Pages

Friday, November 23, 2012

Katibu Mkuu wa CCM,Kanali Mstaafu, Abdulrahman Kinana Aung'uruma Sumbawanga na Kuhudhuria Kikao Cha Shina


Katibu Mkuu wa CCM,Kanali Mstaafu, Abdulrahman Kinana akipokea saluti ya Chipukuizi wa CCM, wakati wa mapokezi yake kwenye Uwanja wa Ndege wa  Sumbawanga mkoani Rukwa, alipowasili mkoani Rukwa, jana, akiwa katika ziara yake ya siku nne kujitambulisha, kukagua na kueleza kwa wananchi utekelezaji wa Ilani ya CCM katika mkoa huo na mikoa ya Mtwara, Geita na Arusha.
Kinana akimsalimia aliyekuwa mbunge wa Sumbawanga mjini Hilary Aeshi, kwenye Uwanja wa Ndege wa  Sumbawanga mkoani Rukwa, jana.
Kinana akimsalimia Mwanasiasa mkongwe, Chrisant Mzindakaya, kwenye Uwanja wa Ndege wa sumbawanga, mkoani Rukwa, jana
Mjumbe wa Shina namba moja la Kisesa mkoani Ruwa,  Simoni Kibona akimsalimia kwa furaha, Kinana alipofika kwenye tawi hilo, jana na kushiriki kikao cha hilo ikiwa ni sehemu ya kuhimiza viongozi kutembelea mashina na matawi ya CCM ili kuimarisha chama.
Wajumbe wa mkutano wa shina namba moja la Kisesa mkoani Rukwa wakimsikiliza Kinana wakati akiwahutubia, aliposhiriki mkutano wao uliofanyika jana.
Kinana akifurahia ngoma ya kina mama wa shina la Isesa, mkoani Rukwa
Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggry Mwanri  akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika jana mjini Sumbawanga
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nape akihutubia  mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika jana mjini Sumbawanga
Katibu wa NEC, Oganaizesheni, Mohamed Seif Khatib akisalimia wananchi wakati wa mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika mjini Sumbawanga mkoani Rukwa.
Wananchi wakiwa na ujumbe wao kwenye bango katika mkutano wa CCM uliofanyika Sumbawanga mjini mkoani Rukwa jana.
Wana-CCM wakiwa na bango la kumpongeza Katibu Mkuu wa CCM, Abdylrahman Kinana, mpongeza Kinana katika mkutano uliofanyika jana Sumbawanga mjini mkoani Rukwa.Picha na Bashir Nkromo-idara ya itikadi na Uenezi-CCM

Popular Posts