Pages

Friday, August 3, 2012

MGOMBEA NAFASI YA MAKAMU MWENYEKITI WA UMOJA WA VIJANA (UVCCM) TAIFA- SANGOGUNGU KASERA

PRESS STATEMENT

HOTUBAYA MGOMBEA NAFASI YA MAKAMU MWENYEKITI WA UMOJA WA VIJANA (UVCCM) TAIFA- SANGOGUNGU KASERA

2August 20112

Ndg:Wanahabari
Ndg: wanaUVCCM wenzangu

Kwa heshima na unyenyekevu mkubwa naomba kutoa salamu zangu za dhati kwa Watanzania na vijana wenzangu wanchi hii pamoja nanyi waandishi wa Habari kwa kushiriki nami katika safari hiiinayolenga kuunganisha na kujenga hatua za mabadiliko ya maisha ya Vijana waTanzania. Kwa namna ya pekee kabisa niwashukuru na kuwaomba mshikamano vijanawenzangu wa Chama cha Mapinduzi ambao kupitia kwao ninatumia nafasi hii kuomba ridhaa yao ili nipate nafasi ya kuwa chemchem ya mafanikio na mabadiliko katika maisha yetu kwa kuanzia na chama chetu. Leo hii naungana na vijana wenzangu hawa wa ndani ya CCM, kufanya jambo moja kubwa, jambo la kuchukua fomuya kuwania moja ya nafasi kubwa katika jumuiya ya Vijana wa CCM Tanzania. Ninafanya kazi hii leo nikitambua mambo yafuatayo:

Kwanza, ninalenga kuleta mabadiliko yanayotazama aina ya vijana tuliopo sasa, aina ya maisha tunayoishi na aina ya changanoto zinazotukabili mimi nikiwa mmojawapo.

Pili kwa upekee mkubwa, nachukua fomu hii nikibaini hali ya vijana huko tulikotoka na , changamoto tulizopitia na hatari inayotukabili mbele kama hatua stahiki hazitaanza kuchukuliwa na vijana wa aina yangu ambao tuna uzoefu wa kutosha wa maisha ya kawaida ambayo yanahitaji nguvu na akili zetu na za wenzetu waliotutangulia katika kuboresha maisha yetu ili tuweze kuwa raia wema katika nchi yetu na wanachama waadilifu wa chama chetu na jumuiya zake.

Ndugu Waandishi wa Habari;

Kazi hii ya kuchukua fomu ninayoifanya leo hii na kisha kuanza zoezi la kutafuta kuungwa mkono. Ni kazi inayohitaji ushirikiano mkubwa kwa uongozi wa Jumuiya yetu pamoja na vijana mbalimbali bila kujali itikadi zao za vyama vya siasa. Nasema hivi kwa kutambua kuwa UVCCM ndiyo Jumuiya pekee yenye kubeba taswira na matarajio ya vijana wa Tanzania na ambayo siku zote inatakiwa kusimamia maslahi na matakwa ya vijana wa Tanzania na kwakuwa jumuhia hii ni jumuhia ya chama kinachoongoza si chama tawala .

Ndugu zangu wanahabari na wana CCM tunafahamu tofauti kati ya kuongoza na kutawala ndio maana nimetumia neno kuongoza, na Kama kazi hii ilikuwa haifanyiki huko nyuma na kama ilifanyika bila kuridhisha, mimi nimeamua kwa moyo mkunjufu kuingia kuonesha namna jumuiya yetu itakavyoweza kuwatumikia vijana wa Tanzaniana kukiboresha chama cha Mapinduzi ili kitambue wajibu wake kwa vijana wote waTanzania na kwa kufanya hivi kiweze kusimamia misingi iliyolijenga Taifa hili na kuachwa na waasisi wa Taifa letu Hayati Baba Wa Taifa na Hayati Rais Karume ambao walilijenga taifa letu katika misingi ya haki, usawa na ustahimilivu.

Ndugu wana habari; Katika kipindi hiki chakutafuta nafasi ya kuteuliwa kuwa mgombea wa nafasi hii nitabakia kuongozwa na Moto isemayo: Vijana kwanza kwa taifa lenye amani na maendeleo. Bila vijana kuangaliwa na kupewa yale wanayostahiki, ni wazi taifa lenye amani na maendeleo halitakuwepo. Natambua fika kuwa vijana wa Tanzania wanakabiliwa na changamoto kubwa hasa ile inayolenga kubaini ndoto ya maisha yao ya sasa na siku zijazo. Naamini mimi ni mmoja wa vijana hawa ambaye pia ninahitaji kuona vijana walio katika kilimo basi wanaweza kupata soko la mazao yao. Vijanawabeba mikokoteni nao wanafanya kazi hiyo kwa miaka kadhaa na kisha kuboreshaajira zao.

Vijana wanaosoma basi wanahitimu vema na kupata ajira wanazostahiki na pia walio makazini na waliopata nafasi za kuongoza wanaonesha mfano wakufanya kazi kwa kujituma na kwa bidii ili kuonesha kuwa vijana tunaweza na hatuwezi kuliangusha taifa. Natambua haya ninayoyazungumza ni mambo magumu lakini pia natambua yanahitaji mbinu nyingi ili kukabiliana nayo. Kwa sasa natumia nafasi hii kukiomba Chama changu, kuiomba Jumuiya Yetu ya Vijana kutambua kuwa nina dhamira, nina nia, nina sifa za kutosha, nina uwezo wa kufanya majukumu haya ninayoyaomba na ninafahamu kazi za majukumu haya.

Tena nina rekodi katika umri wangu huu wa kufanya mambo ya kutukuka ambayo rekodi yake inaweza kutazamwa pote nilipobahatika kutoa utumishi wangu. Kwa namna isiyoonyesha kuyumba naomba kuwaeleza vijana wenzangu kuwa kutokanana mshikamano wa vijana wenzangu kwangu ni wazi tumejiandaa kushinda katika nafasi hii ili tuweze kuleta mwanga wa mabadiliko katika jumuiya yetu na chama chetu katika maandalizi ya chaguzi zijazo. Ndugu wanahabari ninatambua zipo changamoto nyingi zinazoikabili UVCCM na changamoto hizi zinahitaji kiongozi ambaye atakuwa na uthubutu wakuweza kukabiliana nazo, changamoto kuuni kitaswira, kimuundo, kiimani, kimadhumuni kama ambavyo zimehainishwa kwenyekanuni za ummoja wa vijana. Nina maanisha nini ninapozungumzia taswira ya UVCCM.Taswira ya UVCCM Taifa leo siotaswira ya kimapambano.

Historia yetu ipo wazi jumuiya ya vijana ilishiriki katika mapambano ya kuleta Uhuru, Umoja na mshikamano mtakumbuka wakati TANU Inahangaika na kutafuta Uhuru wa Tanganyika na Afro-Shirazi party ikipambana kuleta Uhuru wa Zanzibar vijana waliunganishwa na jumuiya za umoja wa vijana wa vyama hivi viwili ambavyo ni TANU YOUTH LEAGUE na ASP YOUTH LEAGUE, zinafahamika kazi zilizofanywa na wabeba mizigo wa Kariakoo mfano Mzee Rajabu Diwani, leo UVCCM sio tena yawabeba mizigo, sio tena ya wamachingasio tena ya wakulima ,sio tena jumuiya ya wafanyakazi ni jumuiya ya wafanyabiashara, watoto wa vigogo ama wenyenasaba nao ama rafiki zao, inahitaji viongozi wenye dhamira ya dhati ambao watarudisha jumuiya hii kwa vijana wakitanzania na kurudisha taswira ya kimapambano ambayo ni mapambano ya kiuchumi, kazi ya Uhuru imeshafanyika imebakia jukumu la kuleta Uhuru wa kiuchumi na kuwa kimbilio la vijana wote.

Ni dhamirayangu ya kugombea nafasi hii ni kuhakikisha awamu ya pili ya mapambano ya kiuchumi ya umoja wa vijana inaanza rasmi. Nafahamu zipo changamoto za kiutawala, kiuchumi na jumuiya kuendelea kuishi kwa kutegemea misaada na Ruzuku kutoka kwenye chama, nafahamu watendajiwana hali mbaya kiuchumi hasa katika mawilaya, nafahamu ofisi zetu za wilaya zina upungufu wa vitendea kazi ni dhamira yangu kubadili mwelekeo wa utendajiwa jumuiya yetu kutoka “Business as usual” kuvalisha skafu viongozi na kuimba nyimbo, kuwa jumuiya yenye dira namwelekeo sahihi wa kuwaunganisha na kumkomboa kijana wa kitanzania.

Ndugu waandishi wa Habari; Ninafahamu matarajio yavijana wa kitanzania yatafikiwa kupitia CCM imara na CCM inatokana na uimara wajumuiya zake kuwa imara na hili inawezekana kwa kupatikana viongozi Imara na mimi nina amini ni mmoja waviongozi ambao wataifanya jumuiya yetu kuwa Imara.

Kwa kuhitimisha Hotuba yangu naomba kutoa shukrani zangu kwa Mwenyezi Mungu kwa kunifanikisha kuwananyi hapa, niwashukuru wana familia yangu, marafiki na nyie ndugu zanguwaandishi wa Habari kwa kukubali kujumuika nami kunisikiliza leo. Niwaombe Vijana wenzangu wa CCM kuniunga mkono katika azma hii kubwa niliyo nayo na niwakumbushe tu kuwa, zoezi hili la kuchukua fomu nililofanya hapa leo si langu bali la vijana wote wa Tanzania wakiwakilishwa na Vijana wa Chama cha Mapinduzi.

Ni imani yangu kuwa, wana UVCCM hawatakubali kuangusha taa hiiwaliyoiwasha kule Rorya mkoa wa Mara wao wenyewe na badala yake wataungana namibega kwa bega ili kuufikia ushindi. Tutapitisha fomu hii pamoja nao, tutachujwa pamoja nao na kisha tutashinda pamoja nao na kisha kuanza kuwaongoza vijana wa Tanzania pamoja nao. Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehma atubariki na kutupa nguvutufanikishe azma hii muhimu pamoja. Kidumu Chama cha Mapinduzi

Asanteni kwa kunisikiliza.

Mimi Ndg Sango Gungu Kasera- Mjumbe Mkutano Mkuu UVCCM (W) Rorya

Kauli mbiu
MbiuVijana kwanza kwa taifa lenye amani namaendeleo’’.

Popular Posts