Pages

Saturday, August 18, 2012

MUHTASARI WA MKUTANO WA WADAU WA FILAMU TANZANIA ULIOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA LEADERS – KINONDONI MJINI DAR ES SALAAM

MUHTASARI WA MKUTANO WA WADAU WA FILAMU TANZANIA ULIOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA LEADERS – KINONDONI MJINI DAR ES SALAAM

15 AGOSTI 2012.

Utangulizi.
Mheshimiwa Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Viongozi wa Vyama Wanachama wa Shirikisho la Filamu na Wadau wa Filamu nchini.

Napenda kuchukua fursa hii kwa kuwashukuru wote wale wote waliopata bahati ya kuhudhuria katika mkutano ule ambao kwetu ni mkutano wa kihistoria.

Sababu ya Kuwepo kwa Mkutano.

Mnamo siku ya tarehe 7 Agost 2012 majira ya saa 11 jioni Shirikisho la Filamu Tanzania , TAFF kwa ushirikiano wa pamoja na kampuni ya Usambazaji ya Steps Entertaiment, Watayarishaji wa Filamu wa kampuni za Jerusalem Production, Nice Entertainment , Chen Arts Creation , Nyerere the Power, CYG na Wasanii Waongozaji kwa Ushirikiano wa Jeshi la Polisi na ofisi za TRA Makao makuu. Tulifanikiwa kumkamata mtu ambaye inasadikiwa anadurufu kazi mbalimbali za Wasanii wa Filamu na muziki wa taarabu na injili.

Mfanyabiashara huyo haramu wa kazi Wasanii nchini Bwana Rigobert Masawe alikamatwa kwa kushirikiana na raia mwema ambao hawakuridhikia na faida anayopata kutokana na kufanya biashara haramu inayotokana na jasho la Wasanii.

Baada ya kufanikiwa kumkamata Mtuhumiwa huyo na kufikishwa katika vyombo vya sheria. Shirikisho la Filamu – TAFF, iliitisha kikao cha dharura kwa Wasambazaji na Watayarishaji wa Filamu wote ili kwa pamoja kutafuta namna ya kulishughulikia jambo hili kwa haraka na kwa nguvu za Pamoja.

Katika kikao hicho kilichofanyika 08/08/2012 ambacho kilikuwa cha Mafanikio Watayarishaji na Wasambazaji wengi walihudhuria, baada ya majadiliano ya kina na yenye busara ambayo yalionesha ushirikiano mkubwa katika kutetea hali hii, Wajumbe walichangia mawazo mbalimbali na maazimio yalikuwa yafuatayo:

  1. Tufanye Mkutano na Waandishi wa Habari ili kuijulisha jamii na umma wa Watanzania kwamba jambo limezidi kuwa sugu na lisili la kificho na linafanyika wazi Bila ya woga.
  2. Kufanya matembezi ya kulaani kushamiri kwa wizi wa kazi za Sanaa Dhahiri
  3. Ili kuonesha kukerwa huko Wasanii na Wadau waliazimia kwamba kila mmoja awe askari kanzu kwa jambo hili kwa makusudi bila ya hivyo filamu zitakosa mauzo kama ilivyo kwa muziki hapa Tanzania kwa sasa.

Wajumbe pia walikubaliana kwamba mambo yote yafanywe chini ya mwavuli wa TAFF kwa sababu ndio muhimili wao.

Baada ya maazimio hayo iliundwa kamati ya kusimamia na kupanga mkakati wa namna ya kutekeleza mkubaliano hayo, kamati hiyo ilikuwa na Wajumbe wafuatao;

  1. Simoni Mwakifwamba Rais wa TAFF.
  2. Wilson Makubi Katibu Mtendaji wa TAFF.
  3. Steven Mengele (Nyerere)
  4. Simoni Mwapagata (Rado)
  5. Jackob Steven (J.B)
  6. Vincent Gibs (Gibs Media)
  7. Vincent Kigosi ( Ray)
  8. Issa Mussa (Cloud)
  9. Mahsein Awadhi (Dr Chen)
  10. Asha Baraka

Kamati ilikuwa na jukumu la kutafuta namna ya kufanikisha maazimio hayo na Kampuni za Usambazaji na Watayarishaji zilikuwa tayari kusaidia baadhi ya maeneo katika utekelezaji.

Mkutano na Waandishi

Mheshimiwa Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo tarehe 10/08/2012 saa 5 mchana asubuhi kamati ilifanikisha kutekeleza jukumu la kuongea na waandishi wa habari kama maazimio yalivyopendekezwa. Mkutano ulifanyika katika Hotel ya Demagi Kinondoni ulikuwa na mafanikio makubwa kwa sababu wadau mbalimbali walihudhuria pamoja na Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotions Mh. Alex Msama aliweza kufika na aliipongeza TAFF kwa jitihada za makusudi iliyochukua kuokoa hali ambayo inatishia uhai wa kazi za Wasanii wa Filamu nchini kama ilivyo katika Muziki

Wazungumzaji wakuu katika mktano huo na Waandishi wa habari walikuwa ni Rais wa Shirikisho la Filamu na Mwenyekiti wa kundi la Bongo Movies.

Baada ya Mkutano na Waandshi wa Habari TAFF ilifanya kikao na Wasambazaji wote pamoja na kupitia chama cha Wasambazaji nchini TAFDA na ile kamati ya awali pamoja kutafakari kwa pamoja juu ya matembezi ya kulaani wizi wa kazi za wasanii kikao kilifanyika katika ofisi za TAFF zilizopo Magomeni.

Lakini pamoja na Wajumbe wa kikao cha kwanza kupitisha maazimio ya kufanya matembezi ya kulaani wizi bado Uongozi wa TAFF uliona kwamba hakuna ulazima sana wa kufanya Matembezi hayo kwa kuwa Serikali tayari imeonesha nia ya kusaidia tasnia hii na uzuri ni kwamba utekelezaji wake umeshaanza kupitia mpango wake wa urasimishaji Wajumbe wote walikubaliana na hoja hiyo.

Kutokana na hilo Shirikisho la Filamu ikaamua kusitisha suala la Matembezi badala yake likafanya mkutano wa Kulaani wizi wa kazi sanaa katika viwanja vya Leaders kwa makusudio na malengo yale yale yaliyoamuliwa katika kikao na Wanakamati. Wasambazaji waliohudhuria ni Steps Entertainment, PiliPili Entertainment, Whatever Production, Liro Promotion, Zito Entertainment, SSG Distribution, KAPICO, GMC, Papa Zii, Bajomba Production, Sas O entertainment, KIBIKI, Easy Media, Bornagain Film Production,Mega Video na Wengineo wengi.

Kwa kuona umuhimu wa hilo Wasamabazaji walipitisha azimio la kuchangia ili kufanikisha mkutano huo na jumla ya Tshs 1,300,000/= ziliahidiwa na kufanikisha mkutano huo.

Mkutano wa Kulaani Wizi wa Kazi za Sanaa
Mheshimiwa Waziri,
Napenda kukujulisha kwamba miezi miwili iliyopita kabla ya tukio hili kutokea Wadau mbalimbali wa tasnia ya Filamu na Muziki wameipongeza TAFF kwa muenendo wake mzuri katika kusimamia majukumu yake pamoja na mapungufu makubwa yaliyopo ikiwemo suala la tatizo la kifedha, lakini hawakusita kutushauri juu ya mgogoro wa kifikra uliopo kati ya TAFF na kundi la wasanii wa Bongo Movie, wengi walishauri kwamba ipo haja ya kufikia tamati kwa tatizo lenu sababu nafasi tuliyonayo kwa jamii ni kubwa sana. TAFF iliupokea ushauri huo ilikuwa inaufanyia kazi.

Mkutano wa Wadau Kulaani Wizi huo, ulifanyika tarehe 15 Agost 2012 kuanzia saa 6 mchana na kiukweli ni mkutano wa mafanikio kwa sababu pamoja na muda wa mkutano ulikuwa wa jua kali lakini wadau walijitokeza wengi sana.

Mada zilizozungumzwa katika mkutano huo ukiondoa mada kuu ya Kulaani Wizi wa kazi za Sanaa ni zifuatazo:
a. Nafasi ya Wadau wa Filamu katika Urasimishaji wa sanaa nchini
b. Umuhimu wa Bima ya Afya kwa Wasanii
c. Umuhimu wa Wasanii katika mchakato mpya wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano.
d. Umoja na Maadili ya Wasanii na katika kazi zetu.

Wazungumzaji katika Mkutano huo Walikuwa ni
a. Rais wa Shirikisho
b. Mwenyekiti wa kundi la Bongo Movie

Mratibu Mkuu wa Mkutano huo walikuwa ni TAFF chini ya Usimamizi wa Katibu Mtendaji. Mkutano ulifunguliwa saa 6:00 na Mkurugenzi wa kampuni ya Papa Zi kwa kuwashukuru wadu wote wliohudhuria hapo pamoja na hali ya jua kuwa kali. Lakini pia aliwaomba wadau kwamba Jambo linalohusu umoja miongoni mwetu ni la muhimu sana kuliko wanavyofikiria kwa sababu bila ya kuwa na umoja mambo mengi hayatafanikiwa.

Mwenyekiti wa Bongo Movie

Mwenyekiti wa Kundi la Wasanii wa Bongo Movie Jackob Steven (J.B) alisema kwamba sasa ni wakati wa Wasanii kuamka , kujitambua na kuacha tofauti zetu ambazo kimsingi hazitusaidii kupiga hatua bali ni wakati wa kuungana ili kwa pamoja tuweze kumpiga adui yetu kwa nguvu ya pamoja.

Lakini pia aliupongeza uongozi wa TAFF kwa jitihada mbalimbali wanazofanya katika kushughulikia matatizo ya Wasanii, kuwatetea wasanii na mambo muhimu wanayopigania kwa niaba ya Wasanii wote hapa nchini.

J.B aliendelea kusema kuwa Wasanii tusipoonesha ushirikiano na mshikamano wa kweli maharamia wa kazi za filamu wataendelea kunufaika huku wenye haki tukiwa palepale kwa sababu za kuendekeza matatizo yasiyo na tija kwetu. Lakini pia alimuomba Rais wa Shirikisho la Filamu na Uongozi kwa ujumla walitazame suala la mgogoro wetu kwa sababu unachangia kutumaliza wenyewe na aliomba wakati umefika bifu hilo limalizike haraka iwezekanavyo kwa maslahi ya tasnia ya filamu na sanaa kwa ujumla na anamini kwamba hakuna atayeweza kutusuluhisha ikiwa sisi wenyewe hatuko tayari, wao kama Bongo Movie wana tamka wazi kwamba hawana tatizo na Uongozi wa Shirikisho na wanamtambua Rais wa Shirikisho na wako tayari kufanya kazi pamoja .

Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania

Mheshimiwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kabla ya kuanza kuzungumzia ajenda kuhusu Mkutano huo aliwashukuru wadau wote waliohudhuria kwa sababu anaamini wametambua wajibu na ummuhimu wa Shirikisho la Filamu Tanzania.

Lakini pia alichukua fursa hiyo kujibu maelezo yaliyotolewa na J.B kuhusu mgogoro wa Bongo Movie dhidi ya TAFF, Kabla ya yote alimuomba Mwenyekiti wa Bongo Movie na viongozi wengine na Katibu wa Shirikisho na viongozi wengine wapande juu ya jukwaa.

Alisema kwamba anajisikia furaha na amani bila ya kutarajia kama J.B angetoa taarifa hiyo mbele ya umma wa Wadau wa Filamu Tanzania siku hiyo, lakini kwa niaba ya Kamati Kuu ya Shirikisho, Bodi ya Shirikisho la Filamu na Wanachama wote wa Shirikisho la Filamu Tanzania, alitamka wazi kwamba ikiwa Rais wa Shirikisho au Bodi ya Shirikisho na Wanachama waliwakosea Bongo Movie basi kwa niaba ya wote anaomba tusamehewe lakini pia alisema na ikiwa Bongo Movie waliwakosea TAFF pia kwa niaba ya uongozi mzima wa Shirikisho anatamka wazi kwamba tumewasamehe hivyo anaomba tuzike na kusahau tofauti zetu leo na tuanze upya.

Baada ya maelezo hayo ambayo yaliungwa mkono kwa wadau kupiga makofi kwa wingi sana Rais wa TAFF, Simoni Mwakifwamba alimkaribisha J.B naye alisema kwamba kwa niaba ya Uongozi wote wa Bongo Movie nao wamekubali msamaha uliotolewa na wao wamewasamehe wale wote walio wakosea katika mchakato wa mgogoro huo na ameomba tuanze upya mahusiano yetu kama ilivyo kuwa zamani wakati tunaanzisha TAFF na wako tayari kushirikiana na TAFF kwa lolote wataloagizwa kufanya na kuanzia leo wanamtambua Rais wa TAFF na uongozi wote kwa ujumla.

a. Nafasi ya Wasanii wa Filamu katika Urasimishaji wa sekta ya Sanaa

Rais wa TAFF alianza kwa kuishukuru serikali kwa kuweza kusikiliza kilio chetu ambacho kimedumu zaidi ya miaka 20 sasa, lakini pia aliishukuru serikali kwa kuifanya sanaa kuwa ni kazi rasmi ambayo itakuwa ni yenye mchango katika pato la Serikali moja kwa moja. Kwa hiyo aliwataka Wasanii wa filamu kuakikisha kuwa wanaitumia fursa ya urasimishaji huo kwa mambo yafuatayo:

i. Kuzalisha kazi bora zenye zitazokidhi viwango vya soko la ndani na soko la kimataifa na zenye maadili ii. Kuhakikisha kwamba kazi zote lazima ziwe zimezingatia sheria zote za utayarishaji wa filamu kwabla ya kupelekwa sokoni.
iii. Wasambazaji na Watayarishaji wahakikishe kwamba wanarekebisha mikataba yao kuwa ni yenye maslahi kwa Wasanii wote wanaofanya nao kazi.
iv. Kufichua Maharamia wa kazi za Wasanii ili kufichua uharamia wao.

b. Umuhimu wa Bima ya Afya

Rais wa TAFF alisema kwamba sasa wakati umefika muda wa Wasanii kujiunga katika mifuko ya hifadhi ya jamii kwa lengo la kujiwekea akiba zitazo wasaidia katika matatizo ya afya zao, mikopo kwa ajili kuendeleza kazi zetu na mengineyo lakini alitumia fursa hiyo kusema kwamba NSSF wametaka TAFF kuingiza wanachama wake kuingia katika mfuko huo, majadiliano yanaendelea yatapo kamilika wadau watajulishwa kupitia vyama na makundi yao.

b. Ushiriki wa Wasanii wa Filamu katika Katiba Mpya na Sensa 2012

Rais aliwataka Wasanii wa Filamu wote kuhakikisha kuwa pale kamati ya Katiba itapowa fikia wahakikishe kuwa watajitokeza kwa wingi kwa ajili kutoa mapendekezo yetu kwa sababu ni jambo muhimu na limekuja kwa wakati muafaka kwa hiyo si jambo la kuzembea.Alisisitiza kwamba itakuwa ni aibu kwa vizazi vijavyo kwamba katika madiliko ya Katiba mpya ya nchi Wasanii wa Filamu hawakushiriki kutoa maoni yao, aliwaomba wajitokeze kwa wingi sana.

c. Umoja na Maadili kwa Wasanii

Umoja
Rais wa TAFF alisema kwamba katika umoja kwa kiasi Fulani tumeanza kufanikiwa kwa sababu ya Wasanii tumekuwa tukishirikiana katika matatizo mbalimbali lakini pia anapongeza tukio la kumaliza mgogoro uliokuwa kati ya Bongo Movie na TAFF kwa siku ya leo hivyo aliwataka wasanii kuwa wakweli na waaminifu miongoni mwetu. Mwisho aliwataka Wasanii kuhudhuria vikao mbalimbali vitavyoitishwa na vyama wanachama au Shirikisho kwa sababu ya kupata taarifa muhimu.

Maadili
Rais wa Shirikisho la Filamu, katika suala la maadili aliweka wazi kwamba Wasanii wa Filamu mbele ya jamii tumechafuka sana. Tusijione tuko sawa tunapokuwa wenyewe kwa wenyewe lakini mbele ya jamii hatusomeki vizuri. Katika hili anaomba wasanii wote tushirikiane kujilinda na tabia zetu kwa lengo la kuleta heshima mbele ya jamii. Lakini pia alisisitiza kwamba katika suala la maadili Shirikisho la Filamu halitamvumilia hata mmoja miongoni mwa wale wataojitokeza kutuchafua na atayejitokeza tutamshughulikia.ipasavyo.

d. Kukamatwa kwa Mharamia wa Kazi za Wasanii
Kama tulivyotangulia kusema hapo awali kwamba Bwana Masawe maarufu kwa jina la Msukuma alikamatwa nyumbani kwake ambapo pia anafanya ofisi kwa ajili ya kudurufu kazi mbalimbali za Wasanii. Kazi zilizokamatwa kwa haramia huyo ni filamu ya Hatia (Tino) , Glory of Ramadhani (Ray), muziki wa Taarabu Mpenzi Chokalte (Mzee Yusuph). Rais wa TAFF aliwataka wasanii wote ili kuonesha mshikamano wa kweli lazima tuhudhurie kwa wingi mahakamani bila ya kukosa pale kesi itapoanza kusikilizwa. Kuonekana mahakamani kutasaidia kudhihirisha machungu kwa wezi wa kazi zetu na endapo tusipojitokeza maana yake tumeridhika na maovu yanayofanywa na maharamia hawa. Lakini pia kampeni itakuwa endelevu ikiwa ni sehemu ya kutekeleza tamko na agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Gharib Billal alilolitoa Musoma katika Uzinduzi wa kanuni za sheria za filamu na michezo ya kuigiza mwaka 2011 mwezi Oktoba.

KUFUNGA MKUTANO

Harambee Maalumu
Baada ya taarifa ya Rais wa Shirikisho Bwana Simoni Mwakifwamba kumaliza kuzungumza Katibu wa Shirikisho la Filamu Bwana Wilson Makubi aliwashukuru wadau kwa kuhudhuria mkutano huo lakini pia wadau waliomba kufanyike harambee ya kuchangia gharama za kuendesha kesi hiyo. Wadau walikubali kuchangia na ilikuwa kama ifuatavyo:

a. Ahadi ya Usafiri kwenda mahakamani zilitolewa na kampuni zifuatazo;

i. Kampuni ya CYG chini ya Issa Mussa (Cloud )
ii. Kampuni ya Cheni Art Creation (Dr Cheni)
iii. Nice Entartainment (Mtunisi)

b. Ahadi ya Kuchangia Tshirt zenye ujumbe maalumu.

i. Tuesday Kihangalla fulana 100
ii. Dr Cheni fulana 50
iii. Chriss Creation Fulana 100
iv. Issa Mussa (Cloud) Fulana 200
v. Christian Promoters fulana 50.

Jumla ya Fulana ziliahidiwa kutolewa na wadau hao ni 500 Wasambazaji na Watayarishaji walipendekeza kwamba fulana hizo mara baada ya kukamilika zitauzwa kwa gharama ya shilingi 2000/= kila moja kuchangia gharama za uendeshaji wa Shirikisho la Filamu Tanzania.

Fedha Taslimu zilizochangwa zilikuwa ni Shilingi 75,000/= lakini pia wadau waliwachangia Mzee Kankaa na Mzee Small jumla ya shilingi 150,000/= ili ziwasaidie katika matibabu yao na matumizi kwa kuwa Wazee wetu hawa ni wagonjwa kwa muda mrefu sasa Mkutano ulifungwa saa 10 alasiri.

Ushauri kwa Mheshimiwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mh Dk Fenella Mkangara tunaomba achukue hatua za makusudi kuwaita viongozi watatu wa kila upande wa Shirikisho la Filamu Tanzania na Viongozi wa Bongo Movie kwa ajili ya kuhitimisha na kusawazisha zaidi maelewano hayo kuimarisha tasnia.

Muhtasari huu umepitiwa na:
SIMONI J. MWAKIFWAMBA - RAIS
WILSON R. MAKUBI - KATIBU MTENDAJI
TAREHE 18 AGOSTI 2012

Source: http://www.wavuti.com/#ixzz23v3iGISL

Majina ya Wanaowania Nyadhifa mbalimbali UVCCM

1. MWENYEKITI TAIFA

1 Asila Ali SALIM
2 Jamal K. ALI
3 Lulu Mcham ABDALLAH
4 Lusekelo W. MALEMA
5 Mbarouk M. MBAROUK
6 Mwana Amina Haji FARUK
7 Nadra Juma MOHAMED
8 Rashid Simai MSARAKA
9 Sadifa Juma KHAMIS
10 Thabit Jecha KOMBO

2. MAKAMU MWENYEKITI WA TAIFA

1 Abubakari Damiani ASENGA
2 Adolph Florian MILUNGA
3 Ally Salum HAPI
4 Antony MAVUNDE
5 Augustino Oscar MATEFU
6 Daniel Moses ZENDA
7 Daud Paulo MSUNGU
8 Donatus T. RUTAGIMBWA
9 Faidha Suleiman SALIM
10 Felician MTAHENGERWA
11 Godwin E. KUNAMBI
12 Goodhance R. MSANGI
13 Idd Yasini MAJUTO
14 Innocent MELECK
15 Jackson KANGOYE
16 John Maurice DEYA
17 Joseph Kulwa MALONGO
18 Langton ZACHARIA
19 Masoud Hamis MASOUD
20 Mboni MHITA
21 Odilia Abraham BATHLOMEO
22 Paul Christian MAKONDA
23 Peter H. LUENA
24 Salum Halfan MTELELA
25 Sango I. Gungu KASERA
25 Silanda MGOMBELO
26 Theresia Adrian MTEWELE
27 Zangina S. ZANGINA

3. HALMASHAURI KUUYA CCM TAIFA – NAFASI SITA - BARA

1 Abubakari Damiani ASENGA
2 Adolph Florian MILUNGA
3 Ahmed Mustafa NYANG’ANYI
4 Ally Mussa SAMIZI
5 Ally Salum HAPI
6 Amani Wilfred NDUHIJE
7 Angella Onesmo MWANRI
8 Augustino P. NDIMBO
9 Augustine S. SIMWIYA
10 Bertha Yona MINGA
11 Busoro Mohamed PAZI
12 Daud Babu MRINDOKO
13 Daud Paulo MSUNGU
14 Edna Erasto KWILASA
15 Emma Julius MEDDA
16 Emmanuel John SHILANTU
17 Faidha Suleiman SALIM
18 Faidha Suleiman SALIM
19 Fatma Jumbe MWALIM
20 Gilead John TERI
21 Godwin E. KUNAMBI
22 Halima BULEMBO
23 Hadija Mtambi SAID
24 Hassan H. CHAMSHAMA
25 Idrisa Washngton MCHOME
26 Jonas Estomih NKYA
27 Joyce Judith MARTINE
28 Kaeni Edwin NJUNWA
29 Kelvin MBOGO
30 Kheri L. WILLIAM
31 Luhende Richard LUHENDE
32 Lulu Abbas MTEMVU
33 Lusekelo Williard MALEMA
34 Modesta KAMONA
35 Mohamed A. KAPUFI
36 Mohamed Omary MASENGA
37 Mboni Mohamed MHITA
38 Neema K. NYANGALILO
39 Olivia Herry SANARE
41 Peter Isaya KASERA
42 Rahim Juma NG’WANANG’WAKA
43 Rashid GEWA
44 Richard Raymond MBILINYI
45 Salim Rajab KISEBENGO
46 Sango Issaya G. KASERA
47 Saul Thom MWAISENYA
48 Suleiman H. J. SERERA
49 Stephen J. NYAGONDE
50 Theresia Adrian MTEWELE
51 Vaileth Elias SAMBILWA
52 Zuberi Said BUNDALA
53 Lumola Stephen KAHUNDI


4. BARAZA KUU VITI VITANO - BARA

1 Abubakari Damiani ASENGA
5 Ally Mussa SAMIZI
6 Ally Salum HAPI
7 Amani Wilfred NDUHIJE
8 Augustine S. SIMWIYA
8 Baraka NKATURA
9 Bertha Yona MINGA
10 Dotnatus T. RUTAGIMBWA
11 Benson Peter MOLLEL
12 Kaeni Edwin NJUNWA
13 Mohamed A. KAPUFI
14 Fatma Jumbe MWALIM
15 Felician MTAHENGERWA
16 Halima BULEMBO
17 Adinani Selemani LIVAMBA
18 David MWAKIPOSA
19 Ester Charles MAMBALI
20 Emmanuel John SHILANTU
21 Kelvin MBOGO
22 Kheri L. WILLIAM
23 Luhende Richard LUHENDE
24 Mboni MHITA
25 Mwita I. NYAGONDE
26 Nassor Ally CHUMA
27 Salum Rajab KISEBENGO
28 Olivia Herry SANARE
29 Mohamed Omary MASENYA
30 Masoud Hamis MASOUD
29 Sango Issaya G. KASERA
30 Neema Kumba NYANGALILO
31 Saul Thom MWAISENYA
32 Lusekelo Williard MALEMA
33 Peter Isaya KASERA
34 Rahim Juma NG’WANANG’WAKA
35 Rashid Semindu PAWA
36 Rashid GEWA
37 Shedrack Gabriel MBOGOYE
38 Joyce Judith MARTINE
39 Busoro Mohamed PAZI
40 Richard Raymond MBILINYI
41 Stephen J. NYAGONDE
42 Suleiman H. J. SERERA
43 Vaileth Elias SAMBILWA
44 Theresia Adrian MTEWELE
45 Yohana Haruni MUNEMA
46 Zuberi Said BUNDALA
47 Isane Njale MAZWILE
48 Cretus MPIGA
49 Jerome Raymond TINGISI

5. NAFASI MOJA UWAKILISHI UWT

1 Frida WILFRED
2 Joyce Judith MARTINE
3 Josephine S. MWAGOSE
4 Hawa Mchafu CHAKOMA
5 Mboni Mohamed MHITA
6 Neema K. NYANGALILO
7 Vaileth Elias SAMBILWA
8 Rabia Abdalla HAMID

6. NAFASI MOJA UWAKILISHI WAZAZI

1 David John MWAKIPOSA
2 Karim Furaha LICHELA
3 Yusuph Masige LIMA
4 Salum Salum MGAYA
5 Yohana Haruni MUNEMA

7. WAGOMBEA WAHALMASHAURI KUU CCM TAIFA - VITI VINNE ZANZIBAR

1. Abubakari Ali HAMDANI
2. Asha Juma OTHMAN
3. Asha Khamis ABDALLAH
4. Asha Mohamed OMARI
5. Ashura Abdallah SIMAI
6. Bakari Musa VUAI
7. Bukheri Juma SULEIMAN
8. Chirstina Joram ANTHON
9. Daudi K. J. ISMAIL
10. Fahym Ally MWINYI
11. Fadhila Nassor ABDI
12. Haji Shabani MWALIMU
13. Ismail Malick MOHAMED
14. Jumanne Alli HAJI
15. Khamis Juma KHATIBU
16. Khamis Mtumwa ALI
17. Khamisi Rashid KHEIR
18. Latifa Kassim MABROUK
19. Lulu Mshami ABDULLAH
20. Mihayo J. S. N’HUNGA
21. Mwatima Salum HAMED
22. Nadra Ghulam RASHID
23. Omar Juma AMEIR
24. Omari Sleiman MOHAMED
25. Rabia Abdalla HAMID
26. Ramadhan A. SLEIMANI
27. Sadifa Juma KHAMIS
28. Salumu Khamis HAJI
29. Samra Bakari YUSUF
30. Shaka Hamdu SHAKA
31. Suna Jumanne SALEH
32. Thabit Jecha KOMBO

Source: http://www.wavuti.com/#ixzz23v2DEb00

Majina ya Wanaowania Nyadhifa mbalimbali UVCCM

1. MWENYEKITI TAIFA

1 Asila Ali SALIM
2 Jamal K. ALI
3 Lulu Mcham ABDALLAH
4 Lusekelo W. MALEMA
5 Mbarouk M. MBAROUK
6 Mwana Amina Haji FARUK
7 Nadra Juma MOHAMED
8 Rashid Simai MSARAKA
9 Sadifa Juma KHAMIS
10 Thabit Jecha KOMBO

2. MAKAMU MWENYEKITI WA TAIFA

1 Abubakari Damiani ASENGA
2 Adolph Florian MILUNGA
3 Ally Salum HAPI
4 Antony MAVUNDE
5 Augustino Oscar MATEFU
6 Daniel Moses ZENDA
7 Daud Paulo MSUNGU
8 Donatus T. RUTAGIMBWA
9 Faidha Suleiman SALIM
10 Felician MTAHENGERWA
11 Godwin E. KUNAMBI
12 Goodhance R. MSANGI
13 Idd Yasini MAJUTO
14 Innocent MELECK
15 Jackson KANGOYE
16 John Maurice DEYA
17 Joseph Kulwa MALONGO
18 Langton ZACHARIA
19 Masoud Hamis MASOUD
20 Mboni MHITA
21 Odilia Abraham BATHLOMEO
22 Paul Christian MAKONDA
23 Peter H. LUENA
24 Salum Halfan MTELELA
25 Sango I. Gungu KASERA
25 Silanda MGOMBELO
26 Theresia Adrian MTEWELE
27 Zangina S. ZANGINA

3. HALMASHAURI KUUYA CCM TAIFA – NAFASI SITA - BARA

1 Abubakari Damiani ASENGA
2 Adolph Florian MILUNGA
3 Ahmed Mustafa NYANG’ANYI
4 Ally Mussa SAMIZI
5 Ally Salum HAPI
6 Amani Wilfred NDUHIJE
7 Angella Onesmo MWANRI
8 Augustino P. NDIMBO
9 Augustine S. SIMWIYA
10 Bertha Yona MINGA
11 Busoro Mohamed PAZI
12 Daud Babu MRINDOKO
13 Daud Paulo MSUNGU
14 Edna Erasto KWILASA
15 Emma Julius MEDDA
16 Emmanuel John SHILANTU
17 Faidha Suleiman SALIM
18 Faidha Suleiman SALIM
19 Fatma Jumbe MWALIM
20 Gilead John TERI
21 Godwin E. KUNAMBI
22 Halima BULEMBO
23 Hadija Mtambi SAID
24 Hassan H. CHAMSHAMA
25 Idrisa Washngton MCHOME
26 Jonas Estomih NKYA
27 Joyce Judith MARTINE
28 Kaeni Edwin NJUNWA
29 Kelvin MBOGO
30 Kheri L. WILLIAM
31 Luhende Richard LUHENDE
32 Lulu Abbas MTEMVU
33 Lusekelo Williard MALEMA
34 Modesta KAMONA
35 Mohamed A. KAPUFI
36 Mohamed Omary MASENGA
37 Mboni Mohamed MHITA
38 Neema K. NYANGALILO
39 Olivia Herry SANARE
41 Peter Isaya KASERA
42 Rahim Juma NG’WANANG’WAKA
43 Rashid GEWA
44 Richard Raymond MBILINYI
45 Salim Rajab KISEBENGO
46 Sango Issaya G. KASERA
47 Saul Thom MWAISENYA
48 Suleiman H. J. SERERA
49 Stephen J. NYAGONDE
50 Theresia Adrian MTEWELE
51 Vaileth Elias SAMBILWA
52 Zuberi Said BUNDALA
53 Lumola Stephen KAHUNDI


4. BARAZA KUU VITI VITANO - BARA

1 Abubakari Damiani ASENGA
5 Ally Mussa SAMIZI
6 Ally Salum HAPI
7 Amani Wilfred NDUHIJE
8 Augustine S. SIMWIYA
8 Baraka NKATURA
9 Bertha Yona MINGA
10 Dotnatus T. RUTAGIMBWA
11 Benson Peter MOLLEL
12 Kaeni Edwin NJUNWA
13 Mohamed A. KAPUFI
14 Fatma Jumbe MWALIM
15 Felician MTAHENGERWA
16 Halima BULEMBO
17 Adinani Selemani LIVAMBA
18 David MWAKIPOSA
19 Ester Charles MAMBALI
20 Emmanuel John SHILANTU
21 Kelvin MBOGO
22 Kheri L. WILLIAM
23 Luhende Richard LUHENDE
24 Mboni MHITA
25 Mwita I. NYAGONDE
26 Nassor Ally CHUMA
27 Salum Rajab KISEBENGO
28 Olivia Herry SANARE
29 Mohamed Omary MASENYA
30 Masoud Hamis MASOUD
29 Sango Issaya G. KASERA
30 Neema Kumba NYANGALILO
31 Saul Thom MWAISENYA
32 Lusekelo Williard MALEMA
33 Peter Isaya KASERA
34 Rahim Juma NG’WANANG’WAKA
35 Rashid Semindu PAWA
36 Rashid GEWA
37 Shedrack Gabriel MBOGOYE
38 Joyce Judith MARTINE
39 Busoro Mohamed PAZI
40 Richard Raymond MBILINYI
41 Stephen J. NYAGONDE
42 Suleiman H. J. SERERA
43 Vaileth Elias SAMBILWA
44 Theresia Adrian MTEWELE
45 Yohana Haruni MUNEMA
46 Zuberi Said BUNDALA
47 Isane Njale MAZWILE
48 Cretus MPIGA
49 Jerome Raymond TINGISI

5. NAFASI MOJA UWAKILISHI UWT

1 Frida WILFRED
2 Joyce Judith MARTINE
3 Josephine S. MWAGOSE
4 Hawa Mchafu CHAKOMA
5 Mboni Mohamed MHITA
6 Neema K. NYANGALILO
7 Vaileth Elias SAMBILWA
8 Rabia Abdalla HAMID

6. NAFASI MOJA UWAKILISHI WAZAZI

1 David John MWAKIPOSA
2 Karim Furaha LICHELA
3 Yusuph Masige LIMA
4 Salum Salum MGAYA
5 Yohana Haruni MUNEMA

7. WAGOMBEA WAHALMASHAURI KUU CCM TAIFA - VITI VINNE ZANZIBAR

1. Abubakari Ali HAMDANI
2. Asha Juma OTHMAN
3. Asha Khamis ABDALLAH
4. Asha Mohamed OMARI
5. Ashura Abdallah SIMAI
6. Bakari Musa VUAI
7. Bukheri Juma SULEIMAN
8. Chirstina Joram ANTHON
9. Daudi K. J. ISMAIL
10. Fahym Ally MWINYI
11. Fadhila Nassor ABDI
12. Haji Shabani MWALIMU
13. Ismail Malick MOHAMED
14. Jumanne Alli HAJI
15. Khamis Juma KHATIBU
16. Khamis Mtumwa ALI
17. Khamisi Rashid KHEIR
18. Latifa Kassim MABROUK
19. Lulu Mshami ABDULLAH
20. Mihayo J. S. N’HUNGA
21. Mwatima Salum HAMED
22. Nadra Ghulam RASHID
23. Omar Juma AMEIR
24. Omari Sleiman MOHAMED
25. Rabia Abdalla HAMID
26. Ramadhan A. SLEIMANI
27. Sadifa Juma KHAMIS
28. Salumu Khamis HAJI
29. Samra Bakari YUSUF
30. Shaka Hamdu SHAKA
31. Suna Jumanne SALEH
32. Thabit Jecha KOMBO

Source: http://www.wavuti.com/#ixzz23v2DEb00

Friday, August 17, 2012

The Last Ten Days of Ramadan

It was the Habit of the prophet during the last ten nights of Ramadan to increase worship. He used to spend the whole night in worship and encouraged his family to do the same, according to their ability, and he kept away from his wives. Aisha, the wife of the prophet, said "when the last ten nights of Ramadan started the prophet kept away from his wives and spent the whole night worshipping and encouraging his family to do the same.

Lailat el Qadr, or The Night of Power, is one of the nights in the last ten nights of Ramadan and this night is a blessed night. God made it honoured and better than a thousand months. This is because the Holy Quran began to be revealed on this night and it is said in the Holy Quran "in the name of God, most gracious, most merciful, we have revealed this (message) in the night of power. The night of power is better than a thousand months. Therein comes down angels and the spirits descend by the leave of their Lord upon command until the rising of the dawn.

Whoever, spends this blessed night in worship, his previous sins will be forgiven, for the prophet (peace be upon him) said "whoever fasts the month of Ramadan for the belief in, and sake of God, his previous sins will be forgiven and whoever spends the night of power (Lailat al Qadr) praying for belief and for the sake of God, his previous sins will be forgiven".

A large number of the traditions of the prophet encourage the Muslims to believe that the Night of Power is one of the last seven nights of the month. But some traditions make others think that it is one of the last ten nights of the month. Other traditions again, give us to be that it is one of the odd numbered nights of the last ten nights.

One of the above traditions comes from Ibn Umar, who said "A number of the companions of the prophet (peace be upon him) has visions regarding Lailat al Qadr and, according to these visions, it is during the last seven nights of Ramadan. When their visions were related to the prophet (peace be upon him) he said "I see your visions agree that the Night of Power will be during the last seven nights. Whoever wants to look for it he should look on one of these nights".

Aisha, the wife of the prophet, related that the prophet (peace be upon him) looked for the Night of Power on the odd numbered nights within the last ten days of Ramadan, whereas Abu Sa'id al Khudr (may God be pleased with him) " God's Messenger stayed in the mosque for worship (takafa) during the middle ten nights of Ramadan in order to find out the night of power.

This was before it has been shown to him. At the end of this period he request that his tent should be taken down. His request was carried out, but afterwards he knew from God that the night of power would during the last ten nights of the Ramadan. So he asked for his tent to set up again and it was done.

Then he came out to the people and said "O people, God has revealed to me when the night of power will be, and I have come out to inform you. At the same moment two men came to me complaining about each other and with them came Satan. So I have forgotten the exact night. But look for it during the last ten nights of Ramadan, particularly the ninth, seventh, or fifth before the end".

Abu Nadra said " I told Abu Sa'id that he knows numbers better we do". Abu Sa'id agreed, saying "yes, we are more fitted in reckoning than you are". Then Abu Nadra asked "what does the ninth, seventh or fifth mean?" Abu Sa'id answered "it will be the night following by the 21st, the 23rd and 25th".

Therefore Muslim scholars have different opinions regarding the exact date of the night of power. Some look for it on the night of the 23rd and some on the night of the 27th. This latter is the choice of the majority, but the reason is not known for sure.

This uncertainty is a good thing because if people knew exactly which was the night of power they would stop their worship before and after that night, therefore it has been hidden so as to give as opportunity for the people to have more blessing of worship and to follow the ways of the prophet (peace be upon him).

It has been related that some of the prophet's companion confirmed it as being the night of the 27th, as Mu'awia said. And also it has been related that a man named Zirr Ibn Hwbaish said " I have told Ubiyy Ibn Ka'b " your brother Ibn Mas'ud says whoever spends the nights of the whole year for worship will certainly not miss the night of power".

Ubiyya replied "May the mercy of God come to Ibn Mas'ud. He said this because his approval of teaching people to increase their activity of worship, even though Ibn Mas'ud certainly knew the night of power was in the month of Ramadan and its was one of the last ten nights of Ramadan and that it was the night of the 27th.

Then Ubiyya swore by God confirming that it was the night of the 27th. "When I asked on what ground do you state that, Abu Mondhir?", he replied " By the indication of which God's Messenger informed us, thatthe sun rises on that day without rays".

This what Muslim scholars think about the Night of Power. And it is to be hoped that God will guide all and grant us the blessing of this month and this night.

ZAKAT AL- FITIR

At the end of the fasting there is payable a kind of zakat connected with that month and this we call zakat al-fitr. It has to be paid before the Id prayer and is an obligatory payment upon every Muslim, male and female, young and old, freeman or slave, if there is any, and it is the master who is responsible for payment in respect of his servant or his slave.

It is obvious that poor people are exempted from such payment and the head of the family will be responsible for payment on behalf of his wife, children and servant and all those who are under his care. This is because of what is related by Ibn Abbas " At the end of Ramadan bring forth the sadaqa relating to your fast.

God's Messenger prescribed the sadaqa as a Sa' of dry dates or barely or a Sa' of wheat payable by every freeman or slave, male or female, young or old " and also what is related by Ibn Umar who said "God's Messenger prescribed as a Zakat payable by slave and freeman, young or old on breaking the fast of Ramadan as a Sa' of dried dates or a Sa' of barely and gave command that this should be paid before the people went out to pray".

As the need of people now-a-days is more for money, with to buy for themselves and their children what they want, it is permitted that this Zakat be paid in cash, particularly in a country like England. The amount to paid for each person is nearly 30p (thirty pence) but it may be that, in the future, this amount will be increased because of the continued rise in the cost of things.

The aim of prescribing this Zakat at this particular time is to help needy people to get what they and their families need on Id day, so that they can share with the other members of the society their happiness and pleasure, and as a sign of co-operation and unity among all of them.

What I really want to say to my Brothers about their duty during Ramadan according to the guidance of our prophet (peace be upon him)is that I hope they will benefit from it and it will be beneficial in connection with their religious activities.

Wanahabari washiriki semina elekezi kuhusiana na mchakato wa mabadiliko ya katiba mpya

Mwandishi Mkongwe hapa nchini,Mzee Phill Karashani ambaye aliwahi kupata tuzo ya Maisha ya Mafanikio katika Tasnia ya Habari mwaka 2011,katika tuzo ya Wanahabari Bora wa Mwaka 2011,akifafanua jambo kwenye semina elekezi ya jinsi ya ushiriki wa vyombo vya habari kuhusiana na mchakato wa mabadiliko ya Katiba Mpya iliyowahusu Wanahabari/Wachora Katuni na wadau wengine mbalimbali iliyofanyika kwenye moja ya ukumbi wa Land Mark hotel,Ubungo jijini Dar Es Salaam.Semina hiyo imeandaliwa na Kikundi Cha Sheria na Haki za Binadamu Cha TIFPA kwa Msaada wa Shirika la Ford Foundation la Marekani .
Baadhi ya Wanahabari,Wachora Katuni na Wadau wengine mbalimbali wakifuatilia mada mbali mbali zilizokuwa zikitolewa kwenye semina elekezi ya jinsi ya ushiriki wa vyombo vya habari kuhusiana na mchakato wa mabadiliko ya Katiba Mpya iliyofanyika kwenye moja ya ukumbi wa Land Mark hotel,Ubungo jijini Dar Es Salaam.Semina hiyo imeandaliwa na Kikundi Cha Sheria na Haki za Binadamu Cha TIFPA kwa Msaada wa Shirika la Ford Foundation la Marekani .hiyo kuhusiana na mchakato wa kutoa maoni kuhusu Katiba Mpya na pia namna ya kuielimisha jamii katika umuhimu wa kushiriki
Mchora Katuni mahiri Masoud Kipanya na Mmoja wa watangazaji wa kutoka Times FM Radio Ibrahim Issa wakifuatilia mijadala mbalimbali iliyokuwa ikiendelea kwenye semina elekezi ya jinsi ya ushiriki wa vyombo vya habari kuhusiana na mchakato wa mabadiliko ya Katiba Mpya iliyofanyika kwenye moja ya ukumbi wa Land Mark hotel,Ubungo jijini Dar Es Salaam.Semina hiyo imeandaliwa na Kikundi Cha Sheria na Haki za Binadamu Cha TIFPA kwa Msaada wa Shirika la Ford Foundation la Marekani .
Naibu Mhariri Mtendaji wa Free Media ambao ni wachapishaji wa gazeti la Tanzania Daima na Sayari, Ansbert Ngurumo akifafanua jambo mapema leo kwenye semina elekezi ya jinsi ya ushiriki wa vyombo vya habari kuhusiana na mchakato wa mabadiliko ya Katiba Mpya iliyofanyika kwenye moja ya ukumbi wa Land Mark hotel,Ubungo jijini Dar Es Salaam,kushoto kwake ni Mwandishi Mkongwe hapa nchini,Mzee Phill Karashani
Mwenyekiti wa Kikundi Cha Sheria na Haki za Binadamu Cha TIFPA (Chama Cha Wanafunzi waliofadhiliwa na Shirika la Ford Foundation la Marekani) akielezea jambo kwa Wanahabari,Wachora Katuni na wadau wengine mbalimbali kwenye semina elekezi ya jinsi ya ushiriki wa vyombo vya habari kuhusiana na mchakato wa mabadiliko ya Katiba Mpya.
Mijadala ikiendelea kwenye semina hiyo elekezi ya jinsi ya ushiriki wa vyombo vya habari kuhusiana na mchakato wa mabadiliko ya Katiba Mpya
Mwandishi Mwandamizi kutoka Magazeti ya Serikali,Beda Msimbe akifuatilia mijadala mbalimbali iliyokuwa ikitolewa kwenye semina elekezi ya jinsi ya ushiriki wa vyombo vya habari kuhusiana na mchakato wa mabadiliko ya Katiba Mpya.
Washiriki wa Semina hiyo wakifuatilia mijadala iliyokuwa ikiendelea kwenye semina hiyo.
Washiriki wa Semina hiyo wakifuatilia mijadala iliyokuwa ikiendelea kwenye semina hiyo elekezi ya jinsi ya ushiriki wa vyombo vya habari kuhusiana na mchakato wa mabadiliko ya Katiba Mpya.

RAIS KIKWETE AELEKEA MSUMBIJI KUHUDHURIA MKUTANO WA SADC

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali aliyemsindikiza katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana Agosti 16, 2012 muda mfupi kabla ya kuondoka kuekelea Msumbiji kuhudhuria mkutano wa SADC jijini Maputo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mhe Sophia Mjema katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana Agosti 16, 2012 muda mfupi kabla ya kuondoka kuekelea Msumbiji kuhudhuria mkutano wa SADC jijini Maputo.
(Picha na IKULU)

JUMUIYA YA KIISLAMU DMV YATOA RATIBA YA SHEREHE ZA EID

JAMAA ACHENGULIWA NA UZINDUZI WA SHINDA NOAH

Akiwasili eneo la uzinduzi.

...akivutiwa na wacheza shoo.

...akianza makamuzi.

...burudani imekolea.

...akionyesha ufundi.

...akionyesha staili tofauti.

...ilikuwa full burudani.

...wananchi wakishuhudia burudani kutoka kwa mdau huyo.

Mdau mmoja wa magazeti ya kampuni ya Global Publishers ambao ni wachapishaji wa Magazeti ya Uwazi, Amani, Championi, Ijumaa, Risasi, na Ijumaa Wikienda hivi karibuni alichenguliwa na burudani zilizokuwa zinaendelea eneo la Ubungo jijini Dar es Salaam na kuamua kushusha burudani ya aina yake wakati wa uzinduzi wa shindano la SHINDA NOAH linaloendeshwa na Global Publishers

Rais wa Zanzibar Dk Ali Shein Afuturisha Mkoa wa Mjini Magharibi

Baadhi ya Wananchi na Waumini wa Dini ya Kiislamu wa Mkoa wa Mjini Magharibi wakianza kufutari kwa kunywa madafu kabla ya kula futari jana walipoalikwa katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza La Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,ikiwa ni kawaida yake kuwaalika Wananchi wa Mkoa huo kila ifikapo mwezi kama huu kwa futari maalum.
Baadhi ya Viongozi na Wananchi Waumini wa Dini ya Kiislamu wa Mkoa wa Mjini Magharibi,wakiwa katika chakula cha Futari katika Mwezi mtukufu wa Ramadhan,iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar
Baadhi ya Wananchi na Waumini wa Dini ya Kiislamu wa Mkoa wa Mjini Magharibi wakiwa katika futari iliyoandaliwa jana ,katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza La Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,ikiwa ni kawaida yake kuwaalika Wananchi wa Mkoa huo kila ifikapo mwezi kama huu kwa futari maalum.
Baadhi ya Akina mama wa Mkoa wa Mjini Magharibi wakiwa katika chakula cha Futari,iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,katika viwanja vya Ikulu ya Zanzibar.
Baadhi ya Akina mama wa Mkoa wa Mjini Magharibi wakiwa katika chakula cha Futari,iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,katika viwanja vya Ikulu ya Zanzibar.
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, (wa pili kushoto) akijumuika na akinamamawa wa Mkoa wa Mjini Magharibi katika Chakula cha Futari iliyoandaliwa kwa wananchi hao na Rais wa Zanzibar Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein, katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar, (wengine kulia) Mama Shadiya Karume, Mama Pili Balozi Seif na Waziri wa Muungano Samia Suluhu Hassan, (kushoto).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kulia) akijumuika na wananchi pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Mjini Magharibi katika Futari, aliyowaandalia wananchi hao katika viwanja vya IKulu ya Mjini Zanzibar jana, (kulia) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Abdalla Mwinyi Khamis,Rais Mstaafu wa Zanzibar Dk.Amaan Abeid Karume,(kushoto) na Mufti wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Viongozi na wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi baada ya kufutari nao pamoja jana katika futari aliyowaandalia katika viwanja vya IKulu ya Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein, na Mkewe Mama Mwanamwema Shein, wakisalimiana na Viongozi na Wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi baada ya kumalizika Futari waliyowaandalia katika Viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar.
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, (kulia) akisalimiana na mke wa Rais mstaafu wa Zanzibar Mama Shadya Karume, baada ya Futari iliyoandaliwa kwa wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi na Rais wa Zanzibar Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein, katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar.Picha na Ramadhan Othman, Ikulu-Zanzibar

CFAO MOTORS YAFUTURISHA WATEJA WAKE

Mkurugenzi wa Biashara wa CFAO Motors Wayne Mcintosh akizungumza na mmoja wa wateja wa kampuni hiyo kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na CFAO Motors maalum kwa wateja hao katika hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Sales Administration & Suzuki Brand Manager wa CFAO Motors Bw. Luv Gadvi (kulia) akisalimiana na mmoja wa wateja wa kampuni hiyo wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa jijini Dar es Salaam katika hoteli ya Serena maalum kwa wateja wa kampuni hiyo.Katikati ni Mkurugenzi mpya wa kampuni mpya ya Alliance Motors Bw. Alfred Minja.
Meneja Masoko wa CFAO Motors Tharaia Ahmed (kulia) wakibadilishana kadi na mmoja wa wateja wa kampuni hiyo wakati wa hafla ya futari iliyodaliwa na kampuni hiyo maalum kwa wateja wake.
Mkurugenzi mpya wa kampuni mpya inayouza magari ya 'Volkswagon Amarok' ya Alliance Motors Bw. Alfred Minja na baadhi ya wateja wa kampuni ya CFAO Motors.
Meneja Masoko wa CFAO Motors Tharaia Ahmed (kulia) akibadilishana mawazo na mmoja wa Wateja wa Kampuni hiyo Bw. Zahir Somji kutoka Tanzania Sign writers (kushoto) wakati wa hafla ya futari ya pamoja iliyoandaliwa maalum kwa ajili ya wateja wa CFAO Motors katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa Wafanyakazi wa Kampuni ya CFAO Motors Bw. Azizi Masare akiongoza Swala ya Magharibi kwa baadhi ya Wateja wa Kampuni hiyo wakati wa hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Wateja wa Kampuni CFAO Motors wakipakua futari maalum iliyoandaliwa kwa ajili yao.
Wa kwanza Kulia ni Tender Manager wa CFAO Motors Bw. Marco Kahabi sambamba na Baadhi ya Wateja wa kampuni hiyo wakila futari.
Pichani Juu na Chini ni Baadhi ya Wateja na wafanyakazi wa CFAO Motors wakifurahia burudani ya mcheza shoo wa kiarabu alipokuwa akipita kila meza wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa kwa wateja wa kampuni hiyo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Wateja wa CFAO Motors wakionekana kuvutiwa na burudani hiyo.
Mhasibu Mkuu wa Kampuni ya CFAO Motors Bw. Aldo Pagan (kushoto) akifafanua jambo kwa baadhi ya wateja wa kampuni hiyo wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na CFAO Motors katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

MKUTANO WA CHADEMA KILOSA

Sehemu ya Umati Mkubwa wa Wana Kilosa wakifwatilia kwa umakini hotuba mbalimbali kutoka kwenye mkutano wa CHADEMA
-
Vuguvugu la M4C linaloongozwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA limeonekana kutikisa chama cha wananchi CUF wilayani Kilosa ambapo mbali ya wanachama wengi sana wa CUF kujiunga CHADEMA pia Mjumbe wa mkutano Mkuu CUF Taifa Bwana Wille Lemi alijitoa rasmi katika CUF na kukabidhiwa kadi na Kiongozi wa upinzani nchini ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa.

Katika mkutano huo Dr Slaa aliwataka wananchi wa vyama vyote kuunganisha nguvu kwa pamoja chini ya vuguvugu la M4C ili kuhakikisha katika uchaguzi mkuu ujao wananchi wanapata serikali itakayojali maslahi yao chini ya CHADEMA.

Dr Slaa pia alishukuru mwitikio wa wanakilosa kutokana na mkutano huo kufurika umati mkubwa wa watu.Mbali na CUF kupoteza wanachama wengi pia mamia ya wanaCCM walikihama chama chao na kujiunga rasmi CHADEMA kuunganisha nguvu katika vuguvugu la M4C.Idadi ya wanachama wapya waliojiunga CDM katika mkutano wa Kilosa ulikuwa zaidi ya elfu moja.

Kilosa ilikuwa ni mojawapo ya maeneo yenye wanachama wengi wa CUF lakini inaonekana ziara ya Dr Slaa imesimika rasmi CHADEMA kama chama kinachopendwa zaidi Kilosa.

AJINYONGA AKIDHANI AMEUA MKE BAADA YA KUMSHAMBULIA KWA PANGA

Na Luppy Kung’alo wa Jeshi la Polisi Dodoma.

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Jamuhuri John, mwenye umri wa miaka (28)amekutwa amejinyonga katika mti wa mbuyu baada ya kuwajeruhi kwa Panga mke na mtoto wake kisha kukimbia kusikojulikana.

Akizungumzia tukio hilo, Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, Bw. Edmundi Urio alisema tukio hilo la kujinyonga liligundulika mnamo tarehe 17/08/2012 majira ya saa 06:45 asubuhi, na wananchi waliokuwa wakimfuatilia katika Kijiji cha Kikombo Kata na tarafa ya Kikombo Wilaya ya Dodoma Mjini.

“Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha kujinyonga kwa mtu huyo ni ugomvi wa mapenzi kwani marehemu alikuwa amewajeruhi mke na mtoto wake kwa kuwakata na mapanga kisha kukimbia kusikojulikana hadi alipogundulika amejinyonga.“ Alielezea Kamanda Edmundi Urio.
Bw. Urio alieleza kwamba Marehemu alikuwa na ugomvi na mke wake kwa muda mrefu kitu kilichopelekea mwanamke huyo kutoroka nyumbani kwake na kukimbilia kwenda kuishi Tanga inakodaiwa kuwa ni kwa baba yake mzazi.

Kamanda Edmund Urio alisema, baaada ya kukaa muda mrefu bila kumuona mke wake marehemu alikuwa na wasiwasi kuwa ameolewa, hivyo aliamua kumtafuta mke wake huyo na ndipo alipoamua kwenda kwa mtendaji wa Kijiji hicho cha Kikombo Bw. Wenos Dede kuomba barua ya kumtafuta mke wake Tanga na kupatiwa barua hiyo.

Aidh Bw. Urio alieleza kwamba Jana majira ya saa mbili usiku marehemu na mke wake wakiwa wanarudi toka Tanga walipewa maelekezo kwamba, wafike kwanza kwa mtendaji kumjulisha na kwa usuluhishi zaidi, walipofika hawakumkuta mtendaji kwa kuwa alikuwa amekwenda kuhudhuria semina ya mambo ya Sensa katika Kijiji cha Ihumwa.

“Hivyo wakiwa njiani walishindwa kuelewana, kwani mwanamke alikuwa anataka kwenda kulala kwa bibi yake hapo hapo kijijini, ili kesho yake wamtafute mtendaji ili wamalizane lakini mume wake alikataa na kumwambia amsubiri akachukue shuka ndipo akakimbia nyumbani kwao akachukua Hengo na kulificha katika koti kisha kurudi na kuanza kumshambulia mke wake.” alieleza Kamanda Urio.

Kaimu Kamanda huyo wa Mkoa wa Dodoma, alimtaja mwanamke huyo aliyejeruhiwa kuwa nia Aksa John, mwenye umri wa miaka (21), mgogo na mkazi wa Kikombo, pamoja na mtoto wake aitwaye Gerald John mwenye umri wa miaka (4) aliyejeruhiwa kwa kukatwa Panga katika mguu wake wa kushoto.

Alisema mwanamke huyo amejeruhiwa kwa kukatwa na panga mkono wa kulia chini ya kiganja, na mkono wa kushoto kidole chake gumba kilikatwa kabisa pamoja na kujeruhiwa katika mguu wa kushoto karibu na sehemu ya kukanyagia.

Kamanda Urio Amesema majeruhi wote wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, ambapo Mama huyo amelazwa katika wodi namba nane wakati mtoto wake amelazwa wodi namba moja na kwamba wanaendelea vizuri.

Imetolewa na
Jeshi la POLISI MKOA WA DODOMA
DAWATI LA HABARI, ELIMU NA MAHUSIANO,
Phone: 0715 006523, Luppy Kung’alo – Mrakibu msaidizi wa Polisi (ASP)
Phone: 0712 360203, Silyvester Onesmo – Police Konstebo (PC)

KAMATI MAALUMU YA CCM ZANZIBAR YAKUTANA

Makamu Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu wa Zanzibar, Dkt.Amani Abeid Karume, akiendesha kikao cha kamati maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ya Zanzibar, leo katika ukumbi wa CCMKisiwandui Mjini Zanzibar, (kushoto) ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, pia Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Dkt. Ali Mohamed Shein. Picha na Ramadhan Othman,Ikulu
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,pia Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Dkt. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Viongozi wa CCM, alipowasili katika viwanja vya Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar, kushiriki katika kikao cha siku moja cha Kamati maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ya Zanzibar, kilichofanyika leo.
Wajumbe wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar,wakiwa katika kikao cha siku moja chini ya Mwenyekiti wake, Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais Mstaafu wa Zanzibar Dkt. Amani Abeid Karume,wakiwa katika ukumbi wa CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar, leo.

NHIF YACHANGIA SH. MILIONI 3 UJENZI WA ZAHANATI YA SOMANGILA WILAYA YA TEMEKE DAR ES SALAAM

Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) , Mariam Wilmore (kulia) , akimkabidhi hundi yenye thamani ya sh. Milioni 3 Diwani wa Kata ya Somangila, Aisha Mpanjila (wapili kushoto), wengine ni Meneja wa NHIF Kanda ya Temeke, Imelda Likoko, . Fedha hizo ni kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa Zahanati ya Somangila Wilayani Temeke jijini Dar es Salaam.
Diwani wa Kata ya Somangila, Aisha Mpanjila (wapili kulia), akionesha hundi ya sh. Milioni 3 aliyokabidhiwa na Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF), Mariam Wilmore (kulia) kwa ajili ya kuchangia Ujenzi wa Kituo cha Afya cha Somangila. Wengine ni Meneja wa NHIF Kanda ya Temeke, Imelda Likoko (wapili kushoto) , na Meneja wa Masoko na Elimu kwa Umma wa NHIF, Anjela Mziray.
Na Mwandishi Wetu
DIWANI wa Kata ya Somangila, Wilaya ya Temeke, Aisha Mpanjila amesema kitendo cha Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya cha kusaidia Zahanati ya Mbutu kitahamasisha wananchi wengine kuchangia ujenzi unaoendelea katika zahanati hiyo na hatimaye kumaliza tatizo la miundombinu.

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, jana ulikabidhi hundi yenye thamani ya sh. Milioni 3, kwa lengo la kusaidia ujenzi wa wodi ya akina mama na watoto.

Akipokea msaada huo, Diwani Mpanjila, alisema kuwa NHIF imeonesha njia na imekuwa mfano wa kuigwa hasa kwa kutambua mahitaji ya wananchi katika sekta ya afya.

“Kweli nyie ni Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya…pamoja na kusaidia wanachama wenu katika huduma za matibabu lakini mmekwenda mbali zaidi kwa kutoa hata msaada wa kuboresha vituo vya kutolea huduma msaada ambao unamgusa kila mtu…nawapongeza sana,” alisema.

Kutokana na hali hiyo, Diwani huyo alitumia fursa hiyo kuwaomba wananchi wa maeneo hayo ambao ni wanufaika wa moja kwa moja na zahati hiyo kuunga mkono Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa kuchangia ili ujenzi wa wodi zilizopo zikamilike na zianze kutumika mara moja.

Naye Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Mariam Wilmore amesema NHIF imeguswa na matatizo ya wakazi wa kata hiyo hivyo itaendelae kusaidia kadiri ya uwezo wake.

Zahanati ya Mbutu inahudumiwa zaidi ya wakazi wa mitaa SITA inayozunguka kata hiyo.

Popular Posts