Pages

Tuesday, September 11, 2012

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar balozi Seif Ali Iddi ameiagiza Wizara ya Afya kuandaa mkakati wa kujenga Hospitali kubwa Wilaya ya kati

Msimamizi wa Kituo cha Afya cha Kendwa Nungwi Bwana Viola Franco kutoka Hoteli ya Kimataifa ya Lagema Nungwi inayosimamia Kituo hicho akimkaribisha Balozi SeifAli Iddi wakati alipofanya ziara ya kukitembelea Kituo hicho kipya kuona hudumazinazotolewa
Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Kivunge Dr. Ashura Shaib Mussa akimuelezea majukumu yao Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alipoitembelea Hospitalihiyo iliyopo Wilaya ya Kaskazini A.
Mkurugenzi wa Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja Dr. Jamal Adam akimuelezea Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif changamoto wanazopambana nazo Hospitalini hapo ikiwemo idadi kubwa ya wagonjwa.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar balozi Seif Ali Iddi akiwafariji wazazi Hawa Mashauri na Fatma Mohd waliojifungua katika wodi ya Wazazi ya Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja alipofanya ziara ya awamu ya pili katika taasisi za Wizara ya Afya Zanzibar.
--
Uongozi wa Wizara ya Afya Zanzibar umeagizwa kuandaa Mpango Maalum kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali kubwa ndani ya Wilaya ya Kati itakayosaidia kuipunguzia msongamano mkubwa wa Wagonjwa Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja.
Agizo hilo limetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipokuwa akiendelea na awamu ya pili ya ziara yake ndani yaTaasisi za Wizara ya Afya hapa Zanzibar.
Balozi Seif aliueleza Uongozi wa Wizara hiyo ya Afya kwamba Serikali Kuu itakuwa tayari kuangalia uwezekano wa uwezeshaji wa ujenziwa Hospitali hiyo muhimu kwa Jamii.


“ Tumefikia wakati kulingana na mahitaji ya huduma za Afya kwa wananchi wetu kuwa na Hospitali kubwa katika kila Wilaya na hii kwa kiasi kikubwa itaondosha vurumai isiyo ya lazima katika Hospitali yetu ya Rufaa ya Mnazi Mmoja”. Alisisitiza Balozi Seif.
Balozi Seif alisema katika kukabiliana na changamoto zinazoikabili Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja ameahidi kusaidia Vitanda 10 kwa ajili ya wodi ya Wazazi na Serikali itajitahidi kutafuta mbinu za kutatuta changamoto chengine zilizopo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliwapongezaWatendaji wa Hospitali hiyo kwa utendaji wao wa kazi licha ya mazingira magumu wanayofanyia kazi.
Balozi Seif alishuhudia idadi kubwa ya Wagonjwa wanaopata huduma katika Hospitali hiyo ambapo Mkurugenzi wa Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja Dr. Jamal Adam alieleza kwamba uwezo wa kuhudumia wagonjwa bado ni ule ule tokea miaka ya thamanini wakati idadi ya wagonjwa imeongezeka mara dufu.
Akiitembelea Hospitali ya Wazazi ya Muembe Ladu BaloziSeif alielezwa na Watendaji wa Hospitali hiyo mfumo mpya ulioanzishwa wa makuz iya mtoto kwa yule aliyezaliwa akiwa pungufu wa uzito ujuilikanayo kwa jina la Kangaroo.
Mafunzo hayo tayari yameshaanza kufundishwa kwa Wazazi mbali mbali kwa lengo la kujiweka tayari endapo Mzazi atatokezewa kujifungua Mtoto mpungufu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alikagua utendaji wa wafanyakazi wa Hospitali ya Kivunge ambapo Muuguzi mkuu wa Hospitali hiyo Dr.Ashura Shaib Mussa alishauri kuwepo kwa Kitengo cha Upasuaji ili kuwapunguzia hatari wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo ya ghafla.
Dr. Ashura alisema ipo hatari na inaweza kusababisha kifo kwa mzazi anayehitaji operesheni ya ghafla kwa kumsafirisha katika masafa marefu kupatiwa hudumahiyo.
Akizungumza na Watendaji hao Balozi Seif aliwapongeza Madaktari, Wauguzi pamoja na Wafanyakazi wote wa Hospitali ya Kivunge kwajuhudi zao za kuiwekea mazingira safiHospitali hiyo.
Balozi Seif aliahidi kuipatia Hospitali hiyo Vitanda kumi na kuwataka wajenge utamaduni wa kuvifanyia majaribio Vifaa vipya wanavyopelekewa hata kama itakuwa bado kuvifanyia kazi pamoja na kuyapatia changa moto matatizo yanayowakabili.
“Kama sijajua matatizo na changamoto zilizomo ndani ya Mawiza na Taasisi za Serikali wakati mimi ndie Mtendaji Mkuu wa Serikali nitashindwa kutoa maamuzi au ufafanuzi pale unapohitajika”. Alisema Balozi Seif.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alimalizia ziara yake kwa kukaguwa Hospitali mpya ya Wazazi iliyopo katika Kijiji cha Kendwa ambayo imefadhiliwa na Uongozi wa Hoteli ya Kimataifa ya Lagema. Daktali Mkuu wa Hospitali hiyo iitwayo R.G.F Matenity Clinic Dr. Hawa Kivembele alimueleza Balozi Seif kwamba huduma za Hospitali hiyo ambazo ni bure zilizoanza mapema mwezi huu zimelengwa kwa wanakijiji wa eneo hilo.
Hata hivyo Dr. Hawa alisema mbali ya wanakijiji haolakini pia Hospitali hiyo hutoa huduma ya malipo kwa Wafanyakazi wa Hoteli zotezilizoko katika ukanda huo

Na
Othman Khamis Ame,
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

Popular Posts