Translate - Tafsiri
Labels
- Tamko kwa Umma - Press Release
- All Photos - Picha
- CCM CHAMA CHA MAPINDUZI
- Zanzibar
- IKULU - STATE HOUSE
- Sports - Michezo
- CHADEMA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO
- Dodoma
- Editorial Opinion - Maoni Tahariri
- Tanzania
- Dar es salaam
- Habari za Kimataifa - International News
- Burudani - Entertainment
- Bungeni
- Katiba - Constitution
- Dini - Religion
- Mbeya
- SMZ Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
- Vodacom
- Hotuba - Speech
- Arusha
- Iringa
- Tanzia - Msiba - Mazishi
- Afya - Health
- Ofisi ya Waziri Mkuu
- Singida
- Ajali - Accident
- Development Reports
- Morogoro
- Open Letters - Barua za Wazi
- Urembo - Beauty
- Kenya
- CUF Chama cha Wananchi
- Maonyesho ya Sabasaba
- Ofisi ya Makamu wa Rais
- Huduma za Usafiri - Transport Services
- Tanga
- Business Finance Money
- Masuala ya Elimu - Education
- Miundombinu -Infrastructure
- Mtwara
- Rukwa
- UVCCM
- Habari za Mahakamani
- Kilimanjaro
- Serengeti Breweries Limited
- Tourism - Utalii
- Habari za Nyumbani - Local News
- Jakaya Mrisho Kikwete
- Kagame Cup - Kombe la Kagame
- Katavi
- Lindi
- Nishati - Madini - Mining - Energy
- UN United Nations - Umoja Mataifa
- Yanga
- African Union - Umoja wa Afrika
- Bagamoyo
- Agriculture - Kilimo
- Azam FootBall Club
- Balozi na Ofisi za Balozi
- Baraza la Wawakilishi
- Human Rights - Haki za Binadamu
- Jeshi la Polisi Tanzania
- Kigoma
- Maonyesho ya Nane Nane
- Simba Sports Club
- Tabora
- East African Community
- HARUSI - WEDDINGS
- Kagera
- Mwanza
- Pemba
- Shinyanga
- Sumbawanga
- TFF Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania
- Videos - Multimedia
- Wizara ya Mambo ya Nje Na Ushirikiano wa Kimataifa
- Wizara ya Nishati na Madini
- Afdb African Development Bank
- Airtel Tanzania
- Benki - Fedha - Uchumi
- Fiesta 2012
- GEITA
- Mafuta - Oil Issues
- Uganda
- Wizara ya Maliasili na Utalii
- BAJETI 2012 - 2013
- Burundi
- Climate Change - Mabadiliko ya Tabia Nchi
- FASHION - MITINDO - MAVAZI
- ICT Information and communications technology
- Kambi ya Upinzani
- London Olympic Games 2012
- Mambo ya Zamani - Archives
- Maonyesho ya Biashara - Trade Shows
- Mara
- Mobile - Telecoms
- NHIF National Health Insurance Fund
- Peace and Security
- Rwanda
- Sayansi na Tekinolojia
- Wizara ya Elimu na Ufundi
- Wizara ya Mambo ya Ndani
- Wizara ya Uchukuzi
- Zambia
- BOT Bank of Tanzania Benki Kuu ya Tanzania
- Events - Matukio
- Habari za Majimboni
- Mahojiano - Interview
- Makala - Articles
- Malawi
- Mkoa wa Pwani
- Musoma
- NJOMBE
- National Parks - Mbuga za Wanyama
- Ruvuma
- SONGEA
- Shirika la Nyumba laTaifa - NHC
- TBL Tanzania Breweries Limited
- Taifa Stars - Timu ya Taifa
- UDAKU UMBEYA GOSIP
- US EMBASSY - UBALOZI WA MAREKANI
- University of Dar es salaam - Chuo Kikuu cha Dar es salaam
- ABG African Barrick Gold
- BAKWATA
- Banks - Benki
- Environment - Mazingira
- Ilala
- Kilimo Kwanza
- Land and Land Grabbing Issues - Ardhi
- Love Relationships - Mapenzi Mahusiano
- MIKUTANO
- Mabondia - Boxing
- Manyara
- Miradi ya Maendeleo
- Misaada - Donations
- Mombasa
- NCCR MAGEUZI
- Nairobi
- People - Watu
- Picha ya Wiki - Photo of the Week
- Precision Air
- Procurement
- Ripoti Maalumu
- SANAA - ARTS
- Sensa ya Makazi na Watu 2012
- Sheria - Law
- Somalia
- South Africa
- South Sudan - Sudani Kusini
- Takwimu - Statistics
- Tigo
- Travel - Safari
- Ugaidi - Terrorism
- Ulinzi na Usalama - Security and Defence
- Wizara ya Afrika Mashariki
- Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
- Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo
- Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Teknologia
- Wizara ya Viwanda na Biashara
- Zimbabwe
Blog List
Friday, August 3, 2012
MGOMBEA NAFASI YA MAKAMU MWENYEKITI WA UMOJA WA VIJANA (UVCCM) TAIFA- SANGOGUNGU KASERA
HOTUBAYA MGOMBEA NAFASI YA MAKAMU MWENYEKITI WA UMOJA WA VIJANA (UVCCM) TAIFA- SANGOGUNGU KASERA
2August 20112
Ndg:Wanahabari
Ndg: wanaUVCCM wenzangu
Kwa heshima na unyenyekevu mkubwa naomba kutoa salamu zangu za dhati kwa Watanzania na vijana wenzangu wanchi hii pamoja nanyi waandishi wa Habari kwa kushiriki nami katika safari hiiinayolenga kuunganisha na kujenga hatua za mabadiliko ya maisha ya Vijana waTanzania. Kwa namna ya pekee kabisa niwashukuru na kuwaomba mshikamano vijanawenzangu wa Chama cha Mapinduzi ambao kupitia kwao ninatumia nafasi hii kuomba ridhaa yao ili nipate nafasi ya kuwa chemchem ya mafanikio na mabadiliko katika maisha yetu kwa kuanzia na chama chetu. Leo hii naungana na vijana wenzangu hawa wa ndani ya CCM, kufanya jambo moja kubwa, jambo la kuchukua fomuya kuwania moja ya nafasi kubwa katika jumuiya ya Vijana wa CCM Tanzania. Ninafanya kazi hii leo nikitambua mambo yafuatayo:
Kwanza, ninalenga kuleta mabadiliko yanayotazama aina ya vijana tuliopo sasa, aina ya maisha tunayoishi na aina ya changanoto zinazotukabili mimi nikiwa mmojawapo.
Pili kwa upekee mkubwa, nachukua fomu hii nikibaini hali ya vijana huko tulikotoka na , changamoto tulizopitia na hatari inayotukabili mbele kama hatua stahiki hazitaanza kuchukuliwa na vijana wa aina yangu ambao tuna uzoefu wa kutosha wa maisha ya kawaida ambayo yanahitaji nguvu na akili zetu na za wenzetu waliotutangulia katika kuboresha maisha yetu ili tuweze kuwa raia wema katika nchi yetu na wanachama waadilifu wa chama chetu na jumuiya zake.
Ndugu Waandishi wa Habari;
Kazi hii ya kuchukua fomu ninayoifanya leo hii na kisha kuanza zoezi la kutafuta kuungwa mkono. Ni kazi inayohitaji ushirikiano mkubwa kwa uongozi wa Jumuiya yetu pamoja na vijana mbalimbali bila kujali itikadi zao za vyama vya siasa. Nasema hivi kwa kutambua kuwa UVCCM ndiyo Jumuiya pekee yenye kubeba taswira na matarajio ya vijana wa Tanzania na ambayo siku zote inatakiwa kusimamia maslahi na matakwa ya vijana wa Tanzania na kwakuwa jumuhia hii ni jumuhia ya chama kinachoongoza si chama tawala .
Ndugu zangu wanahabari na wana CCM tunafahamu tofauti kati ya kuongoza na kutawala ndio maana nimetumia neno kuongoza, na Kama kazi hii ilikuwa haifanyiki huko nyuma na kama ilifanyika bila kuridhisha, mimi nimeamua kwa moyo mkunjufu kuingia kuonesha namna jumuiya yetu itakavyoweza kuwatumikia vijana wa Tanzaniana kukiboresha chama cha Mapinduzi ili kitambue wajibu wake kwa vijana wote waTanzania na kwa kufanya hivi kiweze kusimamia misingi iliyolijenga Taifa hili na kuachwa na waasisi wa Taifa letu Hayati Baba Wa Taifa na Hayati Rais Karume ambao walilijenga taifa letu katika misingi ya haki, usawa na ustahimilivu.
Ndugu wana habari; Katika kipindi hiki chakutafuta nafasi ya kuteuliwa kuwa mgombea wa nafasi hii nitabakia kuongozwa na Moto isemayo: Vijana kwanza kwa taifa lenye amani na maendeleo. Bila vijana kuangaliwa na kupewa yale wanayostahiki, ni wazi taifa lenye amani na maendeleo halitakuwepo. Natambua fika kuwa vijana wa Tanzania wanakabiliwa na changamoto kubwa hasa ile inayolenga kubaini ndoto ya maisha yao ya sasa na siku zijazo. Naamini mimi ni mmoja wa vijana hawa ambaye pia ninahitaji kuona vijana walio katika kilimo basi wanaweza kupata soko la mazao yao. Vijanawabeba mikokoteni nao wanafanya kazi hiyo kwa miaka kadhaa na kisha kuboreshaajira zao.
Vijana wanaosoma basi wanahitimu vema na kupata ajira wanazostahiki na pia walio makazini na waliopata nafasi za kuongoza wanaonesha mfano wakufanya kazi kwa kujituma na kwa bidii ili kuonesha kuwa vijana tunaweza na hatuwezi kuliangusha taifa. Natambua haya ninayoyazungumza ni mambo magumu lakini pia natambua yanahitaji mbinu nyingi ili kukabiliana nayo. Kwa sasa natumia nafasi hii kukiomba Chama changu, kuiomba Jumuiya Yetu ya Vijana kutambua kuwa nina dhamira, nina nia, nina sifa za kutosha, nina uwezo wa kufanya majukumu haya ninayoyaomba na ninafahamu kazi za majukumu haya.
Tena nina rekodi katika umri wangu huu wa kufanya mambo ya kutukuka ambayo rekodi yake inaweza kutazamwa pote nilipobahatika kutoa utumishi wangu. Kwa namna isiyoonyesha kuyumba naomba kuwaeleza vijana wenzangu kuwa kutokanana mshikamano wa vijana wenzangu kwangu ni wazi tumejiandaa kushinda katika nafasi hii ili tuweze kuleta mwanga wa mabadiliko katika jumuiya yetu na chama chetu katika maandalizi ya chaguzi zijazo. Ndugu wanahabari ninatambua zipo changamoto nyingi zinazoikabili UVCCM na changamoto hizi zinahitaji kiongozi ambaye atakuwa na uthubutu wakuweza kukabiliana nazo, changamoto kuuni kitaswira, kimuundo, kiimani, kimadhumuni kama ambavyo zimehainishwa kwenyekanuni za ummoja wa vijana. Nina maanisha nini ninapozungumzia taswira ya UVCCM.Taswira ya UVCCM Taifa leo siotaswira ya kimapambano.
Historia yetu ipo wazi jumuiya ya vijana ilishiriki katika mapambano ya kuleta Uhuru, Umoja na mshikamano mtakumbuka wakati TANU Inahangaika na kutafuta Uhuru wa Tanganyika na Afro-Shirazi party ikipambana kuleta Uhuru wa Zanzibar vijana waliunganishwa na jumuiya za umoja wa vijana wa vyama hivi viwili ambavyo ni TANU YOUTH LEAGUE na ASP YOUTH LEAGUE, zinafahamika kazi zilizofanywa na wabeba mizigo wa Kariakoo mfano Mzee Rajabu Diwani, leo UVCCM sio tena yawabeba mizigo, sio tena ya wamachingasio tena ya wakulima ,sio tena jumuiya ya wafanyakazi ni jumuiya ya wafanyabiashara, watoto wa vigogo ama wenyenasaba nao ama rafiki zao, inahitaji viongozi wenye dhamira ya dhati ambao watarudisha jumuiya hii kwa vijana wakitanzania na kurudisha taswira ya kimapambano ambayo ni mapambano ya kiuchumi, kazi ya Uhuru imeshafanyika imebakia jukumu la kuleta Uhuru wa kiuchumi na kuwa kimbilio la vijana wote.
Ni dhamirayangu ya kugombea nafasi hii ni kuhakikisha awamu ya pili ya mapambano ya kiuchumi ya umoja wa vijana inaanza rasmi. Nafahamu zipo changamoto za kiutawala, kiuchumi na jumuiya kuendelea kuishi kwa kutegemea misaada na Ruzuku kutoka kwenye chama, nafahamu watendajiwana hali mbaya kiuchumi hasa katika mawilaya, nafahamu ofisi zetu za wilaya zina upungufu wa vitendea kazi ni dhamira yangu kubadili mwelekeo wa utendajiwa jumuiya yetu kutoka “Business as usual” kuvalisha skafu viongozi na kuimba nyimbo, kuwa jumuiya yenye dira namwelekeo sahihi wa kuwaunganisha na kumkomboa kijana wa kitanzania.
Ndugu waandishi wa Habari; Ninafahamu matarajio yavijana wa kitanzania yatafikiwa kupitia CCM imara na CCM inatokana na uimara wajumuiya zake kuwa imara na hili inawezekana kwa kupatikana viongozi Imara na mimi nina amini ni mmoja waviongozi ambao wataifanya jumuiya yetu kuwa Imara.
Kwa kuhitimisha Hotuba yangu naomba kutoa shukrani zangu kwa Mwenyezi Mungu kwa kunifanikisha kuwananyi hapa, niwashukuru wana familia yangu, marafiki na nyie ndugu zanguwaandishi wa Habari kwa kukubali kujumuika nami kunisikiliza leo. Niwaombe Vijana wenzangu wa CCM kuniunga mkono katika azma hii kubwa niliyo nayo na niwakumbushe tu kuwa, zoezi hili la kuchukua fomu nililofanya hapa leo si langu bali la vijana wote wa Tanzania wakiwakilishwa na Vijana wa Chama cha Mapinduzi.
Ni imani yangu kuwa, wana UVCCM hawatakubali kuangusha taa hiiwaliyoiwasha kule Rorya mkoa wa Mara wao wenyewe na badala yake wataungana namibega kwa bega ili kuufikia ushindi. Tutapitisha fomu hii pamoja nao, tutachujwa pamoja nao na kisha tutashinda pamoja nao na kisha kuanza kuwaongoza vijana wa Tanzania pamoja nao. Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehma atubariki na kutupa nguvutufanikishe azma hii muhimu pamoja. Kidumu Chama cha Mapinduzi
Asanteni kwa kunisikiliza.
Mimi Ndg Sango Gungu Kasera- Mjumbe Mkutano Mkuu UVCCM (W) Rorya
Kauli mbiu Mbiu “Vijana kwanza kwa taifa lenye amani namaendeleo’’.
Tuesday, July 10, 2012
Four Seasons Sets Up Camp in Tanzania’s Serengeti National Park
“We have long wanted to expand into Sub-Saharan Africa and offer new outdoor adventure experiences to our guests,” says Kathleen Taylor, president and CEO,
“It’s great to be back in Africa, where each day brings a new wonder,” says Kostecky, an avid photographer with a keen sense of adventure. “This Lodge will be an excellent opportunity for first time safari travellers, families and groups to experience the natural beauty, astounding wildlife and fascinating culture of the Serengeti.”
Development in Africa and Other Ecologically Sensitive Regions
“This is the first step in a bold development project that will see three diverse
As with the company’s award-winning
About
A UNESCO World Heritage Site, Tanzania’s Serengeti National Park covers 14,763 square kilometres (5,700 square miles). The landscape features the largest concentration of plains animals in Africa, and is acclaimed for the best game drives and abundant year-round wildlife, including the famous migrating herds of wildebeest, zebra, antelope and gazelle as well as lions, leopards, cheetahs, elephants, buffalo, rhinoceros, hippopotamuses, crocodiles and abundant birdlife.
Sunday, June 24, 2012
SAFARI YA MWISHO YA MHARIRI WILLY EDWARD OGUNDE
Popular Posts
-
South Sudan Vice-President to attend Business and Security Forum The Vice-President of South Sudan, HE Dr Riek Machar, will join senior mini...
-
Tarehe 6 mwezi wa Aprili, 2012, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushauriana na kukubaliana na Rais wa Zanzibar, aliunda Tume ya ...
-
Baraza la Madaktari Tanganyika limepokea malalamiko kutoka kwa Katibu Mkuu , Wizara y a Afya na Ustawi wa Jamii kwamba , baadhi ya Madakt...
-
RIPOTI YA TUME YA KUCHUNGUZA AJALI YA KUZAMA M. V. SPICE ISLANDER I SEHEMU YA KWANZA UTANGULIZI 1.1 CHIMBUKO Usiku wa kuamkia tarehe 10...
-
This statement outlines how we handle any personal information we obtain PataHabari is committed to respecting and protecting the privac...
-
1. MWENYEKITI TAIFA 1 Asila Ali SALIM 2 Jamal K. ALI 3 Lulu Mcham ABDALLAH 4 Lusekelo W. MALEMA 5 Mbarouk M. MBAROUK 6 Mwana Amina Haji FARU...
-
Usomi wa ngazi mbalimbali si sifa ya mtu kufaa kuwa kiongozi, dunia katika historia yake ina majina lukuki ya baadhi ya viongozi ambao wa...
-
YAH: UTEUZI WA KUJAZA NAFASI YA UONGOZI KATIKA WIZARA YA UCHUKUZI Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Eng. Omar A. Chambo kwa Mamlaka a...
-
Mwananchi wa Kijiji cha Jambiani akiwasilisha maoni yake kwa njia ya Barua kwa Tume. Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wak...
-
Wachezaji wa timu ya mashabiki wa timu ya Manchester City ya Uingereza wakichuana vikali na mchezaji wa timu ya mashabiki wa timu ya Real...