Pages

Thursday, July 12, 2012

MKUTANO WA CUF WA JUMAPILI 15/7/2012 WAAHIRISHWA

MKUTANO WA JANGWANI WA JUMAPILI TAREHE 15.07.2012 UMEAHIRISHWA.

Ndugu zangu, ule mkutano uliokuwa ukisubiriwa sana na WAPENZI NA WANACHAMA wa CUF pamoja na WANANCHI KWA UJUMLA umeahirishwa.

Baada ya majadiliano ya muda mrefu kati yetu, kanisa katoliki na mamlaka za ILALA tumekubaliana kuwa wakatoliki waendelee na MKUTANO WAO WA KIMATAIFA WA UPONYAJI ambao utachukua takribani MWEZ...I MZIMA.

Maombi yetu na ya wakatoliki yalifika pamoja Sasa kilichofuata ni kukubaliana na kwa sababu chama chetu hakina makuu tumekubali kuwapisha wenzetu kwa sababu itakuw vigumu wao kukatisha mkutano wao halafu waendelee tena.

Tulitizamia kupata kiwanja kingine lakini utafiti umeonesha UWANJA UNAOWEZA KUHIMILI SHUGHULI YA CUF DSM NI JANGWANI, kwa hiyo tunasubiri wenzetu wamalize kisha tutafanya.

Hivi Sasa tunaendelea na oparesheni mbalimbali na wiki ijayo tutakuwa mkoa wa morogoro kwenye baadhi ya wilaya.

Poleni kwa usumbufu wowote ambao umejitokeza.

Popular Posts