Pages

Sunday, July 29, 2012

UZINDUZI WA YA RAMADHAN CARE & SHARE YA VODACOM MKOANI-TANGA

Mkuu wa Wilaya ya Tanga Bi.Halima Omary Dendego wapili toka kushoto na Mkuu wa Vodacom Foundation Bw.Yessayta Mwakifulefule wakishuhudia wakati Ofisa Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania,Bw.Hassan Saleh,akimkabidhi madafutari mtoto anaeishi kwenye mazingira magumu mkoani Tanga Juma Hassan,wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ramadhan Care & Share iliyozinduliwa mjini humo ikiwa na lengo la kufuturisha watoto yatima zaidi ya 500 sehemu mbalimbali nchini wakati huu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga mjini Bi.Halima Omary Dendego (kushoto)akishuhudia Ofisa Mkuu wa mauzo na usambazaji wa Vodacom Tanzania Bw.Hassan Saleh akimkabidhi madafutari Zainabu Omary ambae ni mtoto anaeishi katika mazingira magumu mkoani Tanga wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ramadhan Care & Share iliyozinduliwa mjini humo ikiwa na lengo la kufuturisha watoto yatima zaidi ya 500 sehemu mbalimbali nchini wakati huu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan,katikati ni Mkuu wa wa Kampeni hiyo inayoendeshwa na Vodacom Foundation Bw.Yessaya Mwakifulefule.
Ofisa Mkuu wa mauzo na usambazaji wa Vodacom Tanzania,Bw.Hassan Saleh akimkabidhi ndoo ya mafuta ya kula mmoja wa watoto wanaoishi katika mazingira magumu mjini Tanga,Aisha Mohamed,wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ramadhan Care & Share 2012 inayolenga kufuturisha watoto yatima zaidi ya 500 sehemu mbalimbali nchini wakati huu wa mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan,anaeshuhudia watatu kutoka kulia ni Mkuu wa Kampeni hiyo inaendeshwa na Vodacom Foundation Bw.Yessaya Mwakifulefule.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga mjini wapili toka kushoto Bi.Halima Omary Dendego akikabidhi mbuzi pamoja na wafanyakazi wa Vodacom Tanzania,kwa watoto yatima wa mkoani humo wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ramadhan Care & Share mjini humo inayolenga kufuturisha watoto yatima zaidi ya 500 sehemu mbalimbali nchini wakati huu wa mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan,Kampeni hiyo inaendeshwa na Vodacom Foundation.
Imam Mkuu wa Masjid ma’amour ya upanga Dar es Salaam Shekh Issa Othman kushoto akisalimiana na Meneja Mahusiano wa Vodacom Tanzania Bw. Matina Nkurlu, wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ramadhan Care & Share iliyozinduliwa mkoani Tanga,ikiwa na lengo la kufuturisha watoto zaidi ya 500 sehemu mbalimbali nchini wakati huu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan,katikati ni Mkuu wa Vodacom Foundation Bw.Yessaya Mwakifulefule.
Mapokezi
Mkuu wa Vodacom Foundation Bw.Yessaya Mwakifulefule na Meneja Mahusiano wa Vodacom Tanzania Bw.Matina Nkurlu wakiwahudumia watoto wanaoishi katika mazingira magumu mkoani Tanga wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Ramadhan Care & Share iliyozinduliwa mkoani humo ikiwa na lengo la kufuturisha watoto zaidi ya 500 sehemu mbalimbali nchini wakati huu wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga akiwa kwenye uzinduzi huyo…

Popular Posts