Pages

Sunday, July 29, 2012

Zoezi la Epiq Bongo Star Search mkoa wa Tanga

Mshiriki wa Shindano la Epiq Bongo Star Search Digna Mbetela kutoka Dodoma akiwa mbele ya majaji wa shindano hilo (hawapo pichani) walipokuwa wakifanya mchujo mkoani Tanga katika Ukumbu wa Club La Casa Chika Julai 28,2012 na mwana dada huyo kujitosa tena kujaribu bahati yake ya kwenda jijini Dar es Salaam.

Mwamko wa washiriki katika shindano la Zantel Epiq Bong Star Search umekuwa kama ulivyotegemewa ambapo zaidi ya washiriki 300 walikuwa wameisha jisajiri kwanza kwa ajiri ya kufanya usaili siku ya leo.

Washiriki wengi walioshindwa kupata nafasi katika mikoa usaili uliopitiawamejitokeza katika mkoa wa Tanga kitu ambacho kimeongeza ushindani kwawashiriki kutokea eneo hili la Tanga.
Washiriki wa EBSS wakiwa nje ya ukumbi wa Club la Casa Chika jijini Tanga tayari kwa kufanya usaili na kupatiwa namba zao kusubiri kuingia kwa majaji.
Mshewa Mussa akiwakilisha tena baada ya kete yake ya awali mkoani Arusha kugonga mwamba na kuamua kutia maguu jijini Tanga kujaribu bahati yake.
Washiriki wa EBSS wakiwa nje ya ukumbi wa Club la Casa Chika jijini Tanga kusubiri kuingia kwa majaji.
Faisal Jafari wa kutoka Tanga nae akisubiri kurusha kete yake kwa majaji.
Mshiriki Hidaya Hanein akiwa katika foleni ya kuingia kwa majaji

Popular Posts