Pages

Showing posts with label UN United Nations - Umoja Mataifa. Show all posts
Showing posts with label UN United Nations - Umoja Mataifa. Show all posts

Thursday, July 26, 2012

Mdhibiti Na Mkaguzi Mkuu Wa Hesabu Za Serikali Akabidhiwa Ujumbe Wa Bodi Ya Ukakuzi Wa Umoja Wa Mataifa

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaUtouh(Kulia)akikabidhiwa rasmi Ujumbe wa Bodi ya Wakaguzi ya Umoja wa Mataifa ( UNBOA)
---
Na Mwandishi Maalum
Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imekabidhiwa rasmi Ujumbe wa Bodi ya Wakaguzi ya Umoja wa Mataifa ( UNBOA)Makabidhiano hayo yamefanyika siku ya Jumatano hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, katika hafla iliyofanyika mwishoni mwa mkutano wa 66 wa Bodi ya Wakaguzi ya UM.
Katika hafla hiyo Afrika ya Kusini ndiyo iliyoikabidhi Tanzania kijiti hicho. Makabidhiano ambayo yalishuhudiwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Mhe. Balozi Ombeni Sefue ambaye ameiwakilisha Serikali katika makabidhiano hayo.
Afrika ya Kusini imekuwa mjumbe wa Bodi kwa miaka 12 na Tanzania itamaliza ngwe yake mwaka 2018Aidha hafla hiyo pia ilihudhuriwa na Bi Suzan Malcora ambaye ni Msimamizi Mkuu wa Ofisi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (Chief de Cabinet). Akimwakilisha Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Mhe. Ban Ki Moon.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo iliyowashirikisha pia wajumbe wengine wa bodi ambao ni Bw. Dong Dasheng akimwakilishi Mkaguzi Mkuu kutoka Uchina na Bw. Amyas Morse Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu kutoka Uingereza. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu , Bw. Ludovick Utouh amewahakikisha wajumbe wenzie pamoja na sekretariati ya Umoja wa Mataifa kwamba Ofisi yake imejipanga vema kulibeba jukumu hilo.
“ Hafla hii ya leo inahitimisha rasmi mchakato mrefu wa makabidhiano ya jukumu hili, mchakato ulioanza tangu uteuzi wangu ulipofanyika mwezi Novemba mwaka jana. Ni mchakato unaofungua ukurasa wa kubadilishana mawazo, uzoefu na utaalamu. Kwa niaba ya Nchi yangu, Ofisi yangu na mimi mwenyewe binafsi naomba nitoe shukrani zangu za dhati kwa wajumbe wa Bodi ya UM na Kamati ya Operesheni za Ukaguzi” akasema Bw. Otouh.
Akabainisha kwamba Tanzania inachukua jukumu hilo la kuwa mjumbe wa UNBOA katika kipindi muhimu, kipindi ambacho UM unapita katika mageuzi makubwa ya kubadili mifumo yake ya kiutendaji ikiwamo kutoka utumiaji wa mfumo ujulikanao kama UNSAS kwenda mfumo wa IPSAS.
“ Tunaingia katika bodi hii katika kipindi ambacho UM inapitia mageuzi makubwa yakiwamo yale ya kutoka ukaguzi uliokuwa ukifanyika kila baada ya miaka miwili na kuingia katika ukaguzi wa kila mwaka”. Akasisitiza Otuoh
Na kuongeza. “ Matokeo ya mageuzi haya maana yake ni kuongezeka kwa ukubwa wa kazi kwa upande wa wakaguzi, ogezeko ambalo litatupasa si tu kufanya kazi kwa umakini mkubwa lakini pia kutekeleza majukumu mengi na katika muda mfupi”.
Na kwa sababu hiyo, akasema, kwa kutambua uzito na unyeti wa kazi kubwa iliyombele, ndiyo maana baada ya kuteuliwa kwake yeye na maafisa wake walianza jukumu la kujianda kwa kila hali ili waweze kulitekeleza jukumu hilo kwa ukamilifu na weledi mkubwa.
Akatumia fursa hiyo kuishukuru Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Afrika ya Kusini kwa namna ambavyo imetoa ushiriano mkubwa na wa karibu sana, kuanzia siku ile Ofisi ya NAOT ilipopitishwa kwa kauli moja na Baraza Kuu la 66 la Umoja wa Mataifa kushika wadhifa huo.
Aidha akasema ingawa Afrika ya Kusini imemaliza ujumbe wake, Tanzania itaendelea kushirikiana nayo kwa karibu hasa kwa kuzingatia kwamba kukabidhiwa kwa jukumu hilo hakuhitimishi mchakato mzima wa kuendelea kubadilishana uzoefu na utaalamu.
Naye Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue akizungumza kwa niaba ya serikali, pamoja na kuwashukuru wajumbe wa bodi ya UNBOA na sekretarieti yake. Amesema Serikali inauchukulia ujumbe huo kwa uzito wa aina yake.
“Nimefurahi sana kuwapo hapa na kuiwakilisha serikali, ninapenda ninawakikishie kwamba, serikali yangu inalipa jambo hilo uzito wa kipekee sana. Heshima na mchango wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa unafamika na sasa tunapoingia katika jukumu hili ni dhahiri kwamba tunataka kufanya kazi nzuri hata katika maeneo mengine na uwezo huo tunao” akasisitiza.
Naye Naibu Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu kutoka Afrika ya Kusini Bw. Thembekile Makwetu akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, amemhakikisha Bw. Utouh na ofisi yake ushirikiano wa karibu na usiotereka. Huku wajumbe wengine wa Bodi nao wakielezea kutoa ushirikiano kwa Tanzani na kuikaribisha kwa moyo mkunjufu.
Kwa upande wake, Bi Susan Malcora akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, yeye amesema anaikaribisha Tanzania katika ujumbe wa bodi hiyo kwa mikono miwili na kusisitiza kwamba ujumbe wa Tanzania katika Bodi hiyo utasaidi sana katika kusukuma mbele ajenda ya uwajibikaji na udhibiti wa fedha na mali zinazomilikiwa na Umoja wa Mataifa.
Akasema Umoja wa Mataifa, unatambua umuhimu na mchango mkubwa wa Bodi hiyo na kuongeza kwamba itafanya kazi kwa karibu wa wajumbe wa bodi ili kuhakikisha kwamba mageuzi yanayoendelea hivi sasa ndani ya UM yanafanyika kwa ukamilifu na kwamba watazingatia ushauri na maelekezo watakayopewa na Bodi.

Saturday, July 14, 2012

Dr Asha-Rose Migiro appointed as UN Secretary-General’s Special Envoy for HIV/AIDS in Africa

GENEVA, 13 July 2012—United Nations Secretary-General Ban Ki-Moon has appointed Asha-Rose Migiro as his Special Envoy for HIV/AIDS in Africa. “Ms Migiro’s experience in responding to AIDS as UN Deputy Secretary-General, combined with her many years as an advocate for health and social justice in Africa, make her uniquely qualified for this important role,” said Mr Ban.

Ms Migiro served as the United Nations Deputy Secretary-General from 2007 to 2012. In that role, she was integrally involved in promoting the AIDS response globally and within Africa, with special emphasis on reducing the vulnerability of women and girls and ensuring the rights of people living with HIV.

“I am honoured to accept this appointment at this crucial moment in the African AIDS response,” said Ms Migiro. “A decade ago, HIV in Africa was almost entirely an epidemic of despair. Today, we celebrate progress against AIDS that we never thought possible. Now is the time to take our efforts to a new level––I am committed to the Secretary-General’s vision that the beginning of the end of AIDS in Africa starts now.”

Ms Migiro served as Tanzania’s Minister of Foreign Affairs and International Cooperation from 2006 to 2007—the first woman to hold that position since the country’s independence. She was previously the Minister for Community Development, Gender and Children for five years. Prior to Government service, she pursued a career in academia, and, served as a member of Tanzania’s Law Reform Commission in 1997 and as a member of the United Nations Committee on the Elimination of Discrimination against Women in 2000.

“I look forward to working closely with Ms Migiro in helping African countries reduce their AIDS dependency and provide universal access to HIV prevention, treatment, care and support services,” said UNAIDS Executive Director Michel Sidibé. “Her experience and leadership will promote African ownership of the AIDS response at the highest levels and reduce the inequities of people affected by AIDS in the continent.”

Africa remains the continent most affected by HIV. In 2010, about 68% of all people living with HIV resided in sub-Saharan Africa. The region also accounted for 70% of all new HIV infections worldwide.

Thursday, July 12, 2012

WANAFUNZI KUTOKA UN CLUBS KUIWAKILISHA TANZANIA KONGAMANO LA MANDELA AFRIKA KUSINI.


Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa nchini (UNDP) Bw. Phillippe Poinsot akimkabidhi barua Mwanafunzi wa kidato cha nne wa Shule ya Sekondari Azania Rahim Rajab ambaye ni mmoja wa kati ya wanafunzi wawili wajumbe wa UN Clubs waliochaguliwa kuhudhuria Kongamano la maadhimisho ya siku ya kuzaliwa Rais wa Zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela litakalofanyika Johannesburg Afrika Kusini ambayo huadhimishwa kila mwaka Julai 18.

Wanafunzi hao wamepewa duhamini wa Tiketi za kwenda na kurudi na Shirika la Ndege la Afrika Kusini (South African Airways-SAA).
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa nchini (UNDP) Bw. Phillippe Poinsot akimkabidhi barua ya kuchaguliwa kushiriki Kongamano hilo Afrika Kusini Mwanafunzi wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa Nuru Kessy ambaye ni Mwanachama wa Un Clubs.
Bw. Phillippe Poinsot (kulia) akimfafanulia Mwanafunzi Nuru Kessy kuwa katika Kongamano hilo watakutana na wanafunzi wenzao kutoka mataifa mbalimbali duniani wenye umri kati ya miaka 13-18 na kuwa wanahitaji kufanya utafiti kuhusiana na maisha ya Mandela ikiwemo miaka ya mwanzo, maisha yake ya jela, maisha ya uraisi kama mtu aliyepokea tuzo ya Amani ya Nobel, kustaafu kwake na mchango wake kama kiongozi maarufu duniani.
Wanafunzi hao wakitoa shukrani kwa Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa nchini (UNDP) Bw. Phillippe Poinsot (kulia) na Head, Management Support Strategy and Partnership wa UNDP Ishmael Dodoo (kushoto).
Wanafunzi ambao ni wananchama wa UN Clubs wanaoelekea Afrika Kusini katika Kongamano la maadhimisho ya siku ya kuzaliwa ya Nelson Mandela kwa udhamini wa shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa UNDP. Kushoto ni Reference Assistant kutoka kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Harriet Macha, IT Associate Alice Chopeta, Head, Management Support Strategy and Partnership wa UNDP Ishmael Dodoo, Wanafunzi Rahim Rajab na Nuru Kessy, Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa nchini (UNDP) Bw. Phillippe Poinsot na Information Officer UNIC Stella Vuzo.

Friday, July 6, 2012

TAARIFA YA UWEKEZAJI YA UMOJA WA MATAIFA YAZINDULIWA DAR ES SALAAM

Pichani Juu na Chini ni Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou akizungumza wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya Dunia ya Uwekezaji 2012 yenye kauli mbiu 'Sera Kuelekea Kizazi Kipya katika Uwekezaji' ambapo amewasisitiza watunga sera wa Tanzania kutumia rasimu ya Sera ya Uwekezaji ya Maendeleo Endelevu kwa mwaka 2012 kama kipaumbele katika kuunda sera za Kitaifa za Uwekezaji. Kushoto ni Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa(UNIC) Bi. Stella Vuzo.
Baadhi ya Maafisa wa Umoja wa Mataifa nchini waliohudhuria uzinduzi wa World Investment Report 2012.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw. Raymond Mbilinyi akiwasilisha Ripoti hiyo ya Mwaka 2012 ambapo amezungumzia zaidi mazingira ya uwekezaji Tanzania huku akigusia mwelekeo, changamoto na fursa zinazopatikana.

Bw. Raymond Mbilinyi ameweka wazi kuwa mujibu wa Ripoti hiyo Tanzania kwa sasa imepiga hatua katika kuboresha miundo mbinu haswa ya Barabara miongoni mwa nchi za Afrika Mashariki.
Dkt. Alberic Kacou (kushoto) na wadau wakifuatilia uwasilishwaji wa Ripoti ya Fursa za Uwekezaji 2012.
Pichani ni Minongoni mwa Mabalozi, wawakilishi wa Serikali, wakuu wa mashirika ya Maendeleo, wawakilishi wa mashirika ya kijamii katika uzinduzi huo.
Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Stella Vuzo akimkaribisha Dkt. Kacou na Bw. Mbilinyi (hawapo pichani) kuzindua rasmi 'World Investment Report 2012'.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw. Raymond Mbilinyi (kulia) akikata utepe kuzindua kitabu chenye Ripoti ya Uwekezaji ya Kimataifa 2012 sambamba na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou.
Sasa imezinduliwa rasmi.
Mkurugenzi wa Zamani wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania Bw. Emmanuel Ole Naiko akitoa maoni yake kuhusiana na Ripoti ya Kimataifa ya Uwekezaji 2012.
Pichani Juu na Chini Wadau wa Sekta ya Uwekezaji, Maafisa wa Umoja wa Mataifa, Mabalozi pamoja Wawakilishi wa Idara mbalimbali za Serikali waliohudhuria Uzinduzi huo.
Pichani ni Minongoni mwa Mabalozi, wawakilishi wa Serikali, wakuu wa mashirika ya Maendeleo, wawakilishi wa mashirika ya kijamii katika uzinduzi huo.
Dkt. Alberic Kacou na Mkurugenzi wa Zamani wa kituo cha Taifa cha Uwekezaji chini Bw. Emmanuel Ole Naiko wakipeana mkono wa Pongezi baada ya kuzindua Ripoti ya Kimataifa ya Uwekezaji 2012.
Dkt. Kacou akibadilishana mawazo na wageni waalikwa baada ya uzinduzi huo.
Bw. Emmanuel Ole Naiko (kulia) na Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa hapa nchini (UNDP) Bi. Louise Chamberlain wakijadili kuhusu umuhimu wa matumizi ya Ripoti za Uwekezaji katika kukuza uchumi wa nchi.
--
The launch of the 250 page report was paperless and participants to the event were given CD-ROM's by UNIC. However, to get copies of this book, you can contact The United Publications Sales and Marketing Office, 300 E 42nd Street, 9th Floor, IN-919J New York, NY 10017, United States. tel.: +1 212 963 8302, fax: +1 212 963 3489, e-mail: publications@un.org, https://unp.un.org. Price: US$ 95 with a 50% discount for residents of developing countries, and 75% discount for residents of least developed countries(including Tanzania). This price is for a copy of the printed Report and an accompanying CD-ROM. If you would like to order the printed report separately from the CD ROM please indicate.
Contacts:
UNCTAD Communications and Information Unit, +41 22 917 5828, +41 79 502 43 11, unctadpress@unctad.org, http://unctad.org/en/pages/Media.aspx or in Tanzania you may contact: stella.vuzo@unic.org for further assistance.

Wednesday, July 4, 2012

Waziri wa Kazi na Ajira Gaudentia Mugosi Kabaka azungumza Umoja wa Mataifa

Mhe. Gaudentia Mugosi Kabaka ( MB) Waziri wa Kazi na Ajira akizungumza wakati wa mkutano wa Umoja wa Mataifa unaojadilini pamoja na mambo mengine tatizo la ajira na hasa kwa vijana, Mhe. Kabaka anaongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkutano huu wa wiki moja, ukiwashirikisha mawaziri wanaohusika na masuala ya ajira, fedha na uchumi, mambo ya nje , ILO na wanazuoni. katika mchango wake kuhusu changamoto hiyo ya ukosefu wa ajira, Mhe. Waziri Gaudentia Kabaka anasema kama ilivyo kwa nchi nyingine zinazoendelea. Tanzania pia inakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira na kwamba serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kujaribu kulikabili tatizo hilo ambalo limekuwa ni changamoto kubwa kwa mataifa tajiri na maskini pia na ni bomu ambalo limeshaanza kufuka moshi.
Baadhi ya ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano huu unaojadili tatizo la ajira, ni mkutano ambao umeandaliwa na Baraza la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Uchumi na Maendeleo ya Jamii maarufu kama ECOSOC. Walio kaa mbele ni Kamishna. Ahmed Makame Haji, kutoka Tume ya Mipango Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bw. Omar Hamisi Same kutoka Wizara ya Kazi na Ajira, Bi. Aziza J. Ali, Mkuu wa kitengo kinachoratibu misaada, Idara ya Fedha za Nje, Serikali ya Mapinduzi Zanziba na Bw. Humphrey Shangarai, mchumi kutoka Idara ya Sera na Mipango, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
--
Na Mwandish Maalum
Wakati Jumuia ya kimataifa ikiendelea kukuna vichwa kutafuta mbinu na mikakati ya kukabiliana na hatari inayotokana na ongekezo kubwa la ukosefu wa ajira na hususani kwa Vijana. Tanzania inasema kwa kutambua ukubwa wa tatizo hilo imeanza kuandaa mikakati endelevu ya kulikabili janga hilo.
Akizungunza katika siku ya pili ya mkutano unaowakutanisha kwa pamoja mawaziri wanaohusika na masuala ya ajira, wataalamu wa masuala ya fedha , uchumi na wanazuoni. Waziri wa Kazi na Ajira, Mhe. Gaudentia Mugosi Kabaka ( Mb) anasema Tanzania kama ilivyo kwa nchi nyingine zinazoendelea inakabiliwa na tatizo kubwa la ukosefu wa ajira.
Mhe. Waziri Kabaka anaongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkutano wa wiki moja unaofanyika hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa. Mkutano huo ambao umefunguliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon mwanzoni mwa wiki, umeandaliwa na Baraza la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Uchumi na Maendeleo ya Jamii (ECOSOC).
“Kama ilivyo kwa nchi nyingine zinazo endelea duniani, nchi yangu pia inakabiliwa na tatizo kubwa la ukosefu wa ajira na hasa kwa vijana. Na tatizo hili linasababishwa kwa kiasi kubwa na uboreshaji wa elimu yetu hadi ngazi ya elimu ya juu, uboreshani na upanuzi ambazo hauendani sambamba na ongezeko la ajira”.
Amewaeleza wajumbe wamkutano huo kwamba, tatizo la ajira pia lipo zaidi kwa upande wa mijini na hii ni kutoka na wimbi la vijana kuhamia mijini.
“ licha ya kwamba vijana wengi wanahamia mijini na hivyo kuchangia katika ukosefu wa ajira, lakini pia hivi sasa tunashuhudia vijana wale wa vijijini kukoa ajira kutokana na athali za mabadiliko ya tabia nchi , mabadiliko ambayo yamekuwa na athari kubwa kwa upande wa kilimo” akabainisha Kabaka.
Akaitaja baadhi ya mikakati inayofanywa na serikali ya kukabiliana na tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana, kuwa ni pamoja na mpango wa kurasimisha mali za wanyonge ( Mkurabita) ili mali hizo ziweze kutumika kupata mikopo, upanuzi vya vyuo vya ufundi stadi ili vijana waweze kujiajiri wenyewe, na kuanzishwa pamona na mambo mengine sheria ya hifadhi ya jamii, mifuko ya jamii, mifuko ya bima ya afya, na vyama vya ushirika vya kuweka na kukopa ( SACCOS)
Aidha akasema, serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ziwamo taasisi za kitaifa na kimataifa, imekuwa ikiratibu mafunzo mbalimbali yakiwamo ya uwezeshaji katika eneo la kilimo ili vijana wawe kujiajiri katika eneo hilo na kwamba mipango yote inalenga katika kufanikisha utekelezaji wa malengo ya maendeleo ya millennia.
Aidha akasema, Tanzania pia inaendelea na jukumu la kuhakikisha kwamba ajira kwa watoto inakomeshwa, kuwapo kwa ajira zenye tija, endelevu na zenye hadhi na kwa sababu hiyo akauomba Umoja wa Mataifa kupitia ECOSOC, kuisaidia Tanzania katika eneo la teknolojia.
Mada kuu ya mkutano huu ni kukuza uwezo wa uzalishaji wa ajira kwa vijana, na kazi zenye heshima kwa lengo la kuondokana na umaskini na kukuza uchumi endelevu ili kufikira utekelezaji wa MDGs.
Mkutano huo unatoa fursa kwa nchi wanachama wa UMum kujadiliana na kubadilishana mawazo kuhusu masuala ambayo ni changamoto kubwa kwa usalama wa dunia. Na hususani wimbi hilo la ukosefu wa ajira kwa vijana, wimbi ambalo limesha onesha kwamba lisipotafutiwa mikakati ya kudumu ni bomu ambalo tayari limeshaanza kufuka moshi.

Monday, July 2, 2012

UMOJA WA MATAIFA KATIKA MAONESHO YA SABA SABA

Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Hoyce Temu akitoa maelezo kwa mmoja wa wananchi walio telea Banda hilo leo.



Maonesho ya kimataifa ya biashara Dar es Salaam (DITF) maarufu kama Saba saba yameanza Juni 28, 2012 katika viwanja vya Maonesho vya JK Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam.

Wafanyabiashara wa ndani na nje ya Tanzania wanashiriki maonesho hayo makubwa Tanzania, huku serikali na taasisi zake nyingi zikiwa moja ya washiri katika maonesho hayo yanayoratibiwa na Mamlaka ya Maendeleo ya biashara Tanzanaia.

Pia taasisi za Kimataifa na mashirika makubwa duniani yanashiriki maonesho hayo, miongoni mwa mashirika hayo ni Umoja wa Mataifa ambao upon a taasisi zake zote zaidi ya 21. UN Tanzania wapo katika Banda la Ali Hassan Mwinyi na elimu mbalimbali juu ya Umoja huo wa Mataifa ambao Tanzania ni mwanachama wake unapatikana.
Afisa habari wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) Austin Makani akiwa na Afisa Habari wa Umoja wa Umoja wa Mataifa (UN) Hoyce Temu.
Mjasiriamali, Bi Magreth Msuya kutoka Kikundi cha MATA Woman Group cha Tabata jijini Dar es salaam ni moja ya watu wanaofaidika na UN, na hapa anashiriki maonesayo ndani ya Banda la UN. Kulia ni mteja anaeangalia bidhaa zake na kto ni Afisa Habari wa UN Tanzania, Hoyce Temu.
Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Hoyce Temu akitoa maelezo kwa wananchi walio telea Banda hilo leo.
Banda la umoja wa Mataifa.

Thursday, June 14, 2012

Wafanyakazi Wa Umoja wa Mataifa Wachangia Damu Dar Es Salaam

Mshauri Mkuu wa Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Bw. Christopher John Ozga (kushoto) akiwa katika zoezi la kuchangia damu ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya uchangiaji damu duniani. Aliyesimama ni Afisa kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama Bw. Deochris Kaimukilwa.
Mshauri Mkuu wa Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Bw. Christopher John Ozga akifanyiwa vipimo na Bw. Deochris Kaimukilwa baada ya kujitolea damu.
Mtangazaji wa Radio France International (RFI Kiswahili) Emmanuel Makundi akifanya mahojiano na Bw. Hashim Mahige wakati wa zoezi kuchangia damu lililofanyika katika Ofisi za shirika la Afya Duniani (WHO) jijini Dar es Salaam ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya uchangiaji damu duniani.
Ramadhani Ndimba kutoka NASP .
Charles Lutandula wa (WHO) katika zoezi la uchangiaji damu.
Charles Lutandula wa WHO akifanyiwa vipimo vya awali na Mtaalamu kutoka mpango wa Taifa wa Damu Salama Bi. Edith Senga kabla ya kuchangia damu.


Monday, June 4, 2012

Regional Integration and Human Development: A pathway for Africa

The report discusses four main channels linking integration and human development: income; access to services, empowerment, and sustainability. It assesses how factors common to many countries might condition the impacts of regional integration on human development. This qualitative analysis is supplemented with simulations of regional integration processes within Africa and beyond.

http://www.undp.org/content/dam/undp/library/Poverty%20Reduction/Trade,%20Intellectual%20Property%20and%20Migration/RIR%20English-web.pdf

Popular Posts