Pages

Tuesday, July 10, 2012

JUU YA UZUSHI UNAOENEZWA NA MH. MWIGULU NCHEMBA JUU YANGU NA CHAMA CHANGU

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI JUU YA UZUSHI UNAOENEZWA NA MH. MWIGULU NCHEMBA JUU YANGU NA CHAMA CHANGU


Ndugu zangu kwanza nachukua nafasi hii kuendelea kumshukuru Mungu kwa afya njema anayoendelea kunijalia mimi na Mke wangu hapa Hospitali ya KCMC. Pia niwashukuru wote walionifariji/wanaoendelea kunifariji katika kipindi chote cha matatizo yaliyotokea.

UTANGULIZI

Itakumbukwa kuwa tarehe 28/05/2012 nilipata mbaya ya gari. Ajali hiyo ilitokea maeneo ya Boma karibu na chuo cha VETA. Watu wa kwanza kufika kwenye Eneo la ajali na kutupa msaada walikuwa ni Askari Polisi waliokuwa Doria karibu na eneo lile na Raia waliofika wa pia walikuwemo MWENYEKITI WA CHADEMA (W) YA HAI pamoja na MWENYEKITI WA BAVICHA (W) YA HAI. Walisaidiana na Polisi kuchukua majeruhi (Mimi nikiwemo) pamoja na marehemu waliofariki pale hadi Hospitalini.

Baada ya kufika hospitalini pia walifika MHE.MEYA WA MANISPAA YA MOSHI (AMBAYE PIA NI DIWANI WA CHADEMA) akiongozana na baadhi ya VIONGOZI WA CHADEMA WA KATA YAKE NA BAADHI YA MAENEO YA MOSHI MJINI.. Baadaye alifika KATIBU WA CHADEMA MKOA WA KILIMANJARO AKIONGOZANA NA BAADHI YA MADIWANI WA CHADEMA WA MOSHI NA ARUSHA na Viongozi wengine ambapo nakumbuka walitokea Wilaya ya Mwanga kwenye Mikutano ya Hadhara. Tulikuwa wote hadi tunapatiwa huduma na majeruhi tukapelekwa Wodini. Siku iliyofuata nilipokea Simu kutoka kwa MHE. FREEMAN MBOWE (MWENYEKITI WA CHADEMA NA KIONGOZI WA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI) akiwa Mtwara kwa shughuli za Chama akinipa Pole kwa yaliyotokea na kunifariji.

Baadaye hali yangu ilipoimarika kidogo tukapanga taratibu za mazishi ya Marehemu Mama yangu Mzazi (R.I.P) na miongoni mwa watu waliohudhuria kwanza ni WANACHAMA WA CHADEMA, MADIWANI WOTE WA CHADEMA ARUSHA, MADIWANI WA MOSHI MJINI NA MOSHI VIJIJINI. Kutoka makao makuu ya CHADEMA waliwakilishwa na Mhe.Rwakatare na Ndg.Anthony Komu (Mkurugenzi wa Fedha na Utawala) Pia walihudhuria Baadhi ya WWABUNGE WA CHADEMA wakieleza sababu za viongozi na wabunge wengine kutokuhudhuria (Na zilikuwa Sababu za Msingi kabisa) kwa sababu hata baadhi ya viongozi wa serikali waliohudhuria walileta salam za wakubwa wao ambao nao walitamani kuhudhuria lakini kutokana na sababu mbali mbali walishindwa!..

Pamoja na hayo, MHAMA JOSEPHINE MUSHUMBUSI (MKE WA MHE.KATIBU MKUU WA CHADEMA) alinitembelea hospitalini akiwa na wajumbe kadhaa... Aliniletea salam za pole kutoka kwa KATIBU WANGU MKUU WA CHAMA. Nilifarijika sana kuona kuwa kiongozi wangu pamoja na kuwepo kwake safarini kikazi lakini bado aliweza kutuma ujumbe kwangu.

Baadaye nilihamishiwa MOI (Muhimbili) kwa ajili ya matibabu Zaidi. Nakumbuka walifika wabunge wengi sana wa CHADEMA lakini kubwa zaidi alifika MHE.FREEMAN MBOWE (MWENYEKITI WA CHADEMA KIONGOZI WA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI).

KANUSHO

Nimekuwa nikisikia kwenye vyombo vya habari kuwa Mwigulu Nchemba (Mb-CCM) Anatangaza kuwa Chama changu kimenitupa na hakina msaada wala Ushirikiano na mimi kwenye Matatizo yaliyojitokeza..

Kwanza: Sijawahi kumwajiri Mwigulu Nchemba kuwa msemaji wangu!.

Pili: Mwigulu Nchemba si mkweli na hajui chochote kuhusu mimi wala CHADEMA.

Tatu: Mwigulu Nchemba anataka nionekane sina shukrani kwa viongozi na Chama changu kwa Umoja na Ushirikiano wanaoendelea kunipatia hata sasa.

Nne: Viongozi wangu wanafuatilia kwa karibu sana matibabu yangu na Mke wangu.

MWISHO:

Naomba Mwigulu aelewe kuwa sitaki malumbano yasiyo na Tija kwangu wala kwa Wananchi wangu Walionichagua. Pia nisingependa kumtaja Marehemu Mama Yangu (R.I.P) kabla hata ya Arobaini. Zaidi ya yote akumbuke kuwa Viongozi na Wabunge wa CHADEMA wana mambo mengi ya kufanya na hawatakuwa tayari tena kujibu uongo na uzushi DHAIFU kama aliouzusha!!.

Ahsanteni Sana,
Mungu aendelee kuwabariki.
Joseph Selasini
(Mb) Rombo-CHADEMA.

via facebook.com/joseph.selasini

Popular Posts