "aliongeza kamanda huyo wa polisi.
Hata hivyo alisema kuwa kimsingi zoezi la sensa lilipaswa kuhitimishwa Septemba mosi mwaka huu ila kutokana na serikali kuongeza muda wa zoezi hilo bado jeshi hilo la polisi linazingatia maagizo ya Msajili wa vyama vya siasa kama alivyoyatoa kwa jeshi hilo.
Kamanda Kamuanda alisema kuwa jeshi hilo la polisi wala msajili wa vyama vya siasa hajazuia vyama vya siasa kuendelea na vikao vyao vya ndani kwa kipindi hiki na kuwa hata Chadema wakiwa mkoani Iringa wameendelea kufanya vikao vyao vya ndani katika kata mbali mbali za mkoa wa Iringa na hakuna mtu aliyewazuia kuendelea kufanya hivyo.
Friday, August 31, 2012
Dkt Slaa akutana na waandishi wa Habari Mkoani Iringa
KAMANDA UVCCM IRINGA AWAPA SOMO VIJANA IRINGA VIJIJINI
Mwenyekiti mpya UVCCM Iringa vijijini ni Benitho Kayugwa
Huku akiendelea kuwahutubia vijana kwa kutumia mwanga wa tochi za simu za mikononi kabla ya katibu wa mbunge jimbo la Isimani Thomas Malenga kujitolea kukimbia nyumbani kwake kuchukua taa
Sunday, July 29, 2012
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati (CCM) asaidia timu ya Taswa Iringa