Pages

Thursday, May 31, 2012

MAKAMU WA RAIS DK GHARIB BILAL ALIVYOFUNGA MAFUNZO YA WAKUU WA MIKOA, MAKATIBU TAWALA WA MIKOA NA WAKUU WA WILAYA WA TANZANIA BARA MJINI DODOMA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake wakati akifunga rasmi Mafunzo ya Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wa Tanzania Bara, yaliyomalizika mjini Dodoma jana Mei 30, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (kulia) akiteta jambo na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakati alipofika katika Ukumbi wa Mtakatifu Gaspar mjini Dodoma jana Mei 30, kufunga rasmi Mafunzo ya Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wa Tanzania Bara, yaliyomalizika mjini Dodoma jana.
Baadhi wa Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wa Tanzania Bara, waliohudhuria mafunzo hayo wakimsikiliza kwa makini mgeni rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati akisoma hotuba yake ya kufunga mafunzo hayo jana Mei 30, 2012 mjini Dodoma.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal (kulia) akiteta jambo na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakati akiondoka katika Ukumbi wa Mtakatifu Gaspar mjini Dodoma jana Mei 30, baada ya kufunga rasmi Mafunzo ya Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wa Tanzania Bara, yaliyomalizika mjini Dodoma jana.Picha na Muhidin Sufiani-Ofisi ya Makamu wa Rais

Popular Posts