Pages

Friday, June 1, 2012

KUAHIRISHWA KWA MKUTANO WA MADAKTARI WOTE NCHINI

Kwa Madaktari wote

YAH: KUAHIRISHWA KWA MKUTANO WA MADAKTARI WOTE NCHINI

Chama cha madaktari Tanzania (MAT) na Kamati ya Jumuiya ya Madaktari nchini tunapenda kuwataarifu madaktari wote kuwa ule mkutano wa mrejesho wa mazungumzo ya kamati ya Rais ya kushughulikia mgogoro wa madaktari na serikali uliopangwa kufanyika jumamosi tarehe 2/6/2012 umeahirishwa hadi jumamosi tarehe 9/6/2012.

Hii ni kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo kukamilika kwa taarifa ya kikao cha leo (cha kamati ya rais) (31/05/2012), pia kamati inaendelea kukusanya taarifa muhimu kuhusu msimamo wa mwisho wa serikali katika madai yetu yote ili tuweze kuwa na mrejesho uliokamilika.

Madaktari wote tunaombwa kuhamasishana na kuhudhuria kwa wingi kikao hicho cha tarehe 9/6/2012 kwani kitakuwa kikao muhimu sana kwa mustakabali wa fani yetu, huduma kwa wagonjwa na maisha yetu.

Tunaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza

Dr. Namala P. Mkopi
MAT, President

Popular Posts