Pages

Friday, January 4, 2013

Dkt. Mwakyembe akagua uwanja wa ndege wa Songwe, Mbeya


Picture
Waziri wa uchukuzi Dkt. Harrison Mwakyembe akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza ziara yake katika uwanja wa Ndege wa Songwe, Mbeya amesema kuwa uwanja huo una hadhi ya Kimataifa na ni kati ya viwanja vikubwa viwili kujengwa baada ya uhuru, ukitanguliwa na uwanja wa Mkoa wa Kilimanjaro (KIA).

(picha zote na maelezo, credit: Mbeya Yetu blog)
Picture
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) Mhandisi Suleiman S. Suleiman akimwelezea Dkt. Harrison Mwakyembe jinsi uwanja wa ndege wa Songwe unavyofanya kazi toka uzinduliwe mwezi wa 12 mwaka jana na kuwa sasa uwanja huo umebaki kukamilisha maeneo ya maegesho ya ndege kubwa kama Boeing 737.
Picture
Hili ni eneo la kutua ndege na kurukia barabara hiyo ya ndege yenye urefu wa zaidi ya kilometa 3.5 km
Picture
Huu ni mnara wa kuongozea ndege katika kiwanja hicho
Picture
Mwongoza ndege mwandamizi John Chambo akimwezea waziri Mwakyembe jinsi wananvyofanya kazi ya kuongoza ndege katika mnara huo
Picture
Sura ya mbele ya uwanja wa Songwe
Picture
Maegesho ya zimamoto
Picture
Hili ndilo eneo la maegesho ya ndege kubwa aina ya Boeing 737 ambalo mwishoni mwamwezi huu linatarajiwa kuwa limekamilika


Source: http://www.wavuti.com/#ixzz2H2wxliuB

Popular Posts