Pages

Tuesday, July 31, 2012

Ziara ya Wataalamu wa Chakula wa Oxfam wafanya Ziara ya Mafunzo Bagamoyo na Kuzindua Shindano la Mama Shujaa wa Chakula 2012

Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuongoza mjadala wa hali halisi ya kilimo na uzalishaji wa chakula Bagamoyo uliofanyika kijiji cha Zinga, Bagamoyo hivi karibuni. Mjadala huu uliratibiwa na Oxfam na kuwahusisha wakulima wanawake kama mpango endelevu wa Oxfam kutambua na kuthamini mchango wa wanawake wakulima kwenye uzalishaji wa chakula.
Mkulima na mshindi wa shindano la Mama Shujaa wa Chakula kutoka Nigeria, Briskila Jerome akiwahamasisha akina mama wenzake wa kijiji cha Zinga wilaya ya Bagamoyo hivi karibuni, kujiunga na shindano la 'Mama Shujaa wa Chakula' kwa upande wa Tanzania. Shindano hili linaratibiwa na Oxfam kutambua na kuthamini mchango wa wanawake wakulima kwenye uzalishaji wa chakula.
Mkulima kutoka kijiji cha Zinga wilaya ya Bagamoyo, Halima Mwinshehe akitoa hoja yake wakati wa mhadhara ulioandaliwa na Oxfam kuzungumzia kilimo na maswala ya lishe uliofanyika kijini hapo mkoani Pwani hivi karibuni. Mhadhara huu ni moja ya mpango endelevu unaoratibiwa na Oxfam kutambua na kuthamini mchango wa wanawake wakulima kwenye uzalishaji wa chakula.
Wakulima wanawake na wataalamu wa chakula kutoka Oxfam wakiangalia zao la muhogo, wakati walipotembelea moja ya mashamba ya wakulima wanawake katika kijiji cha Zinga wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani hivi karibuni. Wataalamu hawa wa chakula walikuwa nchini kwenye ziara ya mafunzo katika maswala ya lishe na mchango wa wakulima wanawake kwenye uzalishaji wa chakula.
Meneja Kampeni wa Oxfam, David Moriarty (kulia), akigawa fomu za kushiriki shindano la 'Mama Shujaa wa Chakula' kwa kina mama wa kijiji cha Zinga wilaya ya Bagamoyo hivi karibuni mara baada ya kuzindua shindano hilo. Shindano la 'Mama Shujaa wa Chakula' linaratibiwa na Oxfam kutambuwa na kuthamini mchango wa wanawake wakulima kwenye uzalishaji wa chakula.
Wakulima wanawake kutoka vikundi mbalimbali katika kijiji cha Zinga wilaya ya Bagamoyo wakipata futari baada ya kumalizika kwa mjadala wa hali halisi ya kilimo na uzalishaji wa chakula wilayani humo. Mjadala huu uliratibiwa na Oxfam na kuwahusisha wakulima wanawake kama mpango endelevu wa Oxfam kutambua na kuthamini mchango wa wanawake wakulima kwenye uzalishaji wa chakula.Picha Zote na Mdau Badi John

Popular Posts