Pages

Monday, August 27, 2012

MAONI KUHUSU KATIBA MPYA

Maoni yangu kwa leo kuhusu katiba yetu ijayo.

SUALA LA DINI
Amani yetu tuliyo nayo katika Tanzania inachangiwa kwa kiasi kikubwa na hali ya katiba yetu ya sasa kutamka waziwazi kuwa serikali kuwa haina DINI.KUINGIZA VIPEGERE VYA AINA YEYOTE VINAVYOZUNGUMZIA DINI KINYUME NA ILIVYO SASA ITATULETEA MGOGORO NA MAFARAKANO.

Katiba mpya ibaki kama ilivyo sasa katika suala la dini. nalisema hili baada y...
a kuona machapisho yakishawishi masuala ya dini yaingizwe kwenye katiba mpya ikiwemo sheria mabalimbali za kidini kuingizwa kwenye katiba kwa kutamka wazi kutambuliwa na katiba na ama kuwa na uwakilishi wa dini katika BUNGE, Hali hii isikubalike hata kidogo kwani kwa zaidi ya miaka 50 tangu tumepata uhuru tumeweza kuishi kwa amani kwa vile tu serikali yetu haikujihusisha na dini za watu bali kuwapa uhuru wa kuabudu kila mtu kwa kadri ya imani yake ili mradi havunji sheria.

MUUNGANO
Kumekuwa na manuguniko ya muda mrefu ndani ya muungano wetu ya baadhi ya watu ndani ya muungano kudhani kuwa hawatendewi haki sawa sawa na upande mwingine wa muungano wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Maoni yangu ili kuondoa hali hii, nashauri muungano wetu ufuate mfumo wa USA (Marekani), yaani tuwe na majimbo, jimbo la Tanganyika na la zanzibar then tunakuwa na Rais wa jamhuri wa Muungano wa Tanzania atakayeongoza serikali moja ya pande zote hizi, kwa upande mwingine majimbo haya mawili yaongozwe na magavana. nadhani wataalamu mtakuwa mmenielewa.

BUNGE
Tangu tumepata uhuru tumekuwa tukiambiwa kuwa nchi yet ni ya wakulima na wafanyakazi, kwa kipindi sasa makundi haya yanayozalisha na kutegemewa kuinua uchumi wa nchi hii yamekuwa hayasemewi au haywakilishwi ipasavyo bungeni japo ni makundi makubwa ambayo siyo lazima yafungamane na chama chochote cha siasa.

Maoni yangu tuwe na uwakilishi wa wafanyakazi angalau wawili bungeni watakaochaguliwa na wafanyakazi wenyewe kupitia vyama vyao vya wafanyakazi, ili kupata wakuwasemea na kupunguza MIGOMO NA MIGOGORO ILIYOPO.

NA AARON

Popular Posts