Pages

Showing posts with label UDAKU UMBEYA GOSIP. Show all posts
Showing posts with label UDAKU UMBEYA GOSIP. Show all posts

Saturday, July 28, 2012

MACHANGUDOA WACHAPWA VIBOKO

WATUMIA BAJAJ
Kwa mujibu wa shuhuda wetu, waumini hao, wakiwa wamevaa kanzu huku wakitembea na bakora mkononi walichukua jukumu la kukodi Bajaj na kuzunguka maeneo mbalimbali jijini inapofanyika biashara hiyo haramu ya ukahaba.
BARABARA YA SHEKILANGO
Vijana hao waliolenga kukomesha biashara hiyo hasa kipindi hiki cha mfungo walianzia kwenye Barabara ya Shekilango inayokatiza kwenye viunga vya Sinza, Dar ambapo kila kituo cha daladala kuanzia Afrika Sana hadi kwenye mataa ya Shekilango waliwakuta machangu na kuwatandika viboko kabla ya kutua mitaa ya Mwenge.
KINONDONI
Baada ya kufagiafagia Sinza kwa kuwaadabisha wanawake hao ndipo zoezi likahamia mitaa ya Kinondoni ambapo nao walipokea bakora za kutosha huku wengine wakitoka nduki.

KISA KUHARIBIWA SWAUMU
Kwa mujibu wa vijana hao, walifikia hatua ya kufanya zoezi hilo baada ya muumini mmoja wa kiume kukatiza maeneo ya Corner Bar, Afrika Sana na kuvutwa kisha kuchezewa nyeti na makahaba na kusabisha kuharibika kwa swaumu yake.
Ilielezwa kuwa baada ya kukutwa na kimbembe hicho, ilibidi muumini huyo kukatiza safari yake ya kwenda kuswali msikikini mishale ya saa 2:00 usiku.

Ilisemekana kuwa aliporudi nyumbani alitawadha na kufunga safari nyingine ya msikitini na alipofika kwenye nyumba hiyo ya ibada ndipo akawasimulia waumini wenzake ambao nao walikasirishwa na kitendo hicho hivyo wakapanga kuvamia maeneo yote ya biashara hiyo ili kuwashikisha adabu.
Waandishi wetu, wakiwa kwenye mishemishe zao za kutafuta habari mishale ya saa 5 usiku waliwashuhudia waumini hao wapatao saba wakishuka kwenye Bajaj nyeusi maeneo ya Sinza wakiwa na bakora mikononi kisha kuwavaa machangu hao na kuwatandika.
Wakati wakitekeleza zoezi hilo, jamaa hao walisikia wakiwaambia: “Sisi tupo kwenye swaumu nyiye mnatutega, ala!”
HAWAHESHIMU MWEZI MTUKUFU?
Waumini hao waliongeza kuwa makahaba hao wamekuwa hawaheshimu mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan ndiyo maana wanaendeleza biashara yao hiyo ya aibu.

Wednesday, July 18, 2012

FUMANIZI BABKUBWA


Richard Bukos na Issa Mnally

USIOMBE yakukute! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya kusikia kisa cha aliyewahi kuwa mpenzi wa mwanamuziki wa TAKEU, Nice Lucas Mkenda ‘Mr. Nice’, Lulu John (mwenye blauzi nyekundu) anayedai kumfumania mumewe (siyo Mr. Nice), Risasi Mchanganyiko linafunguka.

Lulu alidai kumfumania bwana’ke Abdulatif Salum na mwanamke ambaye jina halikupatika kwenye gesti moja iliyopo Kinondoni B jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita.



SINEMA ILIKUWA HIVI
Kwa mujibu wa Lulu, akiwa kwenye mihangahiko ya kusaka bingo, alitonywa na mtu wake wa karibu kuwa mumewe Abdulatif yupo kwenye nyumba hiyo ya wageni akiigagadua amri ya sita nje ya mkataba.

Lulu, baada ya kuthibitishiwa kuwa mumewe anacheza ‘nje kapu’ ndipo akakodi bodaboda fasta na kuwahi eneo la tukio kwani naye siyo mgeni wa uwanja huo wa mechi za kitandani.
Alidai kuwa ilimchukua dakika 12 tu kutoka Kijitonyama, Dar anakoishi na mumewe hadi eneo la tukio.



MPAKA CHUMBANI
Aliendelea kusema kuwa baada ya kutimba mahali hapo alikwenda moja kwa zote hadi kwenye chumba walichojichimbia wawili hao na kuanza kubamiza mlango huku akipiga mayowe ya kuomba msaada.



WENGINE WADHANI WAMEFUMANIWA
Huku akizidisha kupiga kelele akitaka kuvunja mlango, ndipo akakatiza stimu za watu wengine waliokuwa wakilimega tunda tamtam kwenye vyumba vingine ambao walitoka kwa kihoro wakidhani wamefumaniwa wao.



MUME ATIMKA NA NGUO YA NDANI
Aliendelea kusimulia mkasa kuwa watu walianza kujaa nje ya chumba hicho ndipo Abdulatif akafungua mlango kwa kasi na kutimka kama mkizi akiwa na nguo ya ndani pekee kisha akaruka fensi.



WATU WEWEEE!
Alisema kuwa wakati anachomoka nduki alimgonga kikumbo Lulu na kumwangusha chini huku akimwacha akigaragara ambapo watu walikuwa wakimkimbiza wakisema: “Weweee.”


VITA
Baada ya kunyanyuka na Abdulatif kumchomoka hivihivi ndipo vita kuu ikaanza dhidi ya mgoni wake.



ANG’ATWA PUA
Alisema kuwa ngumi za uhakika zilipigwa hadi yeye (Lulu) akang’atwa pua ambapo alitokwa na damu chapachapa usoni huku aliyefumaniwa akitafuta njia ya kujisitiri baada ya kuchaniwa nguo na kubaki mtupu.

Baada ya hali kuwa mbaya, Lulu alisema walitokea wasamaria wema na kuwatuliza ambapo yeye alikimbilia Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Kinondoni na kumfungulia mgoni wake shitaka la shambulio la kudhuru mwili lenye jalada la kesi namba OB/RB/12675/2012.

Kwa mujibu wa Lulu, kitendo cha kumfumania mwanaume huyo kimemuumiza kwani amekuwa akimtunza kwa hali na mali na hakuweza kuamini kama angeweza kumsaliti.
Juhudi za kumpata Abdulatif hazikuzaa matunda hadi gazeti hili linakwenda mitamboni hata hivyo zinaendelea.



KWA NINI USIOMBE YAKUKUTE?
Lilikuwa ni tukio la aina yake ambalo halikuishia pale gesti tu bali liliingia mtaani ambapo vitendo vya Abdulatif kukimbia akiwa mtupu na Lulu kung’atwa pua viligeuka gumzo na kila mtu akimuomba Mungu asikutwe na kasheshe kama hilo.

Popular Posts