Pages

Showing posts with label Simba Sports Club. Show all posts
Showing posts with label Simba Sports Club. Show all posts

Saturday, August 4, 2012

MRISHO NGASSA AKABIDHIWA JEZI YA SIMBA BAADA YA KUJIUNGA



Ngasa akionyesha ALIVYOTOKELEZEA na jezi yake namba 16

Makamu Mwenyekiti wa Simba Geofrey Nyange 'Kaburu' akimkabidhi jezi atakayokuwa akiitumia mshambuliaji mpya wa timu hiyo, Mrisho Ngasa


Kaburu akizungumza kuhsina na Ngasa








Ngasa akiwa na begi jipya la rangio ya Simba
Kaburu na Ngasa wakipeana mkono wa shukran i kwa kukamilisha mchakato

Friday, August 3, 2012

Mchezaji Mrisho Ngassa aungana na Wachezaji Wenzake Wa Simba Mazoezini

Karibu Ngassa tufanye kazi, maisha menyewe mafupi mshikaji"Kaseja",Ngassa hakuna shaka nimekaribia swaiba.
Aliyekuwa mchezaji wa Azam,Mrisho Ngassa akiwa ameegemea gari yake aliyokabidhiwa jana mara baada ya kuwasili katika ufukwe wa Coco Beach kwa kuungana na wachezaji wenzake wa Simba baada ya maridhiano ya Azam,Simba na yeye kumalizika.Picha na Mdau Machellah

Wednesday, July 18, 2012

SIMBA YAICHAPA SPORTS MABAO 3-0 KOMBE LA KAGAME

Mshambuliaji wa Simba (kulia) akichuana na beki wa timu ya Sports katika mchezo wa Kombe la Kagame, ambapo mchezo huo umemalizika huku Simba wakiibua na ushindi wa mabao 3-0. Mabao ya Simba yamefungwa katika dakika 60 na 64,bao la kwanza likifungwa na Abdallah Juma na la pili likifungwa kwa mkwaju wa penati katika dakika hiyo ya 64, baada ya mchezaji wa Sports, kuunawa mpira akiwa ndani ya eneo la hatari.
Mwinyi Kazimoto (kushoto) akiwania mpira na beki wa Sports.

Thursday, July 12, 2012

SIMBA SC YATWAA KOMBE LA URAFIKI UWANJA WA TAIFA

Ubao wa matangazo ukionyesha Simba 5 Azam FC 3 kwenye uwanja wa Taifa.
Waziri asiyekuwa na Wizara maalum Zanzibar Mh. Machano Othman Said akimkabidhi kombe la ubingwa wa michuano ya Urafiki nahodha wa timu ya Simba Juma K. Juma mara baada ya timu ya Simba kuifunga timu ya Azam FC magoli 5-3 kwa penati, baada ya kutoka suluhu magoli 2-2 katika kipindi cha dakika tisini, kwenye mchezo mzuri na wa kuvutia kwa timu zote uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa leo hivyo kuifanya Simba kuibuka mabingwa wa kombe hilo.
Wachezaji wa timu ya Simba wakimnyanyua juu juu golikipa wao Juma K. Juma baada ya kupangua penati mbili katika mchezo huo uliokuwa wa fainali katika michuano ya Urafiki.
Mashabiki wa timu ya Azam FC wakishangilia timu yao.
Mashabiki wa timu ya Simba wakishangilia timu yao. Picha/Fullshange Blog.

Sunday, July 8, 2012

WABUNGE WA SIMBA WAWAKANDAMIZA WATANI WAO WA YANGA KWA PENALTI 3-2

Wachezaji wa Simba (Wabunge) wakishangilia ushindi baada ya kuwafunga watani wao wa Yanga (Wabunge) kwa penalti 3-2.
Yanga baada ya kipigo hicho.
Hivi ndivyo hali ilivyokuwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam katika mtanange wa watani wa jadi Simba na Yanga (Wabunge) wakati wa TAMASHA LA MATUMAINI ambapo wabunge wapenzi wa timu ya Simba wameibuka kidedea kwa penalti 3-2. Simba wamefunga penalti 3 wakati Yanga wakifunga 2.
(PICHA ZOTE NA GPL)

Saturday, June 30, 2012

KLABU YA SIMBA KUSHIRIKI KOMBE LA URAFIKI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KLABU ya Simba inapenda kutangaza kuwa itashiriki katika michuano ya Kombe la Tanzania (Urafiki) iliyopangwa kuanza visiwani Zanzibar Jumatatu ijayo.

Kwa mujibu wa Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange, maamuzi ya kushiriki katika mashindano hayo yamefikiwa baada ya majadiliano baina ya uongozi, benchi la ufundi na Kamati ya Ufundi ya Simba.

“Tumeamua kushiriki kwa sababu tumeona haitakuwa vema kufanya hivyo wakati watu wa Zanzibar wametupa heshima kubwa ya kutualika kwenye michuano hii. Kombe la Tanzania lina maana kubwa kwa sasa kutokana na hali halisi ya kisiasa na kijamii iliyopo visiwani humo kwa sasa,” alisema.

Makamu alisema zaidi ya kushiriki michuano hiyo, Simba pia itatumia fursa hiyo kuweka kambi maalumu kwa ajili ya kujiandaa na Kombe la Kagame lililopangwa kufanyika kuanzia Julai 14 mwaka huu.

Pia, alisema Simba itatumia ziara hiyo kupeleka kombe la Ligi Kuu ya Vodacom kwa wana Simba wa Zanzibar ambao walichangia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa ubingwa Vodacom na pia.

“Tusisahau pia kwamba kabla ya kucheza mechi yetu ya mwisho dhidi ya watani wetu wa jadi Yanga ambayo tulishinda kwa idadi ya mabao 5-0, Simba ilikwenda kuweka kambi Zanzibar,” alisema Kaburu.

Simba itaanza michuano hiyo siku ya Jumatatu ambapo itacheza na Mafunzo ya Zanzibar katika pambano lililopangwa kufanyika usiku. Awali mechi hiyo ilipangwa kuchezwa Jumatatu jioni lakini imesogezwa mbele hadi Jumatatu usiku.

Jumla ya timu nane zinashiriki katika michuano hiyo ambapo Waekundu wa Msimbazi wapo katika kundi A lenye timu za Simba, Azam, Mafunzo na timu ya soka ya taifa ya vijana ya Zanzibar wenye umri wa chini ya miaka 23 (Karume Boys).

Simba na Express kucheza Taifa

MABINGWA wa soka wa Tanzania, Simba SC, wanatarajiwa kucheza na mabingwa wa soka wa Uganda, Express FC, katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliopangwa kuchezwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, maandalizi yote kwa ajili ya pambano hilo yamekamilika na kwamba kikosi cha Simba kitaundwa na wachezaji wapya na wa zamani.


SIMBA SPORTS CLUB

P.O.BOX 15318 | TEL+255 222183330 |FAX +255 222183330 |MSIMBAZI/MCHIKICHI STREET | DAR ES SALAAM | TANZANIA | EMAIL simbasportsclub@yahoo.com|

WEBSITE www.simba.co.tz| AFFILIATED TO TFF, DRFA and IDFA

Popular Posts