Pages

Showing posts with label GEITA. Show all posts
Showing posts with label GEITA. Show all posts

Wednesday, July 18, 2012

Kampuni ya African Barrick Gold yatoa Msaada wa Chakula Shinyanga na Geita

Kutoka Kushoto: Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale, Ibrahim Marwa, Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya wakipokea msaada wa sehemu ya tani 200 za mahindi kutoka kwa Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof (wa pili kulia)na Makamu wa Rais wa African Barrick Gold (ABG),Utekelezaji Muundo, Peter Gereta katika hafla iliyofanyika katika Kata ya bulyanhulu wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga hivi karibuni. Maeneo yatakayonufaika na msaada huo uliogharimu kiasi cha milioni 163/- ni kwa wale waliokumbwa na uhaba wa chakula katika vijiji 14 vilivyoko Bugarama, Mwingiro na Bulyanhulu wilaya ya Kahama mkoa wa Shinyanga na Nyang'hwale Mkoa mpya wa Geita.
Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya akipokea msaada wa tani 200 za mahindi kutoka kwa Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof (wa pili kulia). Kushoto ni Diwani wa Kata ya Bulyanhulu, Joseph Makoba.
Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale, Ibrahim Marwa akihutubia kabla ya makabidhiano.
Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya akihutubia kabla ya makabidhiano. Kulia ni Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof na Kushoto ni Diwani wa Kata ya Bulyanhulu, Joseph Makoba na Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale, Ibrahim Marwa.
Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige akibadilishana mawazo na Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof (katikati), na Makamu wa Rais wa African Barrick Gold (ABG),Utekelezaji Muundo, Peter Gereta.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof akijadiliana jambo na Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya.
Kutoka Kushoto: Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof , Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya na Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale, Ibrahim Marwa wakikagua sehemu ya shehena ya mahindi mara baada ya makabidhiano.
Sehemu ya viongozi wa vijiji lengwa na msaada huo waliohudhuria hafla hiyo.Picha Zote na Badi John

Saturday, July 14, 2012

KUHUSU MAFAO YA PENSHENI KATIKA MAREKEBISHO YA SHERIA ZA MIFUKO

Ufuatao ni ufafanuzi mfupi kuhusu ombi lililotolewa na Katibu wa Tamico
(Geita) kuhusu marekebisho ya Sheria za Mifuko hasa kuhusu mafao

· Ni kweli kuwa Sheria za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na
Sheria ya Mamlaka zimefanyiwa marekebisho na kupitishwa na Bunge tarehe 13
Aprili, 2012. Sheria hiyo tayari imeshasaininiwa na Mheshimiwa Rais na
imeanza kutumika rasmi. Marekebisho haya yanawahusu wafanyakazi wote nchini
mwetu bila kubagua sekta yoyote ile.

· Kwa mujibu wa marekebisho hayo mafao ya kujitoa (withdrawal
benefits) yamefutwa na kuanzia sasa hayatakuwepo. Mafao hayo yalikuwa
yanatolewa pale mwanachama alipokuwa anaacha kazi. Sasa mwanachama wa Mfuko
atapata mafao yake pale atakopfikisha umri wa kustaafu kwa hiari (miaka
55) au kwa lazima (miaka 60).

· Marekebisho hayo kuhusu kuzuia mafao ya kujitoa yamefanyika ili
kutimiza lengo na madhumuni ya hifadhi ya jamii ambayo ni kuhakikisha kuwa
mwanachama anapostaafu anapata mafao bora yatakayomwezesha kumudu maisha ya
uzeeni wakati ambapo nguvu ya kufanya kazi tayari imeshamwishia. Mafao ya
kujitoa yanapunguza kama si kuondoa kabisa kinga hii ya mfanyakazi
anapofika uzeeni.

· Tunawaomba muwaelimishe wafanyakazi umuhimu na madhumuni ya mafao
ya hifadhi ya jamii. Hifadhi ya jamii ni nyenzo mahususi iliyowekwa
kuwasaidia wafanyakazi kuendesha maisha yao wakati wanapokuwa wameishastaafu
tayari. Umasikini wa kipato wakati wa uzee ni mojawapo ya changamoto ngumu
kukabiliana nazo kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla. Tunawasihi tena
muelimishe wafanyakazi kuhusu jambo hili. Tafadhali msisite kuwasiliana na
Mamlaka pale ufafanuzi zaidi utakapohitajika

· Kwa kuwa marekebisho hayo yamesainiwa na kuanza kutumika rasmi
kama sheria, mafao ya kujitoa hayawezi kutolewa tena na wafanyakazi
watakaoacha kazi kwa sababu ya marekebisho ya kipengele hicho watakuwa
hawajaijitendea haki wao wenyewe na pia itakuwa ni kunyume cha Sheria.
Mamlaka inaandaa kanuni za mafao ambayo lengo lake ni kuboresha maslahi ya
wanachama, kanuni hizo zitajadiliwa na wadau wakiwemo vyama vya wafanyakazi
na waajiri ili kupata maoni yao.

· Tunapenda kuwahakikishia kwamba katika hili maslahi ya wanachama
yatalindwa na hakuna mwanachama atakayepunjika kutokana na utaratibu huo.

Imetolewa na Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Hifadhi ya Jamii.

KWA UFAFANUZI HUU TOKA MAMLAKA HUSIKA,

(i) Hakuna shaka kwamba sheria tayari imeaanza kutumika.

(ii) Hakuna shaka kwamba Bunge na Serikali wamekaa kimya kwa sababu wanajua
kwamba sheria waliyotunga na kupitisha ni pigo kwa wafanyakazi hawa wa
sekta binafsi hasa ukizingatia kwamba

- sekta binafsi ndo wachangiaji wakubwa wa mifuko hiyo.

- Usalama wa Ajira wa wafanyakazi wa sekta binafsi ni asilimia zero maana
waajiri wamekuwa wakiwafukuza kama Popo au senene.serikali hajaiweka kinga
madhubuti kwa wafanyakazi hawa.sheria ya kazi iliopo inawasaidia zaidi
waajiri.

- Mazingira ya kazi kwa sekta binafsi sio rafiki kwa afya na usalama wa
wafanyakazi.Hivi unategemea kijana aliye na miaka 25 kwa sasa na anafanya
kazi migodini,viwanda vya chuma,Ujenzi NK afanye kazi hadi astaafu kwa
mazingira haya? NADHANI HUU NI UVIVU WA KUFIKIRI KWA WATU TULIOWAPA DHAMANA
KUBWA NA HILI NASEMA HALIKUBALIKI HATA KIDOGO!!!!!!!!!!!!!!!!!

NINI KIFANYIKE?

TUNASUBIRI MAJIBU TOKA SERIKALINI NA BUNGENI

Kama kweli wametunga na kupitisha sheria hii kandamizi,nasema kitu hiki
hakikubaliki hata kidogo.Nguzo ya wafanyakazi ni UMOJA NA
MSHIKAMANO.Wafanyakazi wote sekta binafsi tutapiga kura ya maoni kukataa
sheria hii kisha tutapeleka suala hili mahakamani na iwapo mahakama itaamua
ndivyo sivyo nadhani hatua itakayofuata ni kuprotest against this ACT.

Nimeguswa sana na Jambo hili kwa sababu Sheria hii imetungwa kukandamiza
masilahi ya wafanyakazi wanyonge wa nchi hii na kwa pamoja tutahakikisha
sheria hii inafutwa hata kama watatu Kolimba,mwakyembe,ulimboka NK.

MSHIKAMANO DAIMA - SOLIDARITY FOREVER

Benjamin Daudi Dotto

Katibu wa Tamico wilaya ya Geita,

SLP 335,

Geita – Tanzania.

Simu: ofisi +255 774 866635

Simu:mkononi + 255 767 715116 alt.+255 784 715116

Monday, July 2, 2012

ATEKELEZA FAMILIA BAADA YA MKE KUJIFUNGUA WATOTO WANAOFANANA NA NYANI.

Mtoto Alhaj.
Mtoto Alhaj akiwa amesimama.
Mtoto Alhaj akiwa anatembea.
Abdulatifu Sadik (5) akipata kifungua kinywa nje ya nyumbani kwao.
Mwanaharusi Juma akiwa nje ya nyumba yake pamoja na watoto wake Ahaj (10) mwenye shati Nyekundu na Abdulatifu.Picha zote na Nathaniel Limu
---
Mjumbe wa kamati ya shule ya msingi Ndulungu tarafa ya Ndago wilayani Iramba mkoa wa Singida, Sadik Suleman Mnyawi (44), amemtelekeza mke wake mdogo Mwanaharusi Juma (34), kwa zaidi ya miaka miwili na kumsababishia maisha kuwa magumu.Imedaiwa kwamba Mnyawi amemtelekeza mke wake huyo, kwa madai kwamba amezaa watoto wawili wanaofafana na nyani.
Mjumbe huyo wa kamati ya shule, amemtelekeza mke wake mdogo na kumpora nguo zote na kumwachia zile alizokuwa amevaa tu. Pia aliondoka na matandiko yote ya kitandani na kubakisha chaga pekee.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mwanaharusi awali alikuwa ameolewa na mwanaume mwingine waliobahatika kupata mtoto mmoja, Fadhili Juma (15).Alisema baada ya kuachana na mwanaume wa kwanza, mwaka 2002, aliolewa na Mnyawi ambaye amemtoroka na kumwacha bila matunzo yoyote ya watoto watatu aliozaa naye.Alisema katika kipindi cha miaka 10 ya ndoa yake na Mnyawi, walifanikiwa kupata watoto watatu kati yao, wawili wakiwa wanafanana na nyani.

“Mtoto wangu yule niliyezaa na mume wa kwanza, Fadhila Juma, yeye yupo darasa la saba mwaka huu. Ramadhani (6) ambaye nimezaa na Mnyawi, yeye anasoma darasa la kwanza hapa Ndulungu”,alisema.

Mwanaharusi alisema kwa watoto wake aliozaa na Mnaywi,Alhaj (10) na Abdulatifu (5) ambao wana sura ya mnyama kutokana na hali zao zilivyo, wameshindwa kuanza shule.
Akifafanua zaidi, alisema watoto hao wanaofanana na nyani, hawasikii wala hawasemi. Mawasiliano yao yanategemea ishara tu.

“Ukiacha matatizo yao ya kutokusikia na kuzungumza, pia wanahema kwa tabu kubwa. Kama huwaoni, ukisikia wanavyohema, unaweza ukafikiria kwamba hao zio binadamu ni nguruwe anahema”,alisema kwa masikitiko.

Mwanaharusi alisema mikono yao ni midogo mno na mifupi na ni dhaifu, matumbo na macho yao ni makubwa. Alhaji pekee ndiye mwenye uwezo wa kusimama na kutembea umbali mfupi na mwenendo wake unafanana na wa nyani.

Hata hivyo, alisema watoto hao wawili aliwazaa wakiwa wana sura za binadamu na afya zao zikiwa njema kabisa. Lakini wakati wanaendelea kukua, ndipo walipoanza kuugua mara kwa mara na kisha kubadilika sura.

“Wakati bado tunaelewana na mume wangu, tuliwahi kumpeleka Alhaji katika hospitali ya mkoa wa Singida. Alichunguzwa na alibainika kuwa na upungufu wa damu. Aliongezewa damu na kisha tuliruhusiwa kurudi nyumbani”,alisema.

Alisema baada ya kurudi nyumbani, haikuchukua muda, Alhaji alianza kuugua tena na baada ya kumshawishi mume wake Mnyawi, wampeleke hospitali ya rufaa, ndipo alipomkimbia na kuhamia kwa mke wake mkubwa.

Akizungumza kwa masikitiko makubwa,alisema kuanzia wakati huo, anaishi maisha magumu mno ambayo ni ya kuomba omba. Mnyawi pamoja na familia yake, amewabembeleza wamsaidie mizigo wa kuwalea watoto hao, wamegoma kabisa.Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho, Idd Nyauli, alisema wamejitahidi kumshauri Mnyawi amrudie mke wake mdogo ili waweze kuwalea watoto wao pamaja, jitahida hizo zimegonga mwamba baada ya Mnyawi kugoma kumrudia Mwanaharusi.

Naye mratibu elimu wa kata hiyo Mwekwa Mwekwa, alisema watoto hao wawili, shule inayowafaa ni ile ya watoto wenye mtindio wa ubongo na si hizi za kawaida.Jitihada ya kumtafuta Mnyawi ambaye anaishi kijiji hicho cha Ndulungu, hazikuzaa matunda baada ya kuelezwa kwamba baada ya kusikia waandishi wa habari watafika kijijini hapo, alifunga safari na kuelekea jijini Mwanza.

Tuesday, June 26, 2012

TBL YAKAGUA MRADI WA MAJI WA SH. MIL. 25 GEITA

Mkandarasi wa mradi wa visima vya maji, Enock Kangasa akisukuma pump ya moja ya visima vya maji mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Geita Manzie Mangochie (kushoto), kilichojengwa kwa msaada wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kwa gharama ya sh. milioni 25 katika Kijiji cha Mkolani I, wilayani Geita juzi.
Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo (aliyeweka miwani kifuani) akifurahia jambo wakati Mkuu wa Wilaya ya Geita , Manzie Mangochie akijaribu moja ya pump ya visima vya maji katika mradi unaojengwa kwa sh. milioni 25 na TBL katika Kijiji cha Mkolani I, Geita, viongozi hao walikwenda kukagua mradi huo juzi
Mkuu wa Wilaya ya Geita, Manzie Mangochie, akisistiza jambo wakati akikagua juzi mradi wa visima vya maji unaotekelezwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika Kijiji cha Mkolani I wilayani Geita, Katikati ni Mhandisi wa Maji wilayani Geita, Enock Kangasa Mradi huo umegharimu milioni 25.

Popular Posts