Pages

Friday, August 17, 2012

Rais wa Zanzibar Dk Ali Shein Afuturisha Mkoa wa Mjini Magharibi

Baadhi ya Wananchi na Waumini wa Dini ya Kiislamu wa Mkoa wa Mjini Magharibi wakianza kufutari kwa kunywa madafu kabla ya kula futari jana walipoalikwa katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza La Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,ikiwa ni kawaida yake kuwaalika Wananchi wa Mkoa huo kila ifikapo mwezi kama huu kwa futari maalum.
Baadhi ya Viongozi na Wananchi Waumini wa Dini ya Kiislamu wa Mkoa wa Mjini Magharibi,wakiwa katika chakula cha Futari katika Mwezi mtukufu wa Ramadhan,iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar
Baadhi ya Wananchi na Waumini wa Dini ya Kiislamu wa Mkoa wa Mjini Magharibi wakiwa katika futari iliyoandaliwa jana ,katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanibar na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza La Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,ikiwa ni kawaida yake kuwaalika Wananchi wa Mkoa huo kila ifikapo mwezi kama huu kwa futari maalum.
Baadhi ya Akina mama wa Mkoa wa Mjini Magharibi wakiwa katika chakula cha Futari,iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,katika viwanja vya Ikulu ya Zanzibar.
Baadhi ya Akina mama wa Mkoa wa Mjini Magharibi wakiwa katika chakula cha Futari,iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,katika viwanja vya Ikulu ya Zanzibar.
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, (wa pili kushoto) akijumuika na akinamamawa wa Mkoa wa Mjini Magharibi katika Chakula cha Futari iliyoandaliwa kwa wananchi hao na Rais wa Zanzibar Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein, katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar, (wengine kulia) Mama Shadiya Karume, Mama Pili Balozi Seif na Waziri wa Muungano Samia Suluhu Hassan, (kushoto).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,(wa pili kulia) akijumuika na wananchi pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Mjini Magharibi katika Futari, aliyowaandalia wananchi hao katika viwanja vya IKulu ya Mjini Zanzibar jana, (kulia) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Abdalla Mwinyi Khamis,Rais Mstaafu wa Zanzibar Dk.Amaan Abeid Karume,(kushoto) na Mufti wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Viongozi na wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi baada ya kufutari nao pamoja jana katika futari aliyowaandalia katika viwanja vya IKulu ya Mjini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein, na Mkewe Mama Mwanamwema Shein, wakisalimiana na Viongozi na Wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi baada ya kumalizika Futari waliyowaandalia katika Viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar.
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mama Mwanamwema Shein, (kulia) akisalimiana na mke wa Rais mstaafu wa Zanzibar Mama Shadya Karume, baada ya Futari iliyoandaliwa kwa wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi na Rais wa Zanzibar Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein, katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar.Picha na Ramadhan Othman, Ikulu-Zanzibar

Popular Posts