Pages

Friday, September 7, 2012

Uzinduzi wa Mpango Wa Mpya Wa Kuboresha Maarifa Ya Utoaji Damu Kwa Wahudumu Wa Afya

Dr mohammed mohammed) Mkurugenzi wa Usimamizi Ubora Huduma kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii akizungumza katika ufunguzi wa mradi unaogharamiwa na serikali ya Marekani.
Dr Margreth Mhando, Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii akiwa na Dr Mohammed Mohammed wakiwa na mfano wa mkoba wenye vifaa vipya vya kutolea damu kwa njia salamabaada ya uzinduzi wa shughuli hiyo mjini Dar Es Salaam.
Sehemu ya washiriki na wakufunzi wa mafunzo ya utoaji damu salama wakisiliza ufunguzi wa kazi inayotarajiwa kupunguza uwezekano wa watoa huduma ya tiba kupata maambukizi kwa njia salama.
--
Na: Hassan Mhelela

Jumla ya watumishi 500 wa sekta ya afya watanufaika na mafunzo ya mbinu mpya za utoaji damu ya wagonjwa kwa njia salam. Mpango huo mpya ni sehemu ya mradi unaosimamiwa na Wizara ya Afya,

kwa kushirikiana na washirika na wafanyakazi wa sekta ya afya nchini Tanzania.


Kazi hiyo inatekelezwa kwa ushirikiano na Mpango Dharura wa Rais wa Marekani kwa Ajili ya Kupunguza Makali ya UKIMWI (PEPFAR) kupitia taasisi ya udhibiti na kuzuia maradhi (Centers for Disease Control and Prevention - CDC) chini ya Wizara ya Afya ya Marekani na kampuni ya BD (Becton, Dickinson and Company).
Vile vile JHPIEGO, mshirika wa kiufundi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ya Tanzania, watashirikiana katika jitihada za kusimamia na kusambaza huduma hizi zilizoongezwa ubora.


Mpango wa Tanzania Initiative for Blood-Drawing Applications (TIBA) , una malengo ya kuboresha huduma za afya na maabira katika vituo vya afya, hasa katika mikoa yenye maambukizi zaidi ya VVU/UKIMWI. Shughuli ya kutoa damu katika mwili wa mgonjwa kupitia mishipa ya damu kwa kutumia sindano ni mojawapo ya njia zinazotumika kwa wingi katika hospitali na zahanati, ingawa njia hii inakabiliwa na hatari nyingi za kiafya.

Utafiti uliofanyika mwaka 2008 katika taasisi za afya 14 ulibaini kulikuwa na asilimia 52.9 ya matukio ya kujichoma kwa sindano na kujimwagia damu ya wagonjwa asilimia 21.7 miongoni mwa wafanyakazi wa sekta ya afya. Jumla ya wafanyakazi wa huduma ya afya 500 watanufaika na mafunzo hayo kote nchini.

Popular Posts