Pages

Sunday, July 8, 2012

Fainali za shindano la Serengeti Fiesta Mc Shujaa 2012


Pichani kulia ni mmoja wa waratibu wa tamasha la Serengeti Mc Shujaaa-Mwanza,Adam Mchomvu akimtangaza mshindi wa shindano la Serengeti Mc Shujaaa,aitwaye Ramastar pichani shoto ndani ya jijini la Mwanza.Shindano hilo limefanyika jioni ya leo kwenye kiota cha maraha cha Clup Lips,Isamilo jijini humo.Katika mchakato wa shindano hilo kulikuwepo na msisimko mkubwa kwa vijana wengi kujitokeza na kushiriki kikamilifu na kuwa ushindani mkubwa,aidha walijitokeza vijana wapatao 56 na hatimaye kupatikana mshindi mmoja ambaye atakwenda Dar kushindana na wengine kutoka mikoa mbalimbali kwenye kilele cha tamasha la Serengeti Fiesta 2012 lililopangwa kufanyika katika viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni.
Fainali ya kumsaka kinara wa Serengeti Fiesta Mc Shujaa 2012 ndani ya jiji la Mwanza,pichani kulia ni Ramastar akimisikiliza kinara mwenzie Ramside akighani katika hatua ya mwisho kabisa.
Adam Mchomvu akiwa na washiriki wawili wa shindano la Mc Shujaa,kulia ni Ramastar na shoto ni Ramside ambao walionesha umahiri na ushindani mkubwa katika suala zima la kughani mbele ya mashabiki kibao (hawapo pichani) waliojitokeza kushuhudia mpambano huo ndani ya Club Lips,Isamilo jijini Mwanza.
Baadhi ya Mashabiki wakifuatilia mchuano mkali wa kumpata Mc Shujaa ndani ya jiji la Mwanza jioni ya leo.
Pichani kulia ni mmoja wa majaji wa shindano la Serengeti Fiesta Mc Shujaa 2012,Prodyuza Duke akizungumza machache kabla ya shindano halijaanza,shoto kwake ni jaji mwingine na pia ni mmoja wa waratibu wa shindano hilo Reuben Ndege a.k.a Ncha Kali akisikiliza kwa makini.
Jaji Reuben Ndege a.k.a Ncha kali akitoa muongozo kwenye shindano hilo .
Adam Nchomvu akisoma majina ya washiriki waliongia kwenye robo fainali ya Serengeti Fiesta Mc Shujaa 2012
Msanii chipukizi Ramastar akionesha umahiri wake wa kughani.
Baba Johniiii nae akishusha mistari yake mbele ya washiriki walioingia robo fainali.
Mmoja wa washiriki aitwaye Pusha akikamua vilivyo mitindo huru.
Majaji wa shindano la Serengeti Fiesta Mc Shujaa 2012 wakiwa makini katika suala zima la kutafuta kinara wa shindano hilo ambalo kwa asilimia kubwa vijana wengi wamevutiwa nalo,kiasi hata kupelekea vijana wengi kujitokeza na kushiriki safi kabisa.Pichani kulia ni Jaji Ncha Kali,Deey-Classic pamoja na Prodyuza Duke.

Popular Posts