Pages

Saturday, July 14, 2012

Basketball Legend Tim Hickey Visits Tanzania


TBF Vice President Magesa left with Tim Hickey right , Basketball Legend who taught and coached many TZ basketballers in the sixties , he is in TZ to visit the schools he taught in Dar and Moro and meet some of his players in the 60's like Hamidu Alekwa, Jaji Ramadhani (former CJ), Henry Ramadhani (former Dirctor of Sports), Mustafa Nyanganyi (former Minister and Ambassador), John Zembetakis, Wakili Hamidu Abuzeleni, Saleh Zonga , Mohamed Majura just to mention a few.. there are many more.


He has coached many Athletes in TZ and US.. Last time he visited TZ was 1970.
All who remember him at schools and courts please come and meet him and from Tuesday he will be in Morogoro for 4 days and then Back to Dar for 4 more days before departing to US.

Call me to get his contacts.
Phares MagesaTBF - VP.
+255 784 618320+255 767 618320
+255 713 618320

Dr Asha-Rose Migiro appointed as UN Secretary-General’s Special Envoy for HIV/AIDS in Africa

GENEVA, 13 July 2012—United Nations Secretary-General Ban Ki-Moon has appointed Asha-Rose Migiro as his Special Envoy for HIV/AIDS in Africa. “Ms Migiro’s experience in responding to AIDS as UN Deputy Secretary-General, combined with her many years as an advocate for health and social justice in Africa, make her uniquely qualified for this important role,” said Mr Ban.

Ms Migiro served as the United Nations Deputy Secretary-General from 2007 to 2012. In that role, she was integrally involved in promoting the AIDS response globally and within Africa, with special emphasis on reducing the vulnerability of women and girls and ensuring the rights of people living with HIV.

“I am honoured to accept this appointment at this crucial moment in the African AIDS response,” said Ms Migiro. “A decade ago, HIV in Africa was almost entirely an epidemic of despair. Today, we celebrate progress against AIDS that we never thought possible. Now is the time to take our efforts to a new level––I am committed to the Secretary-General’s vision that the beginning of the end of AIDS in Africa starts now.”

Ms Migiro served as Tanzania’s Minister of Foreign Affairs and International Cooperation from 2006 to 2007—the first woman to hold that position since the country’s independence. She was previously the Minister for Community Development, Gender and Children for five years. Prior to Government service, she pursued a career in academia, and, served as a member of Tanzania’s Law Reform Commission in 1997 and as a member of the United Nations Committee on the Elimination of Discrimination against Women in 2000.

“I look forward to working closely with Ms Migiro in helping African countries reduce their AIDS dependency and provide universal access to HIV prevention, treatment, care and support services,” said UNAIDS Executive Director Michel SidibĂ©. “Her experience and leadership will promote African ownership of the AIDS response at the highest levels and reduce the inequities of people affected by AIDS in the continent.”

Africa remains the continent most affected by HIV. In 2010, about 68% of all people living with HIV resided in sub-Saharan Africa. The region also accounted for 70% of all new HIV infections worldwide.

Warsha ya Sekta Binafsi juu ya Maandalizi ya Mkakati wa Taifa wa Kukabiliana na Athari za Mabadiliko ya Tabia nchi

Baadhi ya Washiriki wa Warsha ya sekta Binafsi juu ya Maandalizi ya Mkakati wa Taifa wa kukabiliana na athari za Mabadiliko ya Tabianchi Wakimsikiliza Mgeni Rasmi Dk Julias Ningu Pichani hayupo wakati wa Ufunguzi wa Warsha huko Kwenye Hotel ya Girafe Mjini Dar es Salaam.
Washiriki wa Warsha ya Sekta Binafsi juu ya Maandalizi ya mkakati wa Taifa wa Kukabiliana na athari za Mabadiliko ya Tabianchi wakiwa Katika Picha ya Pamoja na Mkurugenzi wa Mazingira Dk Julias Ningu Mara Baada ya Ufunguzi wa Warsha hiyo kwenye Hotel ya Girafe Mjini Dar es Salaam.Picha na Ali Meja

UJENZI WA BARABARA YA TUNDUMA MPAKA SUMBAWANGA WAENDELEA

Barabara ikiwa tayari imeshaanza kuwekewa lami
Daraja la MPUI
Daraja la LAELA
Vijana wakiwa kazini kurekebisha mifereji kwenye barabara hiyo mpya.Picha zote na Mdau Adam Mzee

FAINALI YA WHITE DENT QUIZ 2012 JIJINI MWANZA

Chemi cotex Industries Managing Director Lakshmi Narayan Rathi awarding the Whitedent squiz trophy to winning school – Pendo English Medium school – Dar es sallam

Chemi cotex industries Managing director Lakshmi Narayan Rathi (left) awarding the 1 million TSH Gift voucher for buying books for the school to the students of the winning school – Pendo English Medium School
--
Dar es Salaam; 13 July, 2012:Chemi & Cotex industries Ltd, watengenezaji wa watunga ya dawa za meno za Whitedent na bidhaa nyingine za usafi wa kinywa ya leo ina furaha kutangaza fainali ya Whitedent shule squiz 2012.

Washindiwasquizhii mwaka huu ni Pendo English Medium kutoka Mwanza, ambayoilichukuakombe la whitedent Squiz mara baada ya kuwabwagaShule ya Msingi Yombo Vituka Dar es sallam katika fainali hizo.

Timu hiyo ilijishindia kompyuta 9, printer pamoja, vocha za shilingi milioni 1 milioni kwa ajili ya kununua vitabu vya shule, baiskeli kwa ajili ya wanafunzi walioshiriki mbali na vocha zenye thamani ya shilingi 200,000 kwa ajili ya kununua vitabu, Shule ilipatiwa kompyuta 4, printer 1 na vocha za manunuzi za shilingi 400,000 kwa ajili ya kununua vitabu na saa, Vochaya100,000 kwaajiliya kununua vitabu kwa wanafunzi walioshiriki.

Zawadinyinginewalizopewawale walioingia katika hatua ya nusu fainali na robo ni kompyuta, taa za nishati yajua, mipira, dawazameno, miswaki mbali na T-shirt nakujishindiavyetivyotehivivikiwana thamani ya shilingi milioni 30.

Hotuba ya kuhitimisha kutokaChemi&Cotex kwa wanafunzi mjini Mwanza iliwapongeza wanafunzi wotena shule zilizoshinda kwa ushirikiano wao wa hali na mali katika mashindano hayonakwa umma piaikiwa ni pamoja na ziara hasa katika vituo vya mayatima, Dar na
Arusha.
Shindano hili lilihusisha wanafunzi wa darasa la sita wenye umri kati ya miaka 12-13 kwa kuzingatia jinsiaili kuweza kukabialiana na changamoto na wote walipewa zawadi mbalimbali.
Zaidi ya hapo shindano hili lilishirikisha zaidi shughuli za kijamii ambapo washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya robo fainali na nusu fainali walipata fursa ya kutembelea vituo vya yatima kujua maendeleo yao kielimu zaidi na pia kuwapatia zawadi mbalimbali kutoka Chemi&Cotex. Tunayo furaha kubwa kutangaza kuwa chemsha bongo mashulenii mehitimishwa rasmi.
Ends.

RAIS JAKAYA KIKWETE ALIPOTEMBELEA MAKAO MAKUU YA SMART PARTNERSHIP

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki katika kikao maalumu cha maandalizi ya mkutano wa Commonwealth Partnership for Technology Management (CPTM) kwenye makao makuu ya CPTM inayojiandaa kwa mkutano wake mkuu wa Global 2012 International Smart Partneship Dialogue unaotarajiwa kufanyika mwezi Mei Mwakani jijini Dar es salaam. Picha na IKULU

JAKAYA KIKWETE ALIPOKUTANA NA KAMATI YA BUNGE YA MAMBO YA NJE NA ULINZI NA USALAMA NCHINI UINGEREZA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsindikiza Mqwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Mhe Edward Lowassa baada ya kukutana nao jijini London, Uingereza, Julai 12, 2012
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki katika kikao maalumu cha maandalizi ya mkutano wa Commonwealth Partnership for Technology Management (CPTM) kwenye makao makuu ya CPTM inayojiandaa kwa mkutano wake mkuu wa Global 2012 International Smart Partneship Dialogue unaotarajiwa kufanyika mwezi Mei Mwakani jijini Dar es salaam.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama jijini London, Uingereza, Julai 12, 2012.Picha na IKULU

MGOGORO WA ARDHI KATI YA WANAKIJIJI WA KIMBIJI NA JWTZ

Wanakijiji wa Kimbiji,Wilayani Temeke,nje kidogo ya jiji la Dar-es-salaam, wamekuwa
wakipata usumbufu wa vitisho na kuharibiwa mazao na makazi yao kutoka baadhi
wanajeshi wa JWTZ,ambao wanania ya kutaka kuyachukua maeneo ya wanakijiji
wa Kimbiji kwa kutumia nembo ya Jeshi (JWTZ),kinyume cha sheria
Kuanzia mwaka jana 2011 wanajeshi wa JWTZ wamekua na tabia za kuvamia mashamba
ya wanakijiji Kimbiji na kuvunja makazi ya wananchi ambao wameipigia kura serikali
ya hawamu ya nne,na huku vyombo vya dola vikiwa vimenyamaza kimya.

Wanakijiji wa Kimbiji wanalalamikia Serikali ya wilaya,mkoa hadi Serikali kuu,kuwa
unyama,unyanyaswaji uharibifu unaofanywa na wanajeshi hao wa JWTZ dhidi ya
wananchi wa Kimbiji hauwezi kuvumiliwa, Kwani ni haibu na udhuni mkubwa kuona
vyombo vya dola vikiwa vinanyamaza kimya na huku wapiga kura walioipigia kura
serikali wananyanyaswa na Wanajeshi JWTZ .

Wanakijiji wa Kimbiji,Wilaya Temeke,wanazifahamu haki zao na maeneo yao ya
asili ambayo wamekua wakiishi kama wenyeji .Pia wanafahamu fika kuwa hakuna
eneo lolote linalomilikiwa na Jeshi bali wanajeshi wanataka kuchukua mashamba
na makazi ya watu kwa maslahi yao binafsi!

JESHI LINAGEUKA CHOMBO CHA KUANGAMIZA WENYEJI WA DAR,
NA UTAMADUNI WAO ! KINYUME CHA KATIBA
Inajulikana wazi kikatiba kuwa kila raia anayo haki ya kulindwa na kulindiwa
mali zake na katiba ya nchi ambayo ndio muongozo wa nchi,
Lakini wakazi wa kijiji na wenyeji wa hasili ya mkoa wa Dar-es-salaam wanajikuta
wanafukuzwa katika maeneo yao ya hasili ,tena maeneo ambayo yapo nje ya jiji !
Wakazi hawa wa Kimbiji, wanalalamikia serikali kuwa Jeshi JWTZ badala ya kuwalinda
limegeuka kuwa hadui wa kutaka kuwanyaka na kuwafukuza katika makazi yao !
ya asili ,

WANAJESHI WANAJARIBU KUTUMA BARUA ZA VITISHO KIJIJINI,

Cha kushangaza ni kuwa baadhi ya maofisa wa Jeshi wanatumia barua zenye
nembo ya jeshi kuzipeleka katika serikali ya kijiji hili kutaka kunyang'anya
maeneo ya watu. Wanakijiji na uongozi wao wanashangazwa sana sana
na unyama huu,ambao ni uvunjaji wa sheria,katiba ya nchi na haki za binadamu !

Wanakijiji wa Kimbiji,wilayani Temeke,Dar-es-salaam, hawajawahi hata siku
moja kukaa kikao na serikali au wizara ya Ardhi, na kujulishwa kuwa kijiji
chenu kitakua cha kijeshi ! Utafiti wa kina unaonyesha kuwa makazi na mshamba
ya kimbiji ni mali ya wanakijiji,hakuna eneo la wanajeshi.

HAIWEZEKANI KUHAMISHA WANAKIJIJI AMBAO NI WAKAZI WA ASILI,
HETI MAOFISA WA JESHI WAPEWE VIWANJA VYA KUJENGA MAKAZI !
kufanya hivyo ni kuwafukuza wenyeji wa hasili na kuua utamaduni wao,pia ni
kuenda kinyume cha katiba ya nchi.


Haiwezekani Serikali ikae kimya na raia wake ambao wameipigia kura wananyanyaswa
na chombo kama JWTZ kwa vitisho vya mtutu wa bunduki na magwanda ya kijeshi !

Wakijiji wanaiomba Serikali na tahasisi za haki ya binadamu kuingilia kati mateso haya.

Labda kwa maelezo zaidi wasiliana na Uongozi wa Kijiji,Diwani simu Na. 0713768082
Mwenyekiti: Simu namba 0713846688

KUHUSU MAFAO YA PENSHENI KATIKA MAREKEBISHO YA SHERIA ZA MIFUKO

Ufuatao ni ufafanuzi mfupi kuhusu ombi lililotolewa na Katibu wa Tamico
(Geita) kuhusu marekebisho ya Sheria za Mifuko hasa kuhusu mafao

· Ni kweli kuwa Sheria za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na
Sheria ya Mamlaka zimefanyiwa marekebisho na kupitishwa na Bunge tarehe 13
Aprili, 2012. Sheria hiyo tayari imeshasaininiwa na Mheshimiwa Rais na
imeanza kutumika rasmi. Marekebisho haya yanawahusu wafanyakazi wote nchini
mwetu bila kubagua sekta yoyote ile.

· Kwa mujibu wa marekebisho hayo mafao ya kujitoa (withdrawal
benefits) yamefutwa na kuanzia sasa hayatakuwepo. Mafao hayo yalikuwa
yanatolewa pale mwanachama alipokuwa anaacha kazi. Sasa mwanachama wa Mfuko
atapata mafao yake pale atakopfikisha umri wa kustaafu kwa hiari (miaka
55) au kwa lazima (miaka 60).

· Marekebisho hayo kuhusu kuzuia mafao ya kujitoa yamefanyika ili
kutimiza lengo na madhumuni ya hifadhi ya jamii ambayo ni kuhakikisha kuwa
mwanachama anapostaafu anapata mafao bora yatakayomwezesha kumudu maisha ya
uzeeni wakati ambapo nguvu ya kufanya kazi tayari imeshamwishia. Mafao ya
kujitoa yanapunguza kama si kuondoa kabisa kinga hii ya mfanyakazi
anapofika uzeeni.

· Tunawaomba muwaelimishe wafanyakazi umuhimu na madhumuni ya mafao
ya hifadhi ya jamii. Hifadhi ya jamii ni nyenzo mahususi iliyowekwa
kuwasaidia wafanyakazi kuendesha maisha yao wakati wanapokuwa wameishastaafu
tayari. Umasikini wa kipato wakati wa uzee ni mojawapo ya changamoto ngumu
kukabiliana nazo kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla. Tunawasihi tena
muelimishe wafanyakazi kuhusu jambo hili. Tafadhali msisite kuwasiliana na
Mamlaka pale ufafanuzi zaidi utakapohitajika

· Kwa kuwa marekebisho hayo yamesainiwa na kuanza kutumika rasmi
kama sheria, mafao ya kujitoa hayawezi kutolewa tena na wafanyakazi
watakaoacha kazi kwa sababu ya marekebisho ya kipengele hicho watakuwa
hawajaijitendea haki wao wenyewe na pia itakuwa ni kunyume cha Sheria.
Mamlaka inaandaa kanuni za mafao ambayo lengo lake ni kuboresha maslahi ya
wanachama, kanuni hizo zitajadiliwa na wadau wakiwemo vyama vya wafanyakazi
na waajiri ili kupata maoni yao.

· Tunapenda kuwahakikishia kwamba katika hili maslahi ya wanachama
yatalindwa na hakuna mwanachama atakayepunjika kutokana na utaratibu huo.

Imetolewa na Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii.

KWA UFAFANUZI HUU TOKA MAMLAKA HUSIKA,

(i) Hakuna shaka kwamba sheria tayari imeaanza kutumika.

(ii) Hakuna shaka kwamba Bunge na Serikali wamekaa kimya kwa sababu wanajua
kwamba sheria waliyotunga na kupitisha ni pigo kwa wafanyakazi hawa wa
sekta binafsi hasa ukizingatia kwamba

- sekta binafsi ndo wachangiaji wakubwa wa mifuko hiyo.

- Usalama wa Ajira wa wafanyakazi wa sekta binafsi ni asilimia zero maana
waajiri wamekuwa wakiwafukuza kama Popo au senene.serikali hajaiweka kinga
madhubuti kwa wafanyakazi hawa.sheria ya kazi iliopo inawasaidia zaidi
waajiri.

- Mazingira ya kazi kwa sekta binafsi sio rafiki kwa afya na usalama wa
wafanyakazi.Hivi unategemea kijana aliye na miaka 25 kwa sasa na anafanya
kazi migodini,viwanda vya chuma,Ujenzi NK afanye kazi hadi astaafu kwa
mazingira haya? NADHANI HUU NI UVIVU WA KUFIKIRI KWA WATU TULIOWAPA DHAMANA
KUBWA NA HILI NASEMA HALIKUBALIKI HATA KIDOGO!!!!!!!!!!!!!!!!!

NINI KIFANYIKE?

TUNASUBIRI MAJIBU TOKA SERIKALINI NA BUNGENI

Kama kweli wametunga na kupitisha sheria hii kandamizi,nasema kitu hiki
hakikubaliki hata kidogo.Nguzo ya wafanyakazi ni UMOJA NA
MSHIKAMANO.Wafanyakazi wote sekta binafsi tutapiga kura ya maoni kukataa
sheria hii kisha tutapeleka suala hili mahakamani na iwapo mahakama itaamua
ndivyo sivyo nadhani hatua itakayofuata ni kuprotest against this ACT.

Nimeguswa sana na Jambo hili kwa sababu Sheria hii imetungwa kukandamiza
masilahi ya wafanyakazi wanyonge wa nchi hii na kwa pamoja tutahakikisha
sheria hii inafutwa hata kama watatu Kolimba,mwakyembe,ulimboka NK.

MSHIKAMANO DAIMA - SOLIDARITY FOREVER

Benjamin Daudi Dotto

Katibu wa Tamico wilaya ya Geita,

SLP 335,

Geita – Tanzania.

Simu: ofisi +255 774 866635

Simu:mkononi + 255 767 715116 alt.+255 784 715116

TAARIFA JUU YA HALI YA UTENDAJI WA VIONGOZI WA BUNGE

TAARIFA KWA UMMA JUU YA HALI YA UTENDAJI WA VIONGOZI WA BUNGE

Taarifa hii ni matokeo ya ufuatiliaji wa shughuli za Bunge na mijadala ya Wabunge juu ya mahitaji ya umma kwao kwenye maendeleo, uongozi, kuimarisha utawala bora, uwajibikaji wa serikali na haki za binadamu na kuimarisha usimamizi wao kwa serikali kupitia mijadala yao katika vikao vya Bunge. Taarifa hii inahusika na utendaji wa viongozi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwaka 2011.

Kwa Ujumla:

Kumekuwa na upendeleo wa vyama katika kujadili na kuchangia hoja na kuonekana Mh Spika na Wenyeviti wa vikao kutumia vibaya kanuni za bunge kuwadhibiti wabunge kulingana na vyama vyao. Mfano ni pale Mh Spika alipomzuia Mh Tundu Lissu kumwuliza swali Mh Mizengo Pinda juu ya mauaji ya raia mikononi mwa vyombo vya dola kwa madai kuwa kuna kesi mahakamani juu ya hoja hiyo. Pamoja na Mh Lissu kujitahidi kufafanua tofauti zilizopo kati ya kesi inayomkabili yeye na wenzake na hoja anayoiulizia, bado Mh Spika ameendelea kuizuia hoja hiyo. Kulingana na maoni ya wabunge 36, Watendaji 22, wachambuzi 11 na wananchi 48 waliohojiwa, ubora wa uongozi wa bunge kwa mwaka 2011 ni kama ilivyo hapa chini:

NAFASI

JINA

SIFA YA KIPIMO

ALAMA WASTANI

MAONI YA WASHIRIKI

1

NDUGAI,

JOB

YUSTINO

USIKIVU KWA WABUNGE

2.5

Amejitahidi sana kukwepa upendeleo wa kisiasa na kuilinda serikali; haoneshi utashi wake kumiliki mamlaka aliyopewa na Kanuni za Bunge anapoongoza vikao.

UZINGATIAJI KANUNI

2.625

UPENDELEO WA KISIASA

2.5625

UZINGATIAJI HOJA

2.375

USHABIKI BUNGENI

3

JUMLA

KIWANGO

13.0625

WASTANI

2.6125

2

SIMBACHAWENE,

USIKIVU KWA WABUNGE

2.125

Msikivu kwa Wabunge haswa wenye HOJA zenye maslahi kwa Taifa; Amejitahidi sana kukwepa upendeleo wa kisiasa na kuilinda serikali; Anayumbishwa na makundi au siasa.

GEORGE

BONIFACE

UZINGATIAJI KANUNI

2.3125

UPENDELEO WA KISIASA

3.28125

UZINGATIAJI HOJA

2.09375

USHABIKI BUNGENI

3.4375

JUMLA

KIWANGO

13.25

WASTANI

2.65

3

MAKINDA,

ANNE

SEMAMBA

USIKIVU KWA WABUNGE

3.03125

Imara kwenye kanuni na kuzingatia hoja; Anayumbishwa na ushabiki kisiasa; si msikivu kwa wabunge.

UZINGATIAJI KANUNI

2.65625

UPENDELEO WA KISIASA

3.46875

UZINGATIAJI HOJA

2.75

USHABIKI BUNGENI

2.9375

JUMLA

KIWANGO

14.84375

WASTANI

2.96875

Anajitahidi sana kuzingatia kanuni; Anayumbishwa na makundi kisiasa; si msikivu kwa wabunge.

4

MHAGAMA,

JENISTER

JOAKIM

USIKIVU KWA WABUNGE

3.21875

UZINGATIAJI KANUNI

3.15625

UPENDELEO WA KISIASA

3.5

UZINGATIAJI HOJA

3.53125

USHABIKI BUNGENI

3.3125

JUMLA

KIWANGO

16.71875

WASTANI

3.34375

5

MABUMBA,

SILVESTER

MASELE

USIKIVU KWA WABUNGE

4.25

Haoneshi ushabiki wa wazi wa kisiasa; hushindwa kuhimili mivuto ya makundi na upendeleo wa kisiasa; Si msikivu kwa wabunge.

UZINGATIAJI KANUNI

4.25

UPENDELEO WA KISIASA

3.78125

UZINGATIAJI HOJA

3.90625

USHABIKI BUNGENI

3.25

JUMLA

KIWANGO

19.4375

WASTANI

3.8875

ANGALIZO LA VIWANGO:

1.00 – 1.49 = Uongozi Mzuri Sana,

1.50 – 2.49 = Uongozi Mzuri

2.50 – 3.49 = Uongozi wa Wastani

3.50 – 4.49 = Uongozi Dhaifu

4.50 – 5.0 = Uongozi Dhaifu Sana

Kwa Ujumla

Taarifa hii imeonesha mapungufu kadhaa kwenye uongozi na utendaji wa kazi wa viongozi wa Bunge na hivyo kutoa changamoto kwa viongozi wa Bunge na wabunge kuimarisha utendaji wao iwapo wangependa kutekeleza wajibu wao kwa jamii. Ni matarajio yetu kuwa wabunge watatumia taarifa hii kuimarisha mjadala wa bajeti ya 2012/13 unaoendelea, ikiwa ni pamoja na kendeha na kusimamia vema vikao na mijadala ya Bunge na kutoa changamoto kwa utendaji wa serkali kwa maslahi ya jamii.

Tunakumbusha pia kuwa bado Bunge limeendelea kutumia muda vibaya kwa wabunge kuendeleza vijembe, kebehi, shukrani, pongezi na salamu. Hata baada ya miaka miwili sasa baada ya Uchaguzi na Serikali kuundwa bado wabunge wameendelea kutoa shukrani kwa Rais, wapiga kura wao na wengineo. Matumizi haya ya muda yanapunguza mijadala na mwendelezo wa ushiriki wa wabunge kwa ufasaha.

Mapendekezo

1. Ipo haja ya wabunge kujiangalia kwa karibu uwezo na utayari wao kujadili maswala ya maslahi kwa taifa bila kuingiza ushabiki na maslahi binafsi.

2. Iangaliwe upya akidi ya wabunge katika kupitisha hoja (angalau iwe robo tatu na sio nusu ya wabunge kama ilivyo sasa).Hii iendane na haja kwa Mhe, Spika kujiridhisha bila kuacha shaka juu ya idadi ya kura za wabunge kwenye hoja husika, na haswa walioshiriki mjadala baadala ya kuingia kwa ajili ya kupiga kura tu;

3. Spika atumie mamlaka na kanuni za Bunge ili kudhibiti maudhui, mantiki na maana ya mijadala ya Bunge bila kuathiri maslahi ya taifa. Katika hili Mhe Spika, Naibu na Wenyeviti wa Bunge,wana dhamana ya kuhakikisha ushabiki wa kisiasa haupati nafasi kuvuruga Bunge

4. Tunaona ipo nafasi kubwa kwa Spika kusaidia na kuelekeza bunge ili lifanye kazi zake vizuri zaidi. Spika atumie nafasi hii baadala ya yeye kuangukia kwenye ushabiki na kuilinda serikali.

Imetolewa na Taasisi ya Raia ya Haki za Kisiasa na Mwenendo wa Bunge,

CIVIL AND POLITICAL RIGHTS WATCH

Marcossy Albanie

Mkurugenzi Mtendaji

Popular Posts