Pages

Sunday, November 11, 2012

TFF YATEUA 10 KUSIMAMIA TIMU YA TAIFA YA VIJANA U17


SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania limeteua wadau 10 kwa ajili ya kusaidia timu ya taifa ya vijana walio na umri chini ya miaka 17, Serengeti Boys itakayopambana na Congo (Brazaville) katika mechi ya raundi ya tatu ya michuano ya awali ya Mataifa ya Afrika.

Uteuzi huo umefanywa na Rais wa TFF, Leodegar Tenga baada ya Kamati ya Vijana ya TFF kufanya kikao chake kujadili kwa umakini ushiriki wa timu hiyo na kupeleka mapendekezo yake kwa rais huyo wa shirikisho.
Kutokana na umuhimu wa mechi hiyo itakayoamua timu itakayofuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika, TFF imeona umuhimu wa kuwa na kamati ambayo itakuwa na majukumu mawili makubwa ambayo ni:
1.       Kuhamasisha vijana waone umuhimu na kuwa na ari ya kushinda mechi hiyo
2.       Kuhamasisha umma uone umuhimu wa mechi hiyo na hivyo kuisaidia iweze kufuzu.
Walioteuliwa kuunda kamati hiyo ni:
1.       Ridhiwani Kikwete                                           Mwenyekiti
2.       Ahmed Seif (Magari)                                      Mjumbe
3.       Nassoro Bin Slum                                             Mjumbe
4.       Henry Tandau                                                    Katibu
5.       Ahmed Mgoyi                                                   Mjumbe
6.       Aboubakar Bakhresa                                      Mjumbe
7.       Angetile Osiah                                                   Mjumbe
8.       Kassim Dewji                                                     Mjumbe
9.       Abdallah Bin Kleb                                             Mjumbe
10.   Salim Said                                                            Mjumbe
Baada ya kuvuka raundi mbili za kwanza bila ya kucheza mechi kutokana na wapinzani wake kujitoa, timu ya Serengeti Boys inahitaji kufanya kila iwezalo kuweza kuiondoa Congo kwenye mashindano hayo na kuweka rekodi ya kufuzu kucheza fainali hizo za Afrika ambazo pia zitatoa wawakilishi wa Afrika kwenye mashindano ya Kombe la Dunia. Mechi za kwanza za raundi ya tatu zitachezwa kati ya Novemba 16 na 18, 2012 na mechi za marudiano zitachezwa kuanzia Novemba 30, 2012 hadi Desemba 2, 2012
 *Kuhusu suala la Azam FC kuwasimamisha wachezaji watatu kwa tuhuma za kuhusika kuhujumu timu, tayari TFF imepokea barua hiyo ya Novemba 8, 2012 na inalishughulikia na kulifuatilia kwa makini.
*TFF inapenda kukipongeza Chama cha Mpira wa Miguu cha Mkoa wa Mwanza kwa kufanya uchaguzi wake kwa amani na kufanikiwa kupata viongozi wapya watakaokuwa chini ya uenyekiti wa Jackson Songora. Rais wa TFF amewapongeza viongozi waliorekjea madarakani na viongozi wapya akieleza magtumaini yake kuwa kamati mpya ya Utendaji ya MRFA itaelekeza nguvu zake katika kuendeleza mikakati iliyokuwepo ya kuinua kiwango cha mpira wa miguu na kubuni mikakati mingine kwenye mkoa huo na Tanzania kwa ujumla ikishirikiana na TFF.
*Ligi Kuu ya Vodacom inatazamiwa kuendelea kesho kwenye viwanja tofauti
1. Simba                               v Toto Africans                                  Uwanja wa Taifa
2. T. Prisons                        v JKT Ruvu                                           Sokoine
3. Kagera Sugar                 v Polisi Moro                                      Kaitaba
4. African Lyon                  v Mtibwa Sugar                                 Azam Complex
5. Oljoro JKT                       v Ruvu Shooting                               Sheikh Amri Abeid
6. Mgambo JKT                 v Azam FC                                           Mkwakwani
Jumapili
1.       Coastal Union    v Young Africans                               Mkwakwani

Popular Posts