Pages

Showing posts with label Balozi na Ofisi za Balozi. Show all posts
Showing posts with label Balozi na Ofisi za Balozi. Show all posts

Wednesday, October 17, 2012

Emergency Message For U.S. Citizens Issued By The U.S. Embassy In Dar Es Salaam


Unrest in Stone Town (Zanzibar) and Dar es Salaam Today Wednesday, October 17, 2012October 17, 2012
U.S. Embassy Dar es Salaam
Stone Town: The U.S. Embassy alerts U.S. citizens that Tanzanian authorities and local media report demonstrations, roadblocks, tire burning, rock throwing, and rioting in the Darajani, Mbuyuni, and Kisonge districts of Stone Town, Zanzibar this afternoon. Demonstrators are upset due to the apparent disappearance of a Muslim cleric in Stone Town.
Dar es Salaam: Police report a crowd is gathering at Police Headquarters on Ohio Street in central Dar es Salaam, demanding the release of a radical cleric who was arrested with 38 other Muslim clerics this morning. There is also a report of unrest in Mbagala, south of Dar es Salaam
These are fluid situations that may change rapidly. Avoid these areas until the situation has returned to normal and continue to monitor local media for updates.
Click this link for a map of the Stone Town area.
Click this link for a map of downtown Dar es Salaam.
We encourage U.S. citizens to enroll in the Smart Traveler Enrollment Program (STEP) for the most up-to-date safety and security information. Keep all of your information in STEP up-to-date by maintaining your current phone numbers and email addresses where you can be reached in case of an emergency.
You can stay in touch and get updates by checking the U.S. Embassy Dar es Salaam website. You can also get global updates at the U.S. Department of State’s Bureau of Consular Affairs website, where you can find the current Worldwide Caution, Travel Warnings, Travel Alerts, and Country Specific Information. Follow us on Twitter and the Bureau of Consular Affairs page on Facebook as well, or you can download our free Smart Traveler iPhone App for travel information at your fingertips.
Current information on safety and security can also be obtained by calling 1-888-407-4747 toll-free in the United States or a regular toll line at 1-202-501-4444 for callers from other countries. These numbers are available from 8:00 a.m. to 8:00 p.m. Eastern Time, Monday through Friday (except U.S. federal holidays).
U.S. Embassy in Dar es Salaam, Tanzania
686 Old Bagamoyo Road, Msasani
Tel: [255] (22) 229-4000; Fax: [255] (22) 229-4721
Email: drsacs@state.govhttp://tanzania.usembassy.gov
After hours U.S. citizen emergencies: call +255-(0)22-229-4000
and wait for the operator to answer.

Thursday, August 16, 2012

U.S Peace Corps Tanzania, sworn-in

Picture
The United States of America Peace Corps Education Volunteers taking oath of service before the US Ambassador to Tanzania, Alfonso Lenhardt at the ambassador's residence in Dar es Salaam yesterday. (PHOTO: JOHN BADI)
Picture
On August 15, U.S. Ambassador Alfonso E. Lenhardt hosted a swearing-in ceremony for 47 Peace Corps Volunteers at his residence. Pictured are U.S. Ambassador Alfonso E. Lenhardt (6th from right), Peace Corps Director Dr. Elizabeth O'Malley (8th from right) and George Yambesi, Permanent Secretary of the President's Office of Public Service Management, and 47 newly sworn-in Peace Corps Volunteers who will work in the education field throughout Tanzania. (PHOTO COURTERSY OF THE U.S EMBASSY in Dar es Salaam, Tanzania)

Tuesday, August 14, 2012

RAIS WA ZANZIBAR DK ALI SHEIN AFANYA MAZUNGUMZA NA MABALOZI WA KOREA NA DENMARK IKULU YA ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK. Ali Mohamed Shein, akifuatana na Balozi wa Korea nchini Tanzania, Kim Young Hoon, alipofika kumuaga Rais, Ikulu mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK. Ali Mohamed Shein, akifuatana na Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Johnny Flento,alipofika Ikulu Mjini Zanzibar jana, baada ya mazungumzo yao.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK. Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Johnny Flento, alipofika Ikulu mjini Zanzibar jana, kwa mazungumzo na Rais
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Johnny Flento, alipofika Ikulu mjini Zanzibar jana, kwa mazungumzo na Rais
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Balozi wa Korea Nchini Tanzania, Kim Young Hoon,alipofika kumuaga Rais,katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar jana
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi DK. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Balozi wa Korea nchini Tanzania, Kim Young Hoon, alipofika kumuaga Rais, Ikulu mjini Zanzibar jana.Picha na Ramadhan Othman, Ikulu-Zanzibar

Balozi wa Marekani nchini Tanzania amtembelea makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akiitikia dua baada ya kushiriki futari iliyoandaliwa na Masjid Iman iliyoko Mbweni Zanzibar.Katikati ni Sheikh Habib Ali Kombo.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akifurahi pamoja na Balozi wa Marekani nchini Tanzania Alfonso Lenhardt, aliyefika nyumbani kwake Mbweni kwa ajili ya kubadilishana mawazo. Picha na Salmin Said-Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar
---
Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Alfonso Lenhardt ameahidi nchi yake itaunga mkono juhudi za Zanzibar kuwa na mipango madhubuti ya uokoaji wakati yanapotokea majanga, ili kunusuru maisha ya watu pale inapotokea hali kama hiyo.

Amesema msaada wa Marekani utaelekezwa zaidi kuiwezesha Zanzibar kuwa na mfumo wa kisasa wa mawasiliano utakaosaidia kujua eneo la tukio na kumudu kufika kwa haraka, kwa nia ya kuokoa maisha ya watu wengi zaidi iwezekanavyo.

Balozi Alfonso amesema hayo leo alipokuwa na mazungumzo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad huko nyumbani kwake Mbweni, nje kidogo ya mji wa Zanzibar kuzungumzia tukio la kuzama kwa meli ya MV. Skagit, pamoja na mambo mengine mbali mbali. “Msaada huu wa kuepusha maafa wakati yanapotokea majanga, utakuwa ni kwa Tanzania nzima, lakini tutahakikisha Zanzibar inanufaika nao na inajijengea uwezo wa kuokoa maisha ya watu wake, wakati wa maafa kama haya ya kuzama kwa meli na mengineyo”, aliahidi Balozi Lenhardt.

Hata hivyo, Balozi huyo wa Marekani alisifu mshikamano wa wananchi wa Zanzibar pamoja na serikali yao, wakati wa maafa ya kuzama kwa MV. Skagit mwezi uliopita, hali ambayo ilisaidia kuokolewa baadhi ya watu waliokuwemo kwenye meli hiyo.

Naye, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad amekaribia azma hiyo ya Marekani kuisaidia Zanzibar katika kukabiliana na majanga mara tu yanapotokea. Katika hatua nyengine Balozi Lenhardt ameisifu Zanzibar kwa hatua kubwa iliyoweza kufikia kudhibiti ugonjwa wa Malaria ambao umekuwa ukisababisha vifo vya watu wengi wakiwemo watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.

Balozi huyo amesema Zanzibar imejijengea heshima na hivi sasa imekuwa mfano Duniani na wataalamu kutoka sehemu mbali mbali wanakuja Zanzibar kujifunza mbinu za kutokomeza ugonjwa huo. Akizungumiza mafanikio hayo, Maalim Seif alisema suala la elimu kwa wananchi juu ya kutokomeza ugonjwa huo limechangia kwa kiasi kikubwa kuwa na uelewa wa hali ya juu kujilinda wasipate maradhi hayo.

Maalim Seif alisema baada ya wananchi walio wengi kuelewa mbinu za kujikinga na Malaria imekuwa rahisi kuweza kuzitumia njia wanazoshauriwa na wataalamu.

Alizitaja baadhi ya mbinu hizo kuwa ni matumizi ya vyandarua, kupuliziwa dawa kwenye nyumba zao, kuweka mazingira yao katika hali ya usafi pamoja na kufika kwenye vituo vya afya kwa uchunguzi na kutibiwa mara wanapoona dalili za kuwa na maradhi hayo.

Balozi huyo wa Marekani pia amemhakikishia Makamu wa Kwanza wa Rais kuwa nchi hiyo itaendelea kufanikisha miradi mbali mbali inayofadhiliwa na Marekani hapa Zanzibar.

Miongoni mwa miradi hiyo ni utandikaji wa laini kuu ya umeme kutoka Dar es Salaam hadi Fumba kupitia chini ya bahari na ujenzi wa barabara tafauti, ambayo yote ipo katika hatua nzuri za utekelezaji.

Wakati huo huo Makamu wa Kwanza wa Rais jana alijumuika katika futari iliyoandaliwa na masjid Iman iliyoko mbweni, nje kidogo ya mji wa Zanzibar.

Futari hiyo iliwajumuisha wananchi mbali mbali wanaosali katika msikiti huo pamoja na viongozi kadhaa wa dini na siasa wakiwemo Sheikh Habib Ali Kombo na Makamu Mwenyekiti wa CUF Machano Khamis Ali.
Na
Hassan Hamad
Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar

Wednesday, July 18, 2012

UBALOZI WA AFRIKA KUSINI WAADHIMISHA MIAKA 94 YA NELSON MANDELA KWA KUIKARABATI SHULE YA MSINGI TANDALE.

Masoud Ramadhani wa Ubalozi wa Afrika Kusini akiosha moja ya Vyoo vya shule hiyo.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na Wafanyakazi wa Ubalozi wa Afrika Kusini nchini wakiwa wamekusanyika katika shule ya Msingi Tandale jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanyakazi za kujitolea kwa dakika 67 ikiwa ni maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe 18 mwezi Julai.
Balozi wa Uganda nchini Tanzania Mh. Ibrahim Mukiibi akiwasili kushiriki zoezi hilo.
Mabalozi wa Afrika Kusini Mh. Henry Chiliza (kushoto) na Mh. Ibrahim Mukiibi wa Uganda wanaoziwakilisha nchi zao hapa Tanzania wakisalimiana baada ya kukutana katika zoezi la kujitolea kufanya kazi za kijamii katika shule ya msingi Tandale ya jijini Dar es Salaam. Kulia ni Joymrey Von de Merwe.
Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini (UNIC) Bi. Stella Vuzo akitoa mwongozo wa namna ya kutekeleza zoezi hilo ambalo limeonyesha mafanikio makubwa baada ya kuweza kukarabati madawati yalioharibika, kupiga rangi Ubao za kuandikia madarasani na kufanya usafi katika mazingira ya shule hiyo.

Bi. Stella Vuzo amesema katika kuadhimisha siku kama hii mwaka jana Umoja wa Mataifa ulitoa huduma za Kibinadamu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa watoto wanaosumbuliwa na ugonjwa wa Saratani na mwaka huu wameonelea ni vyema kuungana na wanafunzi wa shule ya msingi Tandale kwa kuonyesha wanajali na kutoa huduma kama hizo katika shule hiyo chini ya kauli mbiu ya mzee Nelson Mandela "Inspire Change Within Your Self".

Wafanyakazi wa UN na Ubalozi wa Afrika Kusini wakishirikiana kubeba madawati kwa ajili ya kufanyiwa ukarabati.
Pichani Juu na Chini ni Mwenyekiti wa Kamati ya Shule ya Msingi Tandale jijini Dar Hamisi Kubiga (kushoto) sambamba na Balozi wa Afrika Kusini nchini Tanzania Mh. Henry Chiliza wakihakikisha ukarabati wa madawati unakwenda sawa.
Balozi wa Uganda nchini Mh. Ibrahim Mukiibi akifanya usafi katika moja ya madarasa ya Shule hiyo.
Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini (UNIC) Bi. Stella Vuzo akitumia muda wake wa dakika 67 kusafisha maeneo ya shule ya msingi Tandale ya jijini Dar.
Mfanyakazi wa Ubalozi wa Afrika Kusini nchini Masoud Ramadhani (kushoto) akichanganya dawa kwa ajili ya kusafisha vyoo vya shule ya msingi Tandale katika kuadhimisha siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela.
Wanafunzi na wafanyakazi wa UN na Ubalozi wa Afrika Kusini wakisaidiana kuzoa taka kuhakikisha shule ya msingi Tandale inakuwa safi.
Wanafunzi wakionyesha ushirikiano katika kuadhimisha Nelson Mandela International Day.
Pichani Juu na Chini Wafanyakazi wa UN na Ubalozi wa Afrika Kusini wakipiga rangi Ubao wa Kufundishia katika shule ya msingi Tandale jijini Dar es Salaam.
Afisa Mawasiliano wa UNICEF Jacquiline Namfua (kushoto) na wafanyakazi wenzake wakishiriki kupiga rangi katika moja ya ubao wa shule hiyo kuhakikisha wanafunzi wanapata mahali sahihi pakufundishiwa.
Mmoja wa watu aliyejitolea Kapteni wa Ndege Bw. Andre Van Devententer akishirikiana na wanafunzi wa shule ya msingi Tandale kukarabati madawati mabovu katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela leo.
Afisa Habari wa Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini (UNIC) Bi. Stella Vuzo akiwa katika moja ya darasa na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo ambao mpaka leo wana uhaba wa madawati hivyo kulazimika kukaa chini wakati wa kusoma.
Wanafunzi wa shule ya msingi Tandale wakibanana katika dawati moja mithili ya abiria ndani ya Dalala huku tukitegemea kuboreka kwa kiwango cha elimu nchini.
Balozi wa Afrika Kusini nchini Mh. Henry Chiliza akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo katika shule ya Msingi ya Tandale ambapo amesisitiza siku hii ya Kimataifa ya Mandela inaadhimishwa kwa kufanya shughuli za kijamii kwa kuwa Mzee Mandela mwenyewe alikuwa akijitolea muda wake mwingi kusaidia watoto, kufanya shughuli za kijamii, kutetea haki za watoto na wanyonge.
Pichani Juu na Chini Balozi wa Afrika Kusini nchini Mh. Henry Chiliza akikabidhi msaada wa uliotolewa na UN kwa Mwalimu Mkuu msaidizi wa shule hiyo Lucy Mwakibete huku wakishuhudiwa na wafanyakazi wa UN, Ubalozi, Walimu na wanafunzi.
Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Tandale Bi. Lucy Mwakibete (katikati) akitoa shukrani kwa UN na Ubalozi wa Afrika Kusini nchini ambapo ameelezea changamoto mbalimbali zinazoikabili shule zikiwemo Uhaba wa Madawati, Vyoo, Ubovu wa Sakafu za Vyumba vya Madarasa na kuwaomba wadau kujitokeza kuwasaidia ili kuboresha mazingira mazuri kwa wanafunzi wa shule hiyo ili kuongeza kiwango cha ufaulu.
Kutoka kushoto ni Kansela wa Masuala ya Siasa Bw. Terry Govender na Joymery Von De Merwe kutoka Ubalozi wa Afrika Kusini wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Tandale Bi. Lucy Mwakibete.

Tuesday, June 12, 2012

MABALOZI WAPYA WAAPISHWA

Rais Jakaya Kikwete akimwapisha Balozi Bertha Semu Somi Ikulu Jijini Dar es Salaam
Rais Jakaya Kikwete Akimwapisha Balozi Dora Mmari Msechu Ikulu jijini Dar es Salaam
Rais Jakaya Kikwete akimwapisha Balozi Naimi Sweetie Hamza Aziz ikulu jijini Dar es Salaam
Rais jakaya kikwete akimwapisha Balozi Dora Mmari Msechu Ikulu Jijini Dar es Salaam
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete Jana amewaapisha mabalozi wapya kumi ambao wataongoza idara na kurugenzi mbalimbali katika Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Pichani Rais akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wapya aliowaapisha ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.Kutoka kushoto walisimama mstari wa mbele ni Balozi Bertha Semu Somi,Balozi Hassan Simba Yahya, Balozi Vincent Joel Thomas Kibwana,Balozi Naimi Sweetie Hamza Aziz,Balozi Irene Mkwawa Kasyanju na Balozi Dora Mmari Msechu.Waliosimama nyuma kutoka kushoto ni Balozi Silima Kombo Haji,Balozi Celestine Joseph Mushy, Balozi Mbelwa Brighton Kairuki na Balozi Ramadhan Muombwa Haji.Picha na Freddy Maro-IKULU

Popular Posts