Pages

Monday, August 13, 2012

MAMBO YA MSINGI YA KUCHANGIA KATIKA KATIBA

MAMBO YA MSINGI KWA WANA WA UFALME KUCHANGIA WAKATI TUME YA KATIBA ITAKAPITA KWENYE ENEO LAKO

  1. Uhuru wa kuabudu dini anayotaka mtu na kubadilisha dini ubaki pale pale kama inavyosomeka katika Ibara ya 19 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977
  2. Katiba isitoe mwanya wowote wa Serikali/Nchi yetu kujiunga na jumuiya yoyote ya kidini. Ibara ya 3 nayosema kuwa nchi yetu haina dini isibadilike tena iheshimiwe sana
  3. Mahakama ya Kadhi pamoja na sheria zake zisiruhusiwe kabisa kuingia katika Katiba ya Nchi yetu kwani hiyo itaisababishia Nchi kuwa na gharama kubwa sana za kugharamia makadhi wote katika nchi hii. Mahakama ya Kadhi iwe nje ya Katiba kama ambavyo imetangazwa na viongozi wetu tayari. Nchi hii haina dini. Ibara ya 3 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Ikumbukwe kuwa katika Katiba yetu hakuna sehemu yeyote ambapo imetaja Askofu, Mchungaji, Padre au Mwinjilisti. Vipi atajwe Kadhi? Endapo Kadhi ataingizwa katika Katiba, basi Ibara ya 26 (1) itakuwa ni mwiba kwa watu wote kwani kifungu hicho kinawataka Watanzania wote kufuata na kutii Katiba na sheria za Jamhuri ya Muungano. Na hivyo wote tutalazimika kumtii Kadhii na sheria zake
  4. Katiba mpya isiruhusu mifumo yote ya kiuchumi kuingiliwa na sheria za Kiislamu. Benki zote ambazo zimeruhusu ubaguzi huo zifutwe au ziache utaratibu huo mfano NBC – Islamic Banking Division, Amana Bank ambayo kwa sasa iko mbioni kuja Mwanza, Peoples Bank of Zanzibar n.k. Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 Ibara ya 9 (g) “…Serikali na vyombo vyake vyote vya umma vitatoa nafasi zilizo sawa kwa raia wote, wake kwa waume, bila ya kujali rangi, kabila, dini au hali ya mtu..”
  5. Ibara ya 18 ya Katiba yetu ya sasa inayohusu Haki ya Uhuru wa Mawazo kwa kila raia isibadilishwe kabisa
  6. Katiba itoe uhuru ulio wazi kwa Wakristo kuendesha shughuli zao za kidini, kiuchumi, na kijamii ndani ya Zanzibar
  7. Chaguzi mbali mbali za kisiasa zisifanyike siku ya Jumapili ili kutoa fursa kwa Waumini wa Kikristo kuabudu. Badala yake chaguzi zifanyike Jumatatu, Jumanne, Jumatano au Alhamisi. Hili liwe jambo la kikatiba
  8. Katiba mpya iweke bayana kuwa kila Waumini wa dini mbali mbali wachinje wanyama au ndege wao kwa mujibu wa imani yao tofauti na ilivyo sasa ambapo machinjio yote yameshikiliwa na Waislamu na hata imedhaniwa kuwa wao ndio wenye haki ya kisheria ya kuchinja. Wakristo tumeagizwa kuchinja katika Jina la Yesu na si vinginevyo
  9. Katiba mpya ipige marufuku uvaaji wa mavazi yanayowakilisha dini katika shule za Serikali na hata katika shule binafsi au za kidini watoto wasiokuwa wa dini hiyo wasilazimishwe kuvaa mavazi ya imani isio ya kwao na pia wasilazimishwe kushiriki mafunzo yasiokuwa ya Imani yao. Katika kila shule wanafunzi wapewe nafasi ya kuwa na vipindi vya imani yao.
  10. Katiba itamke bayana ulinzi wa walemavu wa ngozi (Albino)
  11. Mambo mengine endelea kusikiliza KWA NEEMA FM RADIO 98.2 MHz
  12. Nitumie anuani pepe (email) kwa taarifa na mafundisho zaidi: Tuma kwenye namba 0767 982 111 au tuandikie: kwaneemafmradio@gmail.com

Popular Posts