Pages

Showing posts with label Tanga. Show all posts
Showing posts with label Tanga. Show all posts

Friday, September 7, 2012

Bumbuli Development Corporation announces new board of directors

I am pleased to announce the formation of the new Board of Directors for Bumbuli Development Corporation (BDC). The BDC Board will provide the leadership and support in ensuring successful implementation of the vision and mission of BDC for the next three years. The ten-member Board will be the topmost governing body of BDC. The primary responsibility of a board member is to participate in the development of strategies and major decision-making at board meetings and being active on an ongoing basis in a committee of the board.

I am proud to announce that this Board of Directors is made of a group of extraordinary individuals, drawn from different sectors and nationalities to provide BDC with the cutting edge leadership and foresight it needs to fulfill its mission.

The new Directors are:


1. Dr. Paul Armington??
Dr. Armington is the President of World Institute for Leadership and Management in Africa (WILMA). He began his career as an economist working in International Monetary Fund (IMF) Research Department, where he produced influential articles on international trade and helped to found the IMF’s now-famous “World Economic Outlook” methodology and publication. Later, he worked at the Organisation for Economic Co-operation and Development (OECD) where he was instrumental in bringing about the international agreement known as the Smithsonian Realignment of Exchange Rates (1971). From 1975-86, Dr. Armington worked as an economist in the private sector, collaborating with the London School of Business, Ford Foundation, Forex Research Ltd., Wharton Econometric Forecasting Associates, and the World Bank.??Dr. Armington is an accomplished academic and taught at the University of Pennsylvania. He is famous for the “Armington Elasticities”, now referred to and taught in graduate courses in international trade and economics.



In 1986, Dr. Armington joined the World Bank as Senior Economist. He also served as Division Chief and advisor in the International Economics Department of the World Bank, and then for three years as Principal Economist in the Africa Region’s Capacity Building Unit. In 1999, he took early retirement to devote his energies to the creation of the World Institute for Leadership and Management in Africa (WILMA), which he now serves as president?.Dr. Armington received his Bachelor’s degree at Swarthmore College, USA and his Ph.D in economics from the University of California, Berkeley.


2. Ambassador Juma V. Mwapachu
Ambassador Juma V. Mwapachu is former Secretary General of the East Africa Community (EAC) and a well-known and respected Tanzanian businessman, diplomat and thought-leader. Ambassador Mwapachu has held a number of senior positions in both the public and private sector of Tanzania. He served as Tanzania’s Ambassador to France from 2002 to 2006. He was the founding Secretary General of the Tanzania Chamber of Commerce, Industry and Agriculture in 1988, served as Chairman of the Confederation of Tanzania Industries between 1996 and 2000 and Chairman of the East African Business Council from 1999 to 2000. Throughout his working career, he has been a leading advocate of the creation of a strong and dynamic private sector in Tanzania.

Ambassador Mwapachu served as a Managing Consultant at Coopers & Lybrand Associates which is now PriceWaterhouseCoopers (PWC) in the early 1980s. He has also served on a number of Presidential Commissions that consolidated Tanzania’s market economy and which ushered in a multi-party political system. He was a member of the Team of Experts that crafted Tanzania’s Development Vision 2025. He played a leading role in the regional integration of East Africa as Secretary General of the East African Community for five years between 2006 and 2011.

He began his career in the public sector in Tanzania as a State Attorney and later served in the National bank of Commerce, rural development and the Foreign Office. He has been Chairman of Board of Directors of Tanzania Railways and the Tanzania Investment Bank. He has been a Non Executive Director of Exim Bank (Tanzania) Limited since December 5, 2008. Ambassador Mwapachu serves as a Director of The Heritage Insurance Company (T) Limited, Non Executive Director of African Barrick Gold Plc. He currently chairs the Governing Council of the University of Dodoma, a public University. Since January, 2012, he serves as President of the Society for International Development (SID). Ambassador Mwapachu holds a Bachelor of Laws Degree from the University of East Africa, Dar es Salaam, a Post graduate Degree in International Law from the Indian Academy of International Law, New Delhi, Doctorate degrees (Honoris Causa) in literature from the University of Dar es Salaam and political sciences from the National University of Rwanda. Kenya has decorated him with the third highest award, the Order of Moran of the Golden Heart (MGH).


3. Ms. Jill Bishop
Ms. Bishop is the Executive Director of Tanzania Education Trust Foundation and President of Tanzania based BSI Ltd., a consultancy that provides strategic advisory services to government, philanthropic and private sector entities, with an emphasis on strategic planning and visioning; partnership formation; program management; and creative problem solving in developing economies. She has over 20 years of expertise in global business development and macroeconomic policy and has worked extensively with governments and private sector firms throughout Africa on a myriad of development initiatives. With a niche expertise in developing and implementing innovative strategies in challenging environments, BSI combines practical global business development experience with inventive future-oriented solutions to enable continued growth and development of its clients. BSI is based in Dar es Salaam, Tanzania.

Ms. Bishop has assisted numerous philanthropic organizations and foreign direct investors with their engagement with Africa, as well as African governments with facilitating international market access. Most recently she served as the Program Manager for the Tanzania Beyond Tomorrow Project of behalf of the Government of Tanzania, overseeing project development and managing multiple multinational business relationships in an effort to create global partnerships for ICT use in education delivery. She previously served as the President of GlobalXccess where she became a patented inventor of financial services products for underserved markets. She has also held several management consulting positions with Deloitte & Touche Consulting where she led a variety of methodology-based consulting projects in Business Process Reengineering, Strategy, and System Integration. Ms. Bishop holds an Executive MBA from the London School of Economics and Political Science; the HEC School of Management, Paris; and the New York University Stern School of Business (TRIUM). She has an undergraduate degree in Economics and Finance from Rutgers University.


4. Mr. Betram Eyakuze

Mr. Eyakuze is a Partner and Co-founder of Serengeti Advisers Limited, a Tanzanian-based consultancy. Previously he was a private equity investment professional with CDC Capital Partners, a British company with significant investments across Africa and other developing countries. Prior to returning to Tanzania with CDC, he was a management consultant with Mitchell Madison Group in New York, where he was a member of a number of engagement teams that assisted in strategy formulation and improving the operational efficiency of large multinational companies. Clients included the largest U.S telecommunications provider, a global insurance group, and a leading technology-products manufacturer. His responsibilities with CDC Capital Partners in Tanzania included the detailed review and improvement of dozens of business plans across all economic sectors with a view to identifying, structuring, negotiating, and completing equity investment opportunities, typically in already-existing enterprises. Mr. Eyakuze has extensive expertise in business development, strategy formulation, and corporate finance.

He is currently involved in the development of a large-scale agro-industrial project as well as a mineral processing venture in Tanzania, and serves on the boards of a number of national businesses, including a microfinance company and a leading pharmaceutical distribution company. Mr. Eyakuze received his B.A.S in Civil Engineering and Economics from Stanford University and his M.B.A from Yale University School of Management.

5. Mr. Edward V.K. Jaycox
Mr. Jaycox is a retired Managing Director of Emerging Markets Partnership (EMP) and the CEO of the US$ 400 million AIG African Infrastructure Fund which he, and others, founded in 1999. Prior to joining EMP, Mr. Jaycox served as Vice President of the World Bank in charge of the Bank’s operations in Sub-Saharan Africa from 1984 to 1996. During this period, he managed the design and negotiation of structural adjustment programs in over thirty African countries and approved over US$30 billion in loans and credits to support economic policy reform and projects in all of the major sectors.

Mr. Jaycox is deeply familiar with Africa’s economic environment and history and intricacies of market reforms in the continent. Earlier, Mr. Jaycox directed the World Bank’s programs in East Asia and led the team that brought China into the World Bank. He also managed the first structural adjustment programs supported by the World Bank in Thailand and South Korea. For over 15 years of his more than 30 years with the World Bank, he appraised projects and managed technical teams, divisions and departments working in the infrastructure sectors including roads, ports, airports, pipelines, railways, waterways, and urban infrastructure, such as water, electricity, expressways, rapid transit and housing.

Mr. Jaycox has an A.B. degree from Yale College and an M.A. degree from Columbia University School of International Affairs and Certificate in African Studies from its African Institute.

6. Mr. January Y. Makamba
Mr. Makamba is the founder-director of Bumbuli Development Corporation and current Member of Parliament for Bumbuli constituency and the Deputy Minister for Communication Science and technology in the government of Tanzania. Before his appointment as a Deputy Minister, he served as a Chairman of a Parliamentary Standing Committee on Energy and Minerals and Deputy Chairman of the Board of Director of the Tea Board of Tanzania. Before being elected as a Bumbuli Constituency representative in the Tanzanian parliament, Mr. Makamba was working at the country’s highest office as a senior Aide to Tanzanian President Jakaya Kikwete for 5 years from 2005-2010. Mr. Makamba started government service as a civil servant where he worked as Foreign Service Officer at the Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation.

Mr. Makamba attended St. Johns University in Minnesota, USA, where he obtained a degree in Peace and Conflict Studies after which he joined the Jimmy Carter Presidential Center, in Atlanta, Georgia, as Research Assistant where he also spent some time in Sierra Leone. He was later enrolled for a Master of Science degree in Conflict Analysis and Resolution at George Mason University in Virginia after the completion of his assignment at the Carter Center. Mr. Makamba has also worked in humanitarian assistance operations as Assistant Camp Manager in the Burundian refugee camps in Kigoma, Tanzania, overseeing the welfare of 120,000 Burundi refugees.


7. Dr. Najim Msenga
Dr. Najim is a native and resident of Bumbuli and one of the most successful entrepreneurs in Bumbuli township. Born and raised in Bumbuli, he has invested in trading, transport and housing in Bumbuli and gemstones business across Tanzania. He is the Executive Director of Najim and Company Ltd, and Kimmse Investment Ltd. ??In 1993 he was awarded the honorarium title of Doctorate after discovering the Green Sapphires in Tanga, Tanzania.

8. Bishop Dr. Stephen Munga
Bishop Munga is a Lushoto-based Bishop of the Evangelical Lutheran Church in Tanzania for the Northern-Eastern Diocese. Bishop Dr. Munga is on a number of committees of the Evangelical Lutheran Council in Tanzania (ELCT) since 2001 when he was elected the Bishop of ELCT North Eastern Diocese. Bishop Dr. Munga .was the first Chairperson of Sebastian Kolowa University College and now is the Chancellor of Sebastian Kolowa Memorial University; is the Chairperson of The Lutheran Mission Corporation; Policy, Finance and Planning Committee of the Christian Council of Tanzania.

Bishop Dr. Munga is a recognised leader in community development in Lushoto. He has been an ardent advocate for environmental protection and sustainable livelihood in the Usambara Mountains. He is also a national leader and activist for the sound management and governance of Tanzania’s natural resources, serving in the national committee of the Extractive Industries Transparency Initiative. He also chaired the Interfaith Standing Committee on Economic Justice and the Integrity of Creation.

Bishop Munga obtained his Doctorate of Theology from the University of Lund, Sweden.

9. Ms. Grace C. Rubambey
Ms. Grace Rubambey is a rural and microfinance expert and former director of the Bank of Tanzania. She holds a BBA (Economics) and a MA (Economics) degrees from Kent State University, Kent, Ohio, USA. Ms. Rubambey has more than 35 years experience in financial issues, policy formulation, program coordination, institution building, and training. She worked at the Bank of Tanzania for more than 28 years, 24 of which were in various management positions, including Manager Economic Research and Statistics, Director of Rural Finance, Director of Financial Markets and Director of Microfinance. While seconded from the Bank of Tanzania, she also served as the first non-FAO Secretary General of the Nairobi-based Africa Rural and Agricultural Credit Association (AFRACA) for five years from 1984 to 1989. In recognition of her work at AFRACA and her personal commitment in the development of rural and microfinance in Africa, in 2006, the Government of Burkina Faso awarded her Knighthood of the National Order (Chevalier de L’ordre National).

Ms. Rubambey, a staunch advocate of rural/microfinance and inclusive financial services in general, has been credited for spearheading the development of rural and microfinance in Tanzania, in particular the Bank of Tanzania’s critical intervention in the sector at a time when the subject was little known in the country and the region as a whole. She established the Directorate of Micro-finance at the Bank of Tanzania and headed it for more than seven, until her retirement. She led the national team that drafted the Tanzania’s National Microfinance Policy, a policy that was internationally acknowledged as one of the best in the industry. She also led the national Task Force that drafted the regulatory, legal and supervisory framework for micro-finance in Tanzania.

Ms. Rubambey has served on a number of boards and policy development committees, including the Financial Sector Deepening Trust (FSDT) Tanzania National Economic Empowerment Council and the Advisory Board to the President’s Empowerment Fund.

10. Prof. Andrew Temu
Prof. Andrew Temu is an Associate Professor at the Department of Agricultural Economics and Agri-business, Sokoine University of Agriculture in Morogoro, Tanzania. Prof. Temu has in the past undertaken Visiting and Research Fellowships at the University of Illinois, Urbana Champaign-USA and the International Food Policy Research Institute, Washington DC, USA. He has also managed the SADC Food Security Training Programme in the 14 member countries.

Prof. Temu has extensive knowledge of agri-business projects appraisal and agricultural finance, privatisation, divestiture of agricultural parastatals and private sector development, and in designing, analysing and evaluating agricultural policies and strategies. He has participated actively in the development of the Agriculture Sector Development Strategy and the Agriculture Sector Development Programme for Tanzania.

Prof. Temu has researched, published and offered consultancy services in a wide range of areas related to agricultural production, marketing, trade and rural development. He is also the Chairman of the Board of Trustees of the Private Agricultural Sector Support (PASS) Trust. He is a board member in a number of organizations, including the African Guarantee Fund Ltd; Tanzania Investment Center; the Southern Agriculture Growth Corridor of Tanzania (SAGCOT); the Economic and Research Foundation. He has in the past also served as a Board member of The CRDB Bank and its subsidiary pursuing Microfinance Services. He is a Founder Chairman of Diligent Consulting Ltd, a private Tanzanian consulting firm.

Prof. Temu has a BSc in Agriculture from the Sokoine University of Agriculture in Morogoro, Tanzania, an MSc. in Agricultural Economics from Reading University in UK, and a PhD in Agricultural Economics from the London University in UK.

I am grateful to all these individuals for agreeing to serve in the Board, and therefore take part in the advancement of the welfare of the people of Bumbuli and Tanzania in general. The cumulation of members’ vast experiences, many accomplishments and diverse backgrounds makes this a formidable team. This is a clear statement on our part at BDC that we intend to create a world-class organisation aiming for excellence and governed by the highest ethical standards. Today, with the appointment of this board, we have taken one more step towards the realisation of the dream and the promise of transformation of Bumbuli.


January Makamba (MP)
Bumbuli Constituency
6 September 2012

Saturday, September 1, 2012

TGNP YALAANI KAULI ZA DC WA KOROGWE

DC Korogwe awajibishwe kwa udhalilishaji

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), tumesikitishwa sana na kauli iliyotolewa na Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga Ndugu Mrisho Gambo, kwa mwanasheria wa Halmashauri hiyo Bi. Najum Tekka, kuhusu uhalali wa shahada aliyonayo hususan kuihusisha shahada hiyo na vitendo vya ngono! Kama ilivyoripotiwa na vyombo vya habari ikiwepo gazeti la Majira Augosti 29,2012 Uk.3

Kauli hii ni udhalilishaji na ukiukwaji mkubwa wa haki za wanawake na inaenda kinyume na misingi ya kuzingatia usawa sanjari na Katiba ya nchi ; Uwezeshaji wa wanawake na utekelezaji wa Maazimio ya Haki na Usawa katika ngazi za Kimataifa Kikanda na Nchini Tanzania.

Aidha kauli hii, inalenga kupotosha na kukatisha tamaa juhudi kubwa wanazofanya wanawake na wasichana katika kupata elimu na mafanikio mbalimbali nchini Tanzania. Zaidi ya hapo, kauli hii inadhalilisha na kushusha hadhi ya vyuo vya elimu ya juu vinavyofanya kazi kubwa ya kutoa elimu kwa Watanzania.

Kutokana na kauli hiyo DC amekiuka maadili ya uongozi wa umma na kukidhalilisha kiti cha ukuu wa wilaya na kiongozi Mkuu wa nchi aliyemteua kushika wadhifa huo. Aidha kauli ya kiongozi huyo ya kutimia mahakama kutetea hoja yake , kunaashiria ubabe , ujeuri, vitisho, kiburi na dharau ya kutaka kuingilia uhuru wa mahakama na ajenda binafsi isiyokuwa na maslahi kwa wanawake na umma wa Watanzania

Kutokana na kauli hiyo ya udhalilishwaji ,sisi wanaharakati wa ukombozi wa wanawake Kimapinduzi, usawa wa kijinsia, haki za kibinadamu demokrasia tunalaani vikali kauli za DC na kutoa Rai ifuatayo:

1. Mkuu wa Wilaya Ndugu Mrisho: amwombe radhi Mwanasheria Bi. Najum Tekka, kwa kosa la kumdhalilisha kijinsia

2. Tume ya maadili ya utumishi wa umma, na Mamlaka nyingine za kinidhamu zimchukulie hatua za kinidhamu Ndugu Gambo kwa kutumia lugha ya kudhalilisha watumishi kinyume na maadili.

3. Wanawake wote, wanaume, vijana wa kike na kiume kuendelea na mapambano dhidi ya mfumo dume na mifumo yote kandamizi, kushikamana katika kudai misingi ya kisheria, uwajibikaji inayozingatia usawa na haki na kukataa kudhalilishwa katika ngazi binasfi na za umma !.

Imetolewa
Dar es salaam leo 31/08/2012 na:
Usu Mallya
Mkrugenzi Mtendaji TGNP

Monday, August 6, 2012

MKUTANO WA WANABUMBULI JIJINI DAR ES SALAAM

Wakazi kutoka jimbo la bumbuli wakiwa katika mkutano huo wa kujadili maendeleo ya wilaya ya Bumbuli
Mbunge wa jimbo la Bumbuli na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. January Makamba akiongea na wakazi kutoka wilaya ya Lushoto jimbo la Bumbuli katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam jana mkutano huo ulikuwa unajadili maendeleo ya jimbo la Bumbuli na kutambulisha shirika la maendeleo la Bumbuli, January Makamba amesema katika kipindi cha mwaka 2011-2012 kiwango cha elimu ya wilaya hiyo imekuwa chini na kusababisha vijana wengi katika mkoa wa Tanga kuwa na sifa ya kuuza chipsi na kubeba mizigo badala ya kufanya kazi kwenye makampuni.
Katibu wa CCM wilaya ya Lushoto Bw. Loth Ole Lemeirut (kushoto)na mwanakamati wa shirika la Bumbuli Bw. Naaman Shauri wakifuatilia kwa umakini mada iliokuwa ikendelea katika mkutato huo leo
Mkurugenzi wa shirika la Bumbuli Bw. Najim Msenga (kushoto), mwenyekiti mteule wilaya ya Bumbuli Bw. Amiri Sheiza (kulia)katibu wa CCM wilaya ya Lushoto Bw. Loth Ole Lemeirut (katikati)wakijadiliana jambo mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo jana
Kikundi cha ngoma kijulikanacho Mount Usambara Voice kikitoa burudani katika mkutano huo

Sunday, July 29, 2012

UZINDUZI WA YA RAMADHAN CARE & SHARE YA VODACOM MKOANI-TANGA

Mkuu wa Wilaya ya Tanga Bi.Halima Omary Dendego wapili toka kushoto na Mkuu wa Vodacom Foundation Bw.Yessayta Mwakifulefule wakishuhudia wakati Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania,Bw.Hassan Saleh,akimkabidhi madafutari mtoto anaeishi kwenye mazingira magumu mkoani Tanga Juma Hassan,wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ramadhan Care & Share iliyozinduliwa mjini humo ikiwa na lengo la kufuturisha watoto yatima zaidi ya 500 sehemu mbalimbali nchini wakati huu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga mjini Bi.Halima Omary Dendego (kushoto)akishuhudia Ofisa Mkuu wa mauzo na usambazaji wa Vodacom Tanzania Bw.Hassan Saleh akimkabidhi madafutari Zainabu Omary ambae ni mtoto anaeishi katika mazingira magumu mkoani Tanga wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ramadhan Care & Share iliyozinduliwa mjini humo ikiwa na lengo la kufuturisha watoto yatima zaidi ya 500 sehemu mbalimbali nchini wakati huu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan,katikati ni Mkuu wa wa Kampeni hiyo inayoendeshwa na Vodacom Foundation Bw.Yessaya Mwakifulefule.
Ofisa Mkuu wa mauzo na usambazaji wa Vodacom Tanzania,Bw.Hassan Saleh akimkabidhi ndoo ya mafuta ya kula mmoja wa watoto wanaoishi katika mazingira magumu mjini Tanga,Aisha Mohamed,wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ramadhan Care & Share 2012 inayolenga kufuturisha watoto yatima zaidi ya 500 sehemu mbalimbali nchini wakati huu wa mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan,anaeshuhudia watatu kutoka kulia ni Mkuu wa Kampeni hiyo inaendeshwa na Vodacom Foundation Bw.Yessaya Mwakifulefule.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga mjini wapili toka kushoto Bi.Halima Omary Dendego akikabidhi mbuzi pamoja na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania,kwa watoto yatima wa mkoani humo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ramadhan Care & Share mjini humo inayolenga kufuturisha watoto yatima zaidi ya 500 sehemu mbalimbali nchini wakati huu wa mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan,Kampeni hiyo inaendeshwa na Vodacom Foundation.
Imam Mkuu wa Masjid ma’amour ya upanga Dar es Salaam Shekh Issa Othman kushoto akisalimiana na Meneja Mahusiano wa Vodacom Tanzania Bw. Matina Nkurlu, wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ramadhan Care & Share iliyozinduliwa mkoani Tanga,ikiwa na lengo la kufuturisha watoto zaidi ya 500 sehemu mbalimbali nchini wakati huu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan,katikati ni Mkuu wa Vodacom Foundation Bw.Yessaya Mwakifulefule.
Mapokezi
Mkuu wa Vodacom Foundation Bw.Yessaya Mwakifulefule na Meneja Mahusiano wa Vodacom Tanzania Bw.Matina Nkurlu wakiwahudumia watoto wanaoishi katika mazingira magumu mkoani Tanga wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ramadhan Care & Share iliyozinduliwa mkoani humo ikiwa na lengo la kufuturisha watoto zaidi ya 500 sehemu mbalimbali nchini wakati huu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga akiwa kwenye uzinduzi huyo…

Zoezi la Epiq Bongo Star Search mkoa wa Tanga

Mshiriki wa Shindano la Epiq Bongo Star Search Digna Mbetela kutoka Dodoma akiwa mbele ya majaji wa shindano hilo (hawapo pichani) walipokuwa wakifanya mchujo mkoani Tanga katika Ukumbu wa Club La Casa Chika Julai 28,2012 na mwana dada huyo kujitosa tena kujaribu bahati yake ya kwenda jijini Dar es Salaam.

Mwamko wa washiriki katika shindano la Zantel Epiq Bong Star Search umekuwa kama ulivyotegemewa ambapo zaidi ya washiriki 300 walikuwa wameisha jisajiri kwanza kwa ajiri ya kufanya usaili siku ya leo.

Washiriki wengi walioshindwa kupata nafasi katika mikoa usaili uliopitiawamejitokeza katika mkoa wa Tanga kitu ambacho kimeongeza ushindani kwawashiriki kutokea eneo hili la Tanga.
Washiriki wa EBSS wakiwa nje ya ukumbi wa Club la Casa Chika jijini Tanga tayari kwa kufanya usaili na kupatiwa namba zao kusubiri kuingia kwa majaji.
Mshewa Mussa akiwakilisha tena baada ya kete yake ya awali mkoani Arusha kugonga mwamba na kuamua kutia maguu jijini Tanga kujaribu bahati yake.
Washiriki wa EBSS wakiwa nje ya ukumbi wa Club la Casa Chika jijini Tanga kusubiri kuingia kwa majaji.
Faisal Jafari wa kutoka Tanga nae akisubiri kurusha kete yake kwa majaji.
Mshiriki Hidaya Hanein akiwa katika foleni ya kuingia kwa majaji

Wednesday, July 25, 2012

Vodacom Tanzania yazindua Ramadhan Care & Share 2012 Mkoani Tanga

002: Msaidizi wa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Bw Josephat Sura akiagana na Meneja Mahusiano ya nje wa Vodacom Tanzania Bw. Salum Mwalim wakati Meneja huyo alipomtembelea Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh. Chiku Gallawa.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh. Chiku Gallawa akizungumza na Meneja Mahusiano ya Nje wa Vodacom Tanzania Bw. Salum Mwalim alipomtembelea ofisini kwake kwa lengo la kusalimiana na kumpatia taarifa rasmi za hafla ya kufuturisha watoto yatima zaidi ya 500 inayoandaliwa na Vodacom Foundation jijini humo.
Meneja Mahusiano ya Nje wa Vodacom Tanzania Bw. Salum Mwalim akizungumza moja kwa moja na wakazi wa Mji wa Tanga na mikoa ya jirani kupitia kituo cha Radio Mwambao FM kuhusu futari iliyoandaliwa na Vodacom Foundation kwa watoto yatima zaidi ya 500 wa jijini Tanga leo Jumatano Julai 25, 2012.
Meneja Uhusiano kwa Umma wa Vodacom Tanzania Bw. Matina Nkurlu akifafanua jambo kwa Meneja wa Radio Mwambao FM ya Jijini Tanga Bw. Hashim Gulamwa (Katikati) na Mkuu wa Vodacom Foundation Bw. Yessaya Mwakifulefule wakati maofisa wa Vodacom walipotembelea kituo hicho leo Jumatano Julai 25, 2012 na kuzungumzia program ya Vodacom Foundation ya Ramadhan Care & Share 2012 inayolenga kufuturisha watoto yatima sehemu mbalimbali nchini wakati huu wa mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
--
Kampuni ya Vodacom Tanzania leo inafuturisha zaidi ya watoto mia tano kutoka madrasa za mjini na nje ya mji wa Tanga katika viwanja vya Ma-awal Islamic ikiwa ni uzinduzi rasmi wa utaratibu wake wa kila wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhan wa kujali na kuonesha upendo kwa watoto yatima na makundi yasiyojiweza kwenye jamii – Ramadhan Care & Share

Futari hiyo inayoandaliwa na Vodacom kupitia kitengo chake cha misaada kwa jamii – Vodacom Foundation itahudhuriwa pia na viongozi mbalimbali wa dini ya kiislamu na viongozi wa serikali mkoa wa Tanga

Mapema jana Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mheshimiwa Chiku Gallawa alitoa baraka zake kwenye futari hiyo alipotembelewa ofisini kwake na Meneja Mahusiano ya Nje wa Vodacom Bw. Salum Mwalim na Meneja Mahusiano kwa Umma Bw. Matina Nkurlu kwa lengo la kusalimiana.

“Utaratibu wa kuwakumbuka yatima ni utaratibu mzuri nawapongeza Vodacom kwa upendo wenu nasikitika sana kwamba sitokuwepo kama nilivyowaeleza wakati mliponitumia ujumbe wa mualiko kwamba nitakuwa safarini Wilayani Handeni kikazi, ila nawatakia kila la kheri na nitawakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mheshimiwa Halima Dendegu”Alisema Mh. Gallawa

Chini ya utaratibu huo Vodacom Tanzania pia itafuturisha watoto yatima na wa-Madrasa katika miji mbalimbali nchini sanjari na utoaji wa sadaka za vyakula na vifaa vya shule kwa watoto hao.

Monday, July 16, 2012

TAMASHA LA WAJANJA WA VODACOM MKOANI TANGA

Msanii Machachari wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platinum akionyesha umahiri wake wa kucheza wakazi wa jiji la Tanga wakati wa Tamasha la Wajanja wa Vodacom lililofanyika katika uwanja wa Mkwakwani mjini humo,likiwa na lengo la kuuelimisha uma kutumia mtandao wa Vodacom kwa kuongea kwa robo shilling na kutuma ujumbe kwa shilingi 25 kwenda mtandao wowote na kuperuzi facebook na twitter bure.
Msanii Mahiri wa Hip Hop Joh Makini akiwapagawisha ilivyo wakazi wa jiji la Tanga wakati wa Tamasha la Wajanja wa Vodacom lililofanyika katika uwanja wa Mkwakwani mjini humo,likiwa na lengo la kuuelimisha uma kutumia mtandao wa Vodacom kwa kuongea kwa robo shilling na kutuma ujumbe 25 kwenda mtandao wowote na kuperuzi facebook na twitter bure.
Msanii wa kizazi kipya Ommy Dimpoz akiwapagawisha wakazi wa jiji la Tanga wakati wa Tamasha la Wajanja wa Vodacom lililofanyika katika uwanjha wa Mkwakwani mjini humo,likiwa na lengo la kuuelimisha uma kutumia mtandao wa Vodacom kwa kuongea kwa robo shilling na kutuma ujumbe kwa shilingi 25 kwenda mtandao wowote na kuperuzi facebook na twitter bure.
Msanii wa kizazi kipya Mabeste akikamua vilivyo na kuwapagawisha wakazi wa jiji la Tanga wakati wa Tamasha la Wajanja wa Vodacom lililofanyika katika uwanja wa Mkwakwani mjini humo,likiwa na lengo la kuuelimisha uma kutumia mtandao wa Vodacom kwa kuongea kwa robo shilling na kutuma ujumbe kwa shilingi 25 kwenda mtandao wowote na kuperuzi facebook na twitter bure.
Msanii wa kizazi kipya Nay wa Mitego akiwapagawisha wakazi wa jiji la Tanga wakati wa Tamasha la Wajanja wa Vodacom lililofanyika katika uwanja wa Mkwakwani mjini humo,likiwa na lengo la kuuelimisha uma kutumia mtandao wa Vodacom kwa kuongea kwa robo shilling na kutuma ujumbe kwa shilingi 25 kwenda mtandao wowote na kuperuzi facebook na twitter bure.
Mtaalam wa Mitambo Haroun a.k.a Dj Run akifanya vitu vyake wakati wa Tamasha hilo.
Nyomi ya wakazi wa jiji la Tanga waliojitokeza katika Taamasha la Wajanja wa Vodacom.
----
Tanga 15 Julai 2012.

Kampuni ya Mawasiliano mu za mkononi ya Vodacom Tanzania imefanya tamasha la wajanja tour mwishoni mwa wiki hii mkoani Tanga ikiwa ni kukamilisha msimu wa kwanza wa tour hiyo ambayo ilizinduliwa Dar Es Salaam na baadae kufanyika Mji kasoro bahari morogoro, Mtwara na sasa Mkoani Tanga.

Akizungumza na waandishi wa habari Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania Matina Nkurlu alisema kuwa tamasha hilo lilifanyika katika uwanja wa mkwakwani ikiwa ni katika kukamilisha msimu wa kwanza wa mfululizo wa matamasha yaliyofanyika katika mikoa mbalimbali ya Tanzania.

“Tamasha hili la Mkoa wa Tanga katika uwanja wa Mkwakwani lilifanyika katika kukamilisha msimu huu wa kwanza. Tunajipanga kwa ajili ya msimu wa pili wa kutoa burudani kwa watanzania. Tunawahakikishia wateja wetu kuwa tamasha hili halitaishia hapa, tunaangalia namna ya kwenda katika mikoa mingine kwani watu wengi wamevutiwa na burudani wanayoipata hivyo tunaangalia uwezekano wa kwenda mikoa mingine ya Tanzania bara na visiwani,” alisema Nkurlu.

“Lengo la Tamasha la Wajanja Tour sio tu kutoa burudani, pia ni njia pekee ya kuwapa vijana nafasi ya kuonyesha vipaji vyao na kupata nafasi ya kuendelea vipaji vyao zaidi kama ambavyo mmeshuhudia katika matamasha mbalimbali vijana wengi wamepata nafasi ya kuonyesha vipaji vyao kwa kuimba,” alisema.

Tamasha la Wajanja wa Vodacom limekuwa na lengo la kuwahamasisha vijana kujiunga na kupata huduma kutoka mtandao wa Vodacom Tanzania ambapo kampuni hiyo imeanzisha huduma mbalimbali ambazo zinaweza kurahisisha matumizi ya simu kwa kuongea kwa robo shilingi,kutuma ujumbe kwa shilingi ishini na tano kwenda mtandao wowote hapa nchini na kuperuzi facebook na twitter bure,Pia wateja wa Vodacom wananufaika sana na huduma ya intanet hasa vijana ikiwemo ofa ya wajanja intanet inayompa mteja huduma ya intaneti kwa shilingi 250 kwa siku, pamoja na ofa ya simu za Nokia Asha kwa shilingi elfu sabini na tano tu.

Mwisho

Sunday, July 15, 2012

MAANDALIZI YA JUKWAA LA TAMASHA LA WAJANJA WA VODACOM MKWAKWANI JIJINI TANGA

Hili ndilo jukwaa la Tamasha la Wajanja wa Vodacom likiwa linaandaliwa katika uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga,wakazi wa Tanga njoeni kwenye tamasha hili litakaloanza leo saa 8 mchana mpaka saa 12 jioni.Fid Q,Diamond,Shetta,Mabeste,Nay Wamitego,Ommy Dimpozi,Wasanii wote hawa watapanda jukwani leo hii,Tamasha hili lina lengo la kuwahamasisha vijana kujiunga na kupata huduma kutoka mtandao wa Vodacom Tanzania,ambapo unaweza kunufaika kwa kuongea kwa robo shilingi,kutuma ujumbe kwa shilingi ishini na tano kwenda mtandao wowote hapa nchini na kuperuzi facebook na twitter bure,Pia huduma ya intanet hasa vijana ikiwemo ofa ya wajanja intanet inayompa mteja huduma ya intaneti kwa shilingi 250 kwa siku.
Baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom wakijipanga namna ya kuweka mambo sawa kwenye tamasha la Wajanja wa Vodacom leo jijini Tanga katika uwanja wa Mkwakwani,Tamasha hilo litaanza saa 8 mchana mpaka saa 12 jioni.Fid Q,Diamond,Shetta,Mabeste,Nay Wamitego,Ommy Dimpozi,Wasanii wote hawa watapanda jukwani leo hii,Tamasha hili lina lengo la kuwahamasisha vijana kujiunga na kupata huduma kutoka mtandao wa Vodacom Tanzania,ambapo unaweza kunufaika kwa kuongea kwa robo shilingi,kutuma ujumbe kwa shilingi ishini na tano kwenda mtandao wowote hapa nchini na kuperuzi facebook na twitter bure,Pia huduma ya intanet hasa vijana ikiwemo ofa ya wajanja intanet inayompa mteja huduma ya intaneti kwa shilingi 250 kwa siku.

Sunday, July 8, 2012

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU SHIRIKA LA MAENDELEO BUMBULI

Napenda kuwatangazia wana-Bumbuli kwamba ile ahadi niliyotoa wakati wa kampeni – ahadi ya kuanzisha Shirika la Maendeleo Bumbuli – imetimia. Shirika limepata usajili, limefungua ofisi, lina watumishi wa mwanzo na tayari ipo miradi minne ambayo utekelezaji wake utaanza mara moja. Tutazindua Shirika hili tarehe 4 Agosti 2012, katika mkutano wangu na wana-Bumbuli waishio Dar es Salaam na mikoa ya jirani, na baadaye katika mikutano na wananchi jimboni Bumbuli.

Chimbuko

Nilipoamua kugombea Ubunge wa Bumbuli mwaka 2010, niliamua kwamba katika utumishi wangu kama Mbunge nitashirikiana na Wana-Bumbuli pamoja na marafiki na washirika wa maendeleo wa ndani na nje ya nchi katika kuleta mageuzi ya kiuchumi na kijamii Bumbuli. Jimbo letu ni kati ya majimbo yaliyo nyuma kimaendeleo kwa kiasi kikubwa na hivyo kuhitaji jitihada za ziada – zaidi ya zile za Serikali. Katika kufikia lengo hilo, niliahidi kuanzisha Shirika litakaloratibu shughuli za maendeleo katika Jimbo.

Nilifikia uamuzi wa kuanzisha Shirika nikitambua kwa dhati uwepo wa jitihada nzuri za serikali katika kuboresha maisha ya watu wa Bumbuli nikitegemea pia serikali kuendeleza jitihada zaidi. Hata hivyo natambua kwamba kazi ya maendeleo si kazi ya serikali pekee, inahitaji ushiriki wa kila mmoja na hasa sekta binafsi ili kuisadia juhudi za serikali kufikia malengo ya maendeleo. Nilitaka kuchambua uwezo wa watu binafsi, wafanyabiashara na taasisi mbalimbali katika kupanua wigo wa ajira na shughuli za kipato kwa watu wa Bumbuli kupitia uwekezaji katika jamii.

Mpango wa Mageuzi Bumbuli

Mpango huu ulitokana na mawazo niliyokuwa nayo nilipoamua kugombea ubunge juu ya haja kuunganisha jitihada za wenyeji wa Bumbuli, wafanyabiashara na taasisi za hapa nchini, na wawekezaji kutoka nje katika kufanikisha mageuzi ya kijamii na kiuchumi. Niliamini jitihada za sekta binafsi zikioana na mipango ya maendeleo ya serikali kutachochea kasi ya ukuaji wa uchumi wa wana-Bumbuli na hivyo kupanua wigo wa ajira na shughuli za kibiashara za uzalishaji mali katika Jimbo.

Malengo ya mpango wa kuikwamua Bumbuli kupitia uwekezaji katika jamii ni kama ifuatavyo:

1. Kuongeza pato la wakulima wa Bumbuli kutokana na mazao wanayovuna kwa kuboresha mbinu za kilimo, mbinu za kuhifadhi mazao, na hatua mahsusi za kuongeza thamani ya mazao hayo (value-addition).

2. Kuwavutia wawekezaji kujenga taasisi au shule itakayokuwa na wanafunzi, walimu na wafanyakazi wengine watakaotumia bidhaa zinazozalishwa Bumbuli, hivyo kutengeneza ajira na fursa za kujiongezea kipato kwa wananchi.

3. Kuleta huduma za kifedha kwa kuanzisha taasisi ya fedha Bumbuli ambayo hatimaye itakuwa benki ya wananchi wa Bumbuli ambayo itatoa mikopo kwa masharti nafuu.

4. Kuchukua hatua mahsusi za kuhifadhi mazingira ya Milima ya Usambara kwani maisha na maendeleo ya kiuchumi ya watu wa Bumbuli yanategemea sana mazingira na mandhari ya milima ya Usambara.

5. Kuanzisha Shirika la Maendeleo Bumbuli litakalokuwa na jukumu la kubuni, kuratibu na kusimamia uendeshaji wa shughuli zilizoainishwa hapo juu. Shirika hili ndilo litakalokuwa kiini cha mtandao wa kijamii wa uchumi kwa Bumbuli.
Malengo haya yamekusudiwa kuwanufaisha wananchi kwa kuanzisha mtandao wa kimataifa wa kibiashara ambapo wadau mbalimbali watashiriki; na hatamu za uchumi zikishikiliwa na watu wa Bumbuli wenyewe.

Shirika la Maendeleo Bumbuli

Shirika la Maendeleo ya Bumbuli ni shirika la maendeleo lisilotengeneza faida lenye lengo la kukuza uchumi na kuchochea maendeleo ya Jimbo. Shirika hili limesajiliwa kama kampuni yenye ukomo wa dhamana, na litafanya biashara ili kulipia gharama za uendeshaji na faida inayopatikana itatumika kugharamia miradi ya maendeleo ili kufikia malengo ya kijamii ya Mkakati wa Mageuzi ya Uchumi wa Bumbuli. Shirika litakuwa na kazi zifuatazo;

1. Kuihamasisha sekta binafsi kushiriki katika maendeleo ya Bumbuli kwa kuwekeza katika maeneo mblimbali. Uwekezaji huu utahusisha wafanyabiashara wa ndani na wale wa kigeni na Shirika litajihusisha zaidi katika kutoa msaada wa kitaalamu, na kuratibu mtandao wa kibiashara utakaoenea kuanzia ngazi ya wilaya, taifa na kimataifa.

2. Kubuni na kuitangaza ‘Chapa Lushoto’ (Lushoto Brand) pamoja na kutayarisha mafunzo kwa wakulima juu ya kutayarisha mazao yao ili yapate kuwa na thamani bora zaidi. Shirika hili litajenga mfumo utakaosaidia kununuliwa kwa mazao ya wakulima na masoko ya bidhaa, muundo utakaotumiwa na wafanyabiashara binafsi.

3. Kuvutia uwekezaji kwa njia ya kuitangaza Bumbuli pamoja na kuishauri halimashauri na serikali za mitaa kuhusu maeneo ya kuwekeza na miundombinu ya kuboresha ili kuvutia uwekezaji zaidi.

4. Kutafuta fedha kwa ajili ya uwekezaji wa kijamii na kibiashara na kutoa msaada wa kihuduma kwa makampuni ya biashara ya nyumbani na uwekezaji wa kutoka nje.

5. Kuratibu mipango ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya wadau mbalimbali wa maendeleo Bumbuli.

6. Kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika mpango wa Maendeleo na Mpango wa uwekezaji.
Shirika litaongozwa na bodi itakayokuwa na watu kati ya nane na kumi na moja na kuendeshwa na timu ya watu watano ambao watakuwa ni, Mkurugegenzi Mtendaji, Mweka Hazina, Wachambuzi wawili na Mhasibu.

Miradi ya Mwanzo ya Shirika la Maendeleo Bumbuli


1. Mradi wa Kituo cha Kukusanya, Kusafisha, Kugredi, Kupaki na Kutafuta Masoko ya Mboga na Matunda ya Bumbuli (Bumbuli Packing House)

Wilaya ya Lushoto, jimbo la Bumbuli likiwemo, inasifika kwa kilimo cha mboga na matunda. Hata hivyo, asilimia hamsini (50%) ya mboga na matunda yanayolimwa Bumbuli yanaharibika – kwa kutokufika sokoni au kutopata soko la uhakika. Hata yale mazao yanayonunuliwa, wakulima wanapata mapato kidogo sana ambayo hayaendani na thamani ya jasho lao.

Mradi wa Bumbuli Packing House, ambao utajiendesha kibiashara, una dhamira ya kumaliza tatizo hili. Pamoja na hili mradi huu utawawezesha wakulima kwa pembejeo – mbegu, mbolea, pampu, nk – na mafunzo ili wazalishe mboga na matunda bora zaidi ya kukidhi mahitaji ya soko la kimataifa.

Mradi huu, katika awamu ya kwanza, utagharimu shilingi milioni 780. Utafiti wa Kibiashara (Market Analysis Survey) umefanyika, Andiko la Kibiashara limekamilika. Na majadiliano na wadhamini kupata fedha hizi yamefikia mwisho ambapo ndani ya mwezi mmoja fedha hizo zitapatikana, na baada ya maandalizi kukamilika (ikiwemo kupata professional management), mradi utaanza.

2. Mradi wa Kiwanda cha Kusindika Mboga na Matunda

Shirika liko katika hatua za mwisho za mazungumzo ya kukifufua upya kiwanda cha kusindika Mboga na Matunda (Natural Choice) kilichopo Soni, jimbo la Bumbuli, ambacho mwanzoni kwa miaka ya 2000 kilikuwa na sifa kubwa ya kutoa bidhaa nyingi, bora na za thamani kubwa.

Mradi huu utaenda hatua ya mbele zaidi ya Bumbuli Packing House kwa kutengeneza juisi, jams, concentrates na bidhaa nyingine za mboga na matunda kwa ajili ya soko la ndani na nje ya nchi. Mradi huu, sio tu utatoa ajira kwa watu wa Bumbuli, bali pia utahakikisha soko la uhakika kwa mboga na matunda ya Lushoto linapatikana na kuongeza thamani ya mazao ya wakulima na hivyo kuwaongezea kipato.

3. Mradi wa Kutoa Mikopo kwa Masharti Nafuu (Bumbuli Microfinance Institutition)

Jimbo la Bumbuli halina tawi la benki yoyote na huduma ya fedha ni tatizo kubwa. Shirika la Maendeleo Bumbuli limeomba leseni kutoka Benki Kuu kuanzisha taasisi ya fedha kwa ajili ya ukopeshaji kwa masharti nafuu na pamoja na huduma nyingine za fedha. Andiko la Mradi huu limefanywa kitaalam sana, baada ya utafiti wa karibu miezi nane kuhusu njia muafaka ya kutoa huduma ya fedha kwa masharti nafuu kwa watu wa Bumbuli. Mradi huu utagharimu shilingi milioni 450 kwa kuanzia na baada ya miaka mitatu mtaji utaongezwa na kufikia shilingi bilioni 1.6. Wakati tunasubiri usajili na leseni kutoka Benki Kuu tayari wapo wafadhili ambao, baada ya kusoma andiko letu, wameonyesha nia ya kusaidia mradi huu.

Msingi wa mradi huu ni kuwezesha vikundi vya kuweka na kukopeshana fedha ambavyo tayari vipo lakini vina mtaji mdogo, kutoa mafunzo ya fedha kwa vikundi hivi, na kuhamasisha kuanzishwa kwa vikundi vingine. Kipaumbele na nafuu ya mikopo itatolewa zaidi kwa vikundi vitakavyotumia fedha hizi kwa uzalishaji mali na shughuli ambazo zitaajiri watu wengine.

4. Mpango wa Malipo kwa Kufanya Vizuri kwa Shule za Sekondari (Cash-On-Delivery for Secondary Education in Bumbuli)

Shirika la Maendeleo Bumbuli (BDC) litakavyotekeleza program ya msaada ya Malipo kwa kufanya vizuri** au cash on delivery (COD), ambayo itaongeza umakini na tija kwenye kujifunza na matokeo ya mitihani katika shule za sekondari jimboni Bumbuli. Kulingana na utafiti wetu, jimbo la Bumbuli liko kwenye hali ya kukata tamaa ya kupata msaada kwenye Sekta yake ya Elimu ya Sekondari. Shirika la Maendeleo Bumbuli (BDC) litatekeleza program ya majaribio ya malipo kwa kufanya vizuri (COD), ya miaka mitatu ambayo itafanya malipo kulingana na idadi ya wanafunzi ambao wamefaulu Mitihani ya Taifa ya Kidato cha Nne. Shirika la Maendeleo Bumbuli (BDC) linalenga kuboresha matokeo ya kujifunza/elimu katika jimbo la Bumbuli kupitia program hii ya kutoa motisha. Program hii itahusu Shule za Sekondari za Serikali za Kata.


Malipo kwa kufanya vizuri (COD) ni utaratibu mpya kutoa msaada ambapo wafadhili hutoa pesa kwenye maendeleo yanayopimika kwa kuangalia matokeo maalum. Unahusianisha moja kwa moja malipo na matokeo maalum, ikiwapatia watendaji/wapokeaji motisha ya kuongeza nguvu zao za kufanyakazi ili kufikia maendeleo.

Msingi na uhalali wa wazo la CDO, ulioanzishwa awali na Kituo cha Maendeleo ya Kimataifa(Center for Global Development) mjini Washington, umejikita kwenye mtazamo kwamba kazi za maendeleo ni lazima zitathminiwe kwenye athari (impact) zinazoletwa. Mbinu inawakilisha mabadiliko kutoka kufuatilia nguvu na rasilimali ambavyo mashirika huwekeza katika kutoa misaada - 'nyenzo/rasilimali', na pia shughuli na vifaa/vitendeakazi vinavyotokana na uwekezaji huo - 'matokeo'. Badala yake, mbinu hii inalenga kujikita kuangalia namna gani maisha ya watu masikini yameweza kubadilishwa kutokana na uwekezaji kwenye sekta au eneo fulani la maendeleo (afya, elimu, n.k).

Mnamo mwezi Septemba 2011, Shirika la Maendeleo Bumbuli lilifanya utafiti wa kina juu ya mazingira ya kujifunzia Bumbuli na kugundua kwamba shule nyingi, walimu, na wanafunzi wa Bumbuli hawana motisha wala rasilimali zinazohitajika kuwawezesha wafanye vizuri kama inavyotarajiwa.

Kwa wastani, kila shule iliyotoa data za matumizi ya pesa ilionyesha ni Sh. 5,268 kwa kila mwanafunzi kwa mwaka 2010 (kiasi kilichotarajiwa kwa shule za Sekondari ni shilingi 25,000 kwa kila mwanafunzi). Pamoja na hayo, utafiti ulionyesha kuwa ni 71% tu ya walimu walikuwepo shuleni, ambapo ni 19% tu walikutwa madarasani. Utafiti huo ulionesha kuwa walimu hupata mishahara yao kwa wakati. Wastani wa mshahara halisi wa mwalimu wa Bumbuli ni Sh.395,000 kutoa malipo ya deni ya Sh.74,000 kila mwezi. Wengi walionesha kuwa na shughuli ya ziada ya kiuchumi (67%), hasa kilimo (90%). Wengi wao (98%) walidai kutokuhusishwa katika hatua za kupanga bajeti za shule. Wastani wa Pato la Mtanzania anayeishi kijijini (ikiwemo Bumbuli) ni Sh.152,000 (HBS, 2010). Wakati 89% ya wanafunzi wanaonesha kushiriki katika shughuli za kiuchumi wa familia, bado 70% wanafanikiwa kupata muda kidogo wa kukamilisha kazi zao za masomo wakiwa nyumbani, huku 34% inaonesha hawakufika shule kwa mwezi uliopita kutokana na kusaidia shughuli za nyumbani. Matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne ya mwaka 2011 kwa Shule za Bumbuli yalikuwa mabaya sana. Kati ya wanafunzi 1,327 waliofanya mtihani, hakuna aliyepata Division 1, waliopata Division 2 ni wanne, waliopata Division 3 ni 39, na waliobakia, yaani wanafunzi 1,274, walipata Division 4 na 0.

Pamoja na hatua mahsusi ambazo Serikali inachukua kuboresha elimu nchini na kuongeza ufaulu, Shirika la Maendeleo Bumbuli, kupitia Program hii ya COD, linataka kuonesha kwamba fedha zinaweza kugawika vizuri na kwa usahihi ili kuboresha elimu kwa kupima kiwango cha ufaulu wa wanafunzi.

Hatua na mikakati inayopendekezwa

Program ya COD kwa Shule za Sekondari Bumbuli itahusisha makubaliano kati ya Shirika la Maendeleo Bumbuli, Shule za Sekondari Bumbuli na Halmashauri ya Wilaya kulipa jumla ya kiasi cha Dola za kimarekeni 100 kwa kila mwanafunzi anayefaulu mitihani ya kidato cha IV kwa daraja la I-III. Malipo ya COD yatafanyika baada ya uthibitisho wa matokeo ya mtihani wa kidato cha nne. Fedha zitapelekwa Halmashauri ya Wilaya, Shule za Sekondari na kwa walimu na wanafunzi. Fedha zitakazogawiwa kwa shule zitatumika kwa ajili ya mahitaji ya kielimu ya shule kama zilivyowekewa vipaumbele na Bodi za Shule.


Watakaonufaika na mradi:

Kwa kila mwanafunzi atakayefaulu mtihani (Div I-III) anapomaliza kidato cha nne, Shirika la Maendeleo Bumbuli kupitia program ya COD litatoa malipo yafuatayo:

1. Walimu: Tsh 60,040/= kwa kila mwanafunzi anayefaulu mtihani
2. Wanafunzi: Tsh 50,500/=Kwa kila mwanafunzi anayefaulu mtihani
3. Shule: Tsh 31,600/= Kwa kila mwanafunzi anayefaulu mtihani
4. Halmashauri ya Wilaya: Tsh 15,800/= kwa kila mwanafunzi anayefaulu mtihani


Vipimo na Ukaguzi:


Data za mitihani kuanzia mwaka 2011 zitatoa msingi wa awali, na msingi huo utakuwa ukibadilishwa kila mwaka na ufanisi wa utendaji wa shule, hivyo kila mwaka unakuwa msingi kwa ajili ya malipo ya mwaka ujao wa. Kiashiria cha matokeo kitakuwa idadi ya wanafunzi ambao wamefaulu kidato cha nne kwa kupata daraja la I-III. Ili kuyadumisha matokeo hayo, hatua mbalimbali zitakuwa vikiripotiwa kila mwaka na shule na halmashauri. Mkataba, matokeo, na taarifa nyingine zitawekwa wazi kwa wananchi ili kuongeza uwajibikaji wa wafadhili na wapokeaji

Shirika la Maendeleo Bumbuli halina nia ya kusema kwamba COD ndio suluhisho pekee la tatizo la maendeleo ya elimu au ufumbuzi wa matatizo yote katika mfumo wa elimu nchini lakini tunaamini inaonesha matarajio ya kutosha kuona thamani ya kujaribu, kujifunza na kutathmini.


Uendelevu wa program

Ili program iwe endelevu, Shirika la Maendeleo Bumbuli(BDC) litaweka mfumo thabiti wa kufanya tathimini na kutoa mrejesho, ambao utatumika kama zana ya kupimia uwajibikaji, na kuendeleza uwazi. Pia ni muhimu kuzingatia ushirikishwaji wa wenyeji wa Bumbuli na umiliki wa program ya COD. Hili linaweza kufanikiwa kwa kuanzisha kampeni ya kuhamasisha elimu bora kama uwekezaji wa wenyeji, na Mtandao wa Wahitimu wa Shule za Sekondari Bumbuli kwa ajili ya fedha za COD. Zaidi sana, Shirika la Maendeleo Bumbuli litahusisha na kutumia Bodi za Shule, ambazo zinahusisha wazazi na walimu. Hii ndiyo njia itakayowafanya watu wa Bumbuli wathamini juhudi zao wenyewe katika kuboresha jamii zao.

5. Kambi ya Wanafunzi Wanaojiandaa na Mtihani wa Kidato cha Nne 2012

Kuanzia tarehe 4 Agosti hadi 5 Septemba, wakati wa likizo za masomo, Shirika limeandaa kambi maalum kwa matayarisho ya vijana wanaojiandaa na mtihani wa Kidato cha Nne mwaka huu. Kambi hii itakuwepo kwenye Kituo cha Elimu Soni, ambacho kina mandhari, mazingira na eneo la kutosha kufundishia na kuishi wanafunzi katika kipindi hiki.

Kila siku, wanafunzi hao watapigwa msasa kwa masomo ambayo hawakupata fursa ya kuyasoma vizuri katika mwaka wa shule, watafundishwa mbinu za kufanya mitihani (ikiwemo time-management), na kufanya revision ya mitihani ya Kidato cha Nne ya kuanzia mwaka 1984 hadi sasa. Shirika litatafuta walimu wenye sifa za kufundisha masomo ya Hesabu, Kiingereza, Historia, Kemia, Fizikia na Biolojia, hata nje ya Jimboni na kuwalipa posho kuja kufundisha kwenye kambi. Pia tutaomba watu mbalimbali, ikiwemo walimu wastaafu, wenye moyo wa kujitolea waje kufundisha kambi hii.

Mwisho

Hadi sasa Shirika la Maendeleo Bumbuli halijapata mfadhili au ufadhili kutoka kokote au kwa mtu yoyote. Miradi hii niliyoitaja ndio iko katika hatua za kupata ufadhili. Fedha ambazo zimetumika hadi sasa kuanzisha Shirika, kuweka ofisi, kuajiri watumishi wa muda na kufanya utafiti na kutengeneza maandiko ya miradi zimetokana na mkopo niliouchukua kama Mbunge, ikiwemo mkopo wa gari ambao sikuutumia kununua gari bali kuanzisha Shirika.

Napenda kutoa mwito kwa wana-Bumbuli wenzangu na Watanzania kwa ujumla kusaidia kuchangia maendeleo ya Jimbo la Bumbuli, hasa kwa miradi ambayo hatukuitafutia ufadhili kama huu wa COD na kambi. Kwa kuchangia unaweza kutumia namba ya M-PESA 0762088050. Kwa maelezo zaidi kuhusu Shirika la Maendeleo Bumbuli, tuma barua pepe: getinvolved@bumbuli.org au piga simu: +255 22 2129821/6 au tuma fax: +255 22 2129796

Katika miezi ijayo, BDC pia itatekeleza miradi ya kitaifa yenye manufaa kwa maendeleo na utawala bora kwa nchi yetu. Naamini nchi yetu itapiga hatua za maendeleo kwa kasi zaidi kama kila mmoja wetu, kwa nafasi na uwezo wake, atathubutu, lakini pia kama sote tutasaidiana katika kuchangiana na kupeana mawazo kuhusu shughuli za maendeleo.

January Makamba
Mbunge Bumbuli
8 Julai 2012

Popular Posts