Pages

Thursday, September 6, 2012

TBL YATOA MSAADA WA VIFAA VYA SH. MIL. 11 WIKI YA NENDA KWA USALAMA BARABARANI

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Kuruthum Bambe (kushoto) akiwa na Mkaguzi wa Polisi, Zauda Mohamed wakati wa hafla hiyo.
Kamanda Mpinga (kulia) akiteta jambo na msaidizi wake, Kahatano wakati wa hafla hiyo.
Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo (kulia), akimkabidhi Kamanda wa Kikosi cha Polisi cha Usalama Barabarani nchini, Mohammed Mpinga sehemu ya fulana 550, kofia 200 na stika 350 kwa ajili ya maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani katika hafla iliyofanyika, Dar es Salaam jana. Vifaa hivyo vina thamani ya sh. mil. 11.
Kamanda wa Kikosi cha Polisi cha Usalama Barabarani nchini, Mohammed Mpinga, akiangalia moja ya fulana baada ya kukabidhiwa na Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo.
Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo (kulia), akimkabidhi Kamanda wa Kikosi cha Polisi cha Usalama Barabarani nchini, Mohammed Mpinga sehemu ya stika 350 kwa ajili ya maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani katika hafla iliyofanyika, Dar es Salaam jana. TBL pia ilikabidhi fulana 550 na kofia 200 vyote vikiwa na thamani ya sh. mil. 11.
Kamanda Mpinga akionesha stika hizo zenye ujumbe maalumu maadhimisho hayo
Kamanda Mpinga (kushoto), akitoa shukrani kwa TBL. Kutoka kulia ni Ofisa Uhusiano wa TBL, Dorris Malulu na Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa kampuni hiyo, Steve Kilindo.

Popular Posts