Mchezaji
 Millan Mbise kutoka Tanzania ameombewa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa 
(ITC) itakayomwezesha kucheza mpira wa miguu nchini Marekani.
Shirikisho
 la Mpira wa Miguu la Marekani (USSF) limemuombea hati hiyo Mbise kama 
mchezaji wa ridhaa ili ajiunge na timu ya Virginia Youth Soccer.
Klabu
 ya zamani ya Mbise aliyezaliwa Agosti 18, 1994 imetajwa kuwa Super 
Sport FC, na mechi ya mwisho kwenye timu hiyo alicheza Novemba 15 mwaka 
juzi.
Shirikisho
 la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linafanya mawasiliano na pande husika 
kabla ya kutoa hati hiyo kwa mchezaji huyo kama ilivyoombwa na 
shirikisho hilo la Marekani.
**************************************
TWFA YATAKA ORODHA YA WAPIGA KURA
Kamati
 ya Uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) 
chini ya Mwenyekiti wake Ombeni Zavala imewataka wanachama wa TWFA ambao
 ni mikoa ya Tanzania Bara kuwasilisha orodha ya wajumbe wao wa mkutano 
wa uchaguzi.
Wajumbe
 wenye sifa ya kuhudhuria Mkutano wa TWFA ni kutoka vyama vya mikoa 
ambavyo tayari vimefanya uchaguzi. Wajumbe hao ni Mwenyekiti, Katibu na 
Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TWFA.
Mikoa
 ambayo imeshafanya uchaguzi mpaka sasa ni Iringa, Kigoma, Mwanza, Pwani
 na Tanga. Mikoa ambayo bado inahimizwa kufanya uchaguzi, na mwisho wa 
kutuma majina ya wajumbe kwa Mwenyekiti Zavala ni Oktoba 25 mwaka huu.
Mkoa ambao utakuwa haujafanya uchaguzi utakuwa umenyimwa haki ya kushiriki uchaguzi wa TWFA utakaofanyika Novemba 4 mwaka huu.
*****************************************
TASMA WAANZA MCHAKATO WA UCHAGUZI
Chama
 cha Madaktari wa Tiba ya Michezo Tanzania (TASMA) leo (Oktoba 19 mwaka 
huu) kimetangaza kuanza mchakato wa uchaguzi wa chama hicho uliopangwa 
kufanyika Novemba 28 mwaka huu.
Kwa
 mujibu wa Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TASMA, Dk. Francis
 Mchomvu, fomu kwa wanamichezo wanaotaka kugombea uongozi wa chama hicho
 zitaanza kutolewa Oktoba 21 mwaka huu.
Mwisho
 wa kuchukua na kurejesha fomu hizo zinazopatikana ofisi za Shirikisho 
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ni saa 10.00 alasiri ya Oktoba 26 mwaka
 huu. Ada ya fomu kwa nafasi nne za juu ni sh. 200,000 wakati kwa nafasi
 nyingine zilizobaki ni sh. 100,000. Kati ya Oktoba 27-31 mwaka huu 
Kamati ya Uchaguzi ya TASMA itapitia fomu na kutangaza majina ya 
waliojitokeza kuomba uongozi.
Nafasi
 zitakazogombewa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu 
Msaidizi, Mhazini, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF na wajumbe wawili wa 
Kamati ya Utendaji.
Kipindi
 cha pingamizi kwa waombaji ni kuanzia Novemba 1-6 mwaka huu, na 
pingamizi zinatakiwa kuwasilishwa kwa Katibu wa Kamati ya Uchaguzi ya 
TASMA kabla ya saa 10.00 alasiri ya Novemba 6 mwaka huu. Hakuna ada 
kwenye pingamizi.
Pingamizi
 zitajadiliwa na kufanyiwa uamuzi kati ya Novemba 7-9 mwaka huu. Usaili 
utafanyika kati ya Novemba 10-11 mwaka huu ambapo matokeo ya usaili huo 
vilevile yatatangazwa ili kutoa fursa kwa rufani ambazo zinatakiwa 
kukatwa kati ya Novemba 11-13 mwaka huu.
Rufani
 ambazo zinaambatana na ada y ash. 500,000 zinatakiwa kufikishwa kwa 
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kabla ya saa 
10.00 alasiri ya Novemba 13 mwaka huu.