Pages

Friday, August 17, 2012

KAMATI MAALUMU YA CCM ZANZIBAR YAKUTANA

Makamu Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu wa Zanzibar, Dkt.Amani Abeid Karume, akiendesha kikao cha kamati maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ya Zanzibar, leo katika ukumbi wa CCMKisiwandui Mjini Zanzibar, (kushoto) ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, pia Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Dkt. Ali Mohamed Shein. Picha na Ramadhan Othman,Ikulu
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,pia Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Dkt. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Viongozi wa CCM, alipowasili katika viwanja vya Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar, kushiriki katika kikao cha siku moja cha Kamati maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ya Zanzibar, kilichofanyika leo.
Wajumbe wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar,wakiwa katika kikao cha siku moja chini ya Mwenyekiti wake, Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais Mstaafu wa Zanzibar Dkt. Amani Abeid Karume,wakiwa katika ukumbi wa CCM Kisiwandui Mjini Zanzibar, leo.

Popular Posts