Mhe.   Gaudentia Mugosi Kabaka ( MB)  Waziri wa Kazi na Ajira  akizungumza   wakati wa mkutano wa  Umoja wa Mataifa unaojadilini pamoja na mambo   mengine tatizo la ajira na hasa kwa vijana, Mhe. Kabaka anaongoza ujumbe   wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkutano huu wa wiki moja,   ukiwashirikisha  mawaziri wanaohusika na masuala ya ajira, fedha na   uchumi, mambo ya nje ,   ILO na wanazuoni.  katika mchango wake kuhusu   changamoto hiyo ya  ukosefu wa ajira, Mhe. Waziri Gaudentia Kabaka   anasema kama ilivyo kwa nchi nyingine zinazoendelea. Tanzania pia   inakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa ajira na kwamba serikali   imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kujaribu kulikabili tatizo hilo   ambalo limekuwa ni changamoto kubwa kwa mataifa tajiri na  maskini pia   na ni bomu ambalo limeshaanza kufuka moshi.
  Baadhi   ya ujumbe wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano huu   unaojadili tatizo la ajira, ni  mkutano ambao umeandaliwa na Baraza la   Umoja wa Mataifa  linalohusika na masuala ya Uchumi na Maendeleo ya   Jamii maarufu kama   ECOSOC.  Walio kaa mbele ni  Kamishna. Ahmed Makame   Haji,  kutoka Tume ya  Mipango  Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bw.   Omar Hamisi Same kutoka Wizara ya Kazi na Ajira,  Bi. Aziza J. Ali, Mkuu   wa kitengo kinachoratibu misaada,  Idara ya Fedha za Nje, Serikali ya    Mapinduzi Zanziba na  Bw. Humphrey Shangarai, mchumi kutoka Idara ya   Sera na Mipango, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa  Kimataifa.
  --
   Na Mwandish Maalum
  Wakati   Jumuia ya kimataifa ikiendelea kukuna vichwa kutafuta mbinu na  mikakati  ya  kukabiliana na  hatari inayotokana  na  ongekezo kubwa la  ukosefu  wa ajira  na hususani kwa Vijana. Tanzania  inasema kwa  kutambua ukubwa  wa tatizo hilo imeanza kuandaa mikakati endelevu ya  kulikabili janga  hilo.
  Akizungunza   katika siku ya pili ya  mkutano  unaowakutanisha kwa pamoja mawaziri   wanaohusika na masuala ya ajira, wataalamu wa masuala ya fedha , uchumi   na  wanazuoni. Waziri wa   Kazi na Ajira, Mhe. Gaudentia Mugosi Kabaka (   Mb) anasema Tanzania  kama ilivyo kwa nchi  nyingine zinazoendelea   inakabiliwa na tatizo kubwa la ukosefu wa ajira.
  Mhe.   Waziri Kabaka anaongoza  ujumbe wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania   katika mkutano wa wiki moja unaofanyika hapa Makao Makuu ya Umoja wa   Mataifa. Mkutano huo ambao umefunguliwa na  Katibu Mkuu wa Umoja wa   Mataifa, Ban Ki  Moon mwanzoni mwa wiki,   umeandaliwa na  Baraza la   Umoja wa Mataifa linalohusika na  masuala ya  Uchumi na Maendeleo ya   Jamii (ECOSOC).
  “Kama   ilivyo kwa nchi nyingine  zinazo endelea duniani, nchi yangu pia   inakabiliwa na tatizo kubwa la ukosefu wa ajira  na hasa kwa vijana. Na    tatizo hili linasababishwa kwa kiasi kubwa na uboreshaji wa elimu  yetu   hadi ngazi ya elimu ya juu, uboreshani na upanuzi ambazo  hauendani  sambamba na  ongezeko la ajira”.
  Amewaeleza   wajumbe wamkutano huo kwamba, tatizo la ajira pia  lipo zaidi kwa   upande wa mijini na hii ni kutoka na wimbi la vijana kuhamia mijini. 
  “   licha ya kwamba vijana wengi wanahamia  mijini na hivyo kuchangia   katika ukosefu wa ajira, lakini pia hivi sasa tunashuhudia vijana wale   wa vijijini kukoa ajira kutokana na athali za mabadiliko ya tabia nchi ,   mabadiliko ambayo  yamekuwa na athari kubwa kwa upande wa kilimo”   akabainisha  Kabaka.
  Akaitaja   baadhi ya mikakati inayofanywa na serikali ya kukabiliana na tatizo la   ukosefu wa ajira kwa vijana, kuwa  ni pamoja na  mpango wa  kurasimisha   mali za wanyonge ( Mkurabita) ili mali hizo ziweze  kutumika kupata  mikopo, upanuzi vya  vyuo vya ufundi stadi ili vijana  waweze kujiajiri  wenyewe, na  kuanzishwa pamona na mambo mengine   sheria ya   hifadhi ya  jamii, mifuko ya  jamii, mifuko ya bima ya  afya,  na vyama vya    ushirika vya kuweka na  kukopa ( SACCOS)
  Aidha   akasema, serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali  ziwamo taasisi   za  kitaifa na kimataifa, imekuwa ikiratibu mafunzo mbalimbali  yakiwamo  ya uwezeshaji katika eneo la kilimo ili vijana wawe kujiajiri  katika  eneo hilo na kwamba mipango yote inalenga katika kufanikisha  utekelezaji  wa malengo ya maendeleo ya millennia.
  Aidha   akasema, Tanzania pia inaendelea na jukumu la kuhakikisha kwamba   ajira  kwa watoto inakomeshwa, kuwapo kwa ajira zenye tija, endelevu na  zenye  hadhi na kwa sababu hiyo akauomba Umoja wa Mataifa kupitia   ECOSOC,  kuisaidia Tanzania  katika eneo la  teknolojia.
  Mada   kuu ya mkutano huu  ni kukuza uwezo wa uzalishaji wa ajira kwa vijana,   na kazi zenye heshima kwa lengo la kuondokana na umaskini na kukuza   uchumi endelevu ili kufikira utekelezaji wa MDGs.
  Mkutano   huo unatoa  fursa kwa nchi wanachama wa UMum kujadiliana na   kubadilishana mawazo kuhusu masuala ambayo ni changamoto kubwa kwa   usalama wa dunia. Na  hususani wimbi hilo la ukosefu wa ajira kwa   vijana,  wimbi ambalo limesha onesha kwamba lisipotafutiwa mikakati ya kudumu ni bomu ambalo tayari limeshaanza kufuka moshi.