Pages

Showing posts with label All Photos - Picha. Show all posts
Showing posts with label All Photos - Picha. Show all posts

Sunday, November 11, 2012

MKUTANO WA NEC - CCM MJINI DODOMA LEO


Meza Kuu ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete (wa nne kulia) wakati Mkutano Mkuu wa Nane wa NEC - CCM ukiendelea ndani ya Ukumbi wa Kizota mjini Dodoma leo.
Kapteni John Komba akiimba mbele ya wajumbe kutoka mikoa mbalimbali

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye akiongoza Mkutano Mkuu wa Nane, katika Ukumbi wa Kizota mjini Dodoma leo.
Ukumbi wa Kizota ukiwa umefurika wajumbe kutoka kona mbalimbali.

Ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)na Hotel za Hadhi ya Nyota Tano Eneo la Makulu Mjini Dodoma


 Picha zinazoonyesha Michoro ya Ukumbi,Ofisi za Makao makuu na Hotel ya nyota tano.

Thursday, November 8, 2012

UBORESHAJI WA MIUNDOMBINU MKOA WA DODOMA


 Barabara za katikati ya mitaa ya manispaa ya Dodoma zikiwa zinatengenezwa kwa kiwango cha Lami.
Wajasiriamali wakiwa wameweka biashara zao kwenye moja ya mageti ya makao makuu ya CCM,kipindi hiki cha mkutano mkuu kumekuwa na maongezeko ya mahitaji ya bidhaa za chama bora Tanzania,hivyo kutoa fursa kwa wafanya biashara wengi kuuza bidhaa za chama hicho.Picha na Adam Mzee-Dodoma

Wednesday, October 17, 2012

RAIS WA ZANZIBAR DK ALI SHEIN AWAAPISHA MJUMBE (MBM), NAIBU MAWAZIRI NA NAIBU KATIBU WAKUU WA WIZARA MBALI MBALI IKULU ZANZIBAR


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akimuapisha Mhe,Saidi Mohamed Said,kuwa Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi, wakaati wa  hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar, leo mchana.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akimuapisha CDR Julius Nalimy Maziku,kuwa Naibu Katibu Mkuu  Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Idara Maalum za SMZ katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akimuapisha Bw Juma Ameir Hafidh,kuwa Naibu Katribu Mkuu Ofisi ya Rais (Fedha Uchumi na Mipango ya Maendeleo), katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo. Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akimuapisha Bw Mustafa Aboud Jumbe,kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Makaazi,Maji na Nishati, katika haflailiyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar, leo mchana.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akimuapisha Bw Tahir M. Abdulla,kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano,wakati wa hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar, leo mchana.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akimuapisha Mhe.Shawana Bukheti Hassan, kuwa Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi wakati wa hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, akimuapisha Mhe, Mtumwa Kheir Mbarak,kuwa Naibu Waziri Kilimo na Maliasili,  wakati hafla iliyofanyika Ikulu MjiniZanzibar leo.Picha na Ramadhan Othman,Ikulu-Zanzibar

Monday, September 10, 2012

Rais Jakaya Kikwete Apokea Hati Za Utambulisho Kutoka Kwa Balozi wa Ubelgiji na Qatar

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Ubelgiji hapa nchini Mheshimiwa Adam Koenvaad huko Ikulu tarehe 10.9.2012.
Rais Jakaya Kikwete akifanya mazungumzo na Balozi wa Qatar hapa nchini Mheshimiwa Jassim Mohamed Mubarak Darwesh mara baada ya Balozi huyo kutoa hati zake za utambulisho kwa Rais Kikwete huko Ikulu tarehe 10.9.2012.Picha Zote na John Lukuwi

Friday, September 7, 2012

MAANDAMANO YA WAISLAMU JIJINI DAR ES SALAAM




Rais Jakaya Kikwete Akutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Watu wa China Mheshimiwa Hui Liangya

Rais Jakaya Kikwete akipeana Mkono na Naibu Waziri Mkuu wa China, Hui Liangyu alipomtembelea ikulu, Dar es Salaam.
Rais Jakaya Kikwete akimkaribisha ikulu Jijini Dar es Salaam jana Naibu Waziri Mkuu wa China, Hui Liangyu
--
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete jana, Jumatano, Septemba 5, 2012, amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Watu wa China Mheshimiwa Hui Liangya kuhusu masuala mbali mbali yanayohusu uhusiano kati ya nchi hizo mbili.
Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam mara tu baada ya Mheshimiwa Liangya kuwasili nchini kwa ziara ya siku tatu katika Tanzania kama sehemu ya ziara ya nchi za Afrika, viongozi wote wawili wameeleza kuridhishwa kwao na hali na ustawi wa uhusiano kati ya nchi hizo mbili.
Rais Kikwete ametumia nafasi ya ziara hiyo ya Mheshimiwa Liangya kuishukuru China kwa michango yake katika jitihada za maendeleo za Tanzania.
Amesema Rais Kikwete: ”Jamhuri ya Watu wa China imetusaidia mengi katika jitihada zetu za maendeleo kuanzia kwenye ujenzi wa Reli ya TAZARA, ujenzi wa Uwanja wa Taifa, ujenzi wa Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere, ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Dar Es Salaam, ujenzi wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, na ahadi ya kusaidia kuanzisha Benki ya Kilimo Tanzania. Kwa hakika Jamhuri ya Watu wa China imetusaidia mengi na tunaishukuru sana.”
Rais Kikwete pia ameitaka China kuendelea kuisaidia Tanzania hasa katika maeneo ya jinsi ya kuongeza kasi ya uchumi. “Tunataka kwa kweli kujifunza kutoka mifano ya mafanikio ya marafiki zetu wa karibu kama China. Hivyo, bado tunaendelea kusisitiza ushirikiano wa China katika kuanzisha na kuendesha maeneo maalum ya uzalishaji –Special Economic Zones “
Naye Mheshimiwa Liangya amemwambia Rais Kikwete kuwa China itaendelea kuimarisha uhusiano wake na Tanzania ambao umekuwa unashamiri tokea ulipoanzishwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na Mwenyekiti Mao Tse Dung.
Mheshimiwa Liangya amesema kuwa undani wa miradi yote ambayo China inasaidia katika Tanzania ungejadiliwa kwenye mkutano kati yake na Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda katika mazungumzo rasmi yaliyofanyika baada mchana wa jana
Kiongozi huyo wa China pia ameisifu Serikali ya Mheshimiwa Kikwete kwa uamuzi wake wa kuanzisha Mpango wa Maendeleo wa Miaka mitano na kuongeza kuwa mpango huo umeandaliwa kwa umakini mkubwa. “Nawapongezeni kwa uamuzi wenu wa busara wa kuanzisha tena Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano. Ukitekelezwa vizuri unaweza kusukuma kwa kasi zaidi maendeleo ya nchi yetu.”


Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.

5 Septemba, 2012

Monday, September 3, 2012

Tamasha la Serengeti Fiesta 2012 Jijini Mwanza

Mkongwe wa muziki wa kizazi kipya aka Bongofleva,Prof Jay akishusha mistari yake kama kawa mbele ya umati wa watu (hawapo pichani),usiku huu ndani ya uwanja wa CCM Kirumba.

Mzee wa Miduara katika anga ya muziki wa kizazi kipya,IT akiimba jukwaani.
Masharobaro ndio habari ya mujiniiiii....! Bob Junior na kundi lake wakitumbuiza kwenye jukwaa la Serengeti fiesta 2012 usiku huu kwenye uwanja wa CCM Kirumba,jijini Mwanza.

Msanii wa kike anaekuja kwa kasi Recho akiimba kwa hisia jukwaani usiku huu

Mwanadada machachari kabisa awapo jukwaani,Mwasiti akiimba jukwaani usiku huu.

Msanii Ney wa Mitego kama kawa akikamua kwa hisia mbele ya wakazi wa jiji la Mwanza (hawapo pichani) waliojitokeza kwa wingi ndani ya uwanja wa ccm kirumba.
Msanii wa bongofleva,Bob Junior a.k.a Shombe shombe akitumuiza na densa wake jukwaani
Pichani kulia ni msanii Recho kutoka THT akiwa sambamba na densa wake wakionesha umahiri wa kuimba jukwaani mauno kwa mbalii hivi.

Msanii Ommy Dimpoz pozi kwa pozi akitumbuiza jukwaani na kundi lake

Mkurugenzi wa Vipindi na Utafiti kutoka Clouds Media Group Bwa. Ruge Mutahaba akisoma namba ya mshindi aliyejishindia gari aina ya Vits ambazo zimekuwa zikitolewa na kampuni ya Push Mobile katika mchakato mzima wa Tamasha la Serengeti Fiesta 2012,Kati ni Meneja Masoko wa kampuni ya Push Mobile Bwa,Rugambo Rodney na shoto ni mmoja wa wakilishi wa bodi ya Taifa ya michezo ya kubahatisha Bwa.Bakari Maggid wakishuhutia tukio hilo usiku huu ndani ya uwanja wa CCM Kirumba.Mshindi wa gari hiyo aina ya Vitz alitajwa kuwa ni Bahati Joseph,mkazi wa jiji la Mwanza,mjasilia mali.
Sehemu ya timu ya amsha amsha ya tamasha la serengeti fiesta 2012,kulia ni Dj Fetty,Bonge,Mully
Sehemu ya umati wa watu ukishangweka vilivyo usiku huu ndani ya uwanja wa ccm kirumba.
Msanii wa hip hop Roma Mkatoliki akiwa amepozi na mashabiki wake kabla ya kupanda jukwaani usiku huu.

Baadhi ya mashabiki wakiwa wamejitokeza usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012,linalofanyika kwenye uwanja wa ccm Kirumba.

Popular Posts