Pages

Saturday, August 4, 2012

TAMKO LA KITAALUMA KWA UMMA KUHUSU SERIKALI KULIFUNGIA GAZETI LA MWANAHALISI KWA MUDA USIOJULIKANA

THE PRESIDENT,
P.O.BOX 7447,
Dar es Salaam.
Tel/Fax 255-222 760737

Mob:+255-764450000/719-222448

+255-786450000.
2 Augosti 2012


YAH: TAMKO LA KITAALUMA KWA UMMA KUHUSU SERIKALI KULIFUNGIA GAZETI LA MWANAHALISI KWA MUDA USIOJULIKANA:

NB: Kuandika habari bila ATTRIBUTION(kumtaja source WAKO) na kushindwa ku-BALANCE Habari yako kwa MTUHUMIWA katika HABARI unayoandika ni ukandamizaji wa uhuru wa vyombo vya habari na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu –MCQUAIL (2005).


Kwa sababu hiyo ya MAADILI ya fani yetu,TAJA inalaani kwa nguvu zake zote gazeti la MWANAHALISI na SERIKALI kwa kuwa VIRANJA wa KUBINYA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI kwani hawa wawili ( MWANAHALISI NA SERIKALI) ni MAADUI HATARI wa maendeleo ya TASNIA YA HABARI na HADHI YA Waandishi wa Habari wasomi na makini hapa Nchini.


Aidha tunashangazwa sana na wale wote wanaoilaumu serikali kwa madai ya kwamba inakandamiza uhuru wa habari na kutetea Gazeti la mwanahalisi eti wanadai linatumia uhuru wa habari kama unavyoelezwa katika katiba. TAJA tunaelewa watu hao wote wakiwemo wanaodaiwa kuwa NGULI wa tasnia ya habari ni watu ambao elimu yao ya TAALIMU YA HABARI INA MASHAKA au ni ndogo kiasi kwamba hawaelewi maana ya uhuru wa vyombo vya habari kitaaluma duniani kote MAANA YAKE.


Duniani kote wasomi wa tasnia ya habari wanajua vigezo vya kuwepo uhuru wa habari misingi yake mikuu (1) Uandishi wa habari kwa kuzingatia misingi ya fani ya uandishi wa habari (Journalistic genre ethics) ambapo habari yoyote ni lazima iwe na ATTRIBUTION na pili BALANCE isipokuwa inaruhusiwa kuandika bila kutaja jina kama kwa kufanya hivyo utahatarisha usalama wa mtoa habari (source). MWANAHALISI ni MAHIRI katika kuandika habari za upande mmoja (UNBALANCED STORIES) na zinazohusu tukio moja tu. MWANAHALISI kwa kutozingatia maadili ya uandishi wa habari ni mvunjifu mkubwa wa uhuru wa habari hapa nchini na anadhalilisha fani ya UANDISHI WA HABARI NA WANAHABARI WENGINE MAHIRI (WATCHDOGS). TAJA Tuna wasiwasi na wale wote wanaounga mkono uandishi wa habari za MWANAHALISI zisizo attribution NA Balance.

MWANAHALISI ukiwapa ushauri wa kitaaluma wepesi kuitikia lakini HAWATEKELEZI- Rais wa TAJA amewahi kuzungumza na Mhariri, ameishia kuitikia kimaelewano lakini hakuna hatua aliyoichukua “kitaaluma” katika ku-BALANCE habari za upande mmoja wanazolalamikiwa.,Hivyo TAJA hatutafuni maneno na wala hatuoni haya kwamba wao ni WADHALILISHAJI WAKUBWA wa waandishi wa habari makini hapa Nchini na ni WAVUNJAJI WAKUBWA WA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI HAPA TANZANIA.Wanaowatetea yawezekana wana AGENDA zao nyingine sio ukiukwaji wa uhuru wa vyombo vya habari.

UHURU WA VYOMBO VYA HABARI si ufunguo wa kuandika habari zisizozingatia maadili na weledi wa uandishi wa habari. TAJA inawaomba wale wote wanaotoa mchango kuhusu jambo hili wajiridhishe kwanza na kuijua fani hii wasivyamie tu kama wanavyofanya ndugu zetu wa fani ya sheria eti wapeleke kesi mahakamani(mbona waao mawakili wakivunja maadili ya uwakili hawawapeleki Mahakamani ila wanawafukuza?),sisi tunawauliza kesi gani wakati MWANAHALISI habari zake hazizingatii maadili GAZETI hili pia ni mkosaji kama serikali yenye sheria KANDAMIZI. Hawa wawili hawana tofauti wanalaumiana kwa makosa ambayo wote wanayafanya-wakandamizaji wa uhuru wa habari Tanzania kila mmoja kwa aina yake-hakuna wa KUTETEWA katika MGOGORO HUU.

SERIKALI nayo TUNAILAANI kwa nguvu zetu zote, kwani yenyewe inaongoza kwa ubinyaji UHURU WA HABARI hapa Nchini, ingawa washabiki wa MWANAHALISI wanalalamikia sheria moja tu ya MAGAZETI YA MWAKA 1976 NO 3. Ukweli ni kwamba hiyo inaoonyesha ufinyu wao katika kuelewa ukandamizaji wa Serikali kwa Uhuru wa Habari. HAPA NCHINI.

SERIKALI YA TANZANIA ni kandamizi sana ina zaidi ya sheria 20 ZINAZOBINYA UHURU WA HABARI NCHIN I, aidha hata ukiifuta hiyo sheria ya mwaka 1976 ukaacha mlolongo nilioutaja bado hujatatua tatizo la ukosefu wa uhuru wa vyombo vya habari Nchini. UTATUZI ni kuandikwa sheria mpya ya upatikanaji habari na kufuta zote kandamizi zilizopo,lakini SIO KUTETEA UANDISHI HOLELA WA AINA YA MWANAHALISI USIOZINGATIA JOURNALISTIC GENRE ETHICS.

TAJA tunasema wasiokuwa wasomi katika fani hii wasidandie HOJA HII NYETI yahitaji wasomi wa fani hii ambao kwa sasa tupo na tumemaliza Vyuo vikuu sio mazoea eti mtu akiwa mwandishi wa miaka mingi NGULI –mawazo hayo yamepitwa na wakati-TUSOME TUELEWE VYEMA MAANA YA UHURU WA HABARI ILI TUELEWEKE DUNIANI SIO KUTETEA WAVUNJA MAADILI YA FANI YETU-“TUNAJIAIBISHA WENYEWE MBELE YA WENYE WELEDI KAMA VILE JIRANI ZETU KENYA”

TAJA TUNAWAOMBA SERIKALI AMBAO NI WAONGOZAJI KATIKA UBINYAJI WA UHURU WA HABARI WAFANYE HIMA KUPITISHA SHERIA YA UHURU WA HABARI NA SHERIA HIYO LAZIMA IWE NA KIPENGELE CHA KUFUNGIA CHOMBO CHOCHOTE CHA HABARI KISICHOZINGATIA MAADILI YA UA NDISHI WA HABARI

Tunazungumza kisomi na tunaomba tueleweke,TAJA haiungi mkono sheria ya magazeti ya mwaka 1976,lakini kitendo cha kufungia gazeti lolote lisilozingatia maadili ya uandishi wa habari hata baada ya kupewa ushauri TAJA TUNAKIUNGA MKONO ili kuweka heshima ya fani yetu,isiendelee kuchezewa kama kichwa cha MWENDAWAZIMU.

1). Tunaomba serikali IUNDE jopo la wasomi wa fani ya habari kutoka CHUO Kikuu HURIA, UDSM, SAUT na TUMAINI Iringa tukae na hao wanaotetea MWANAHALISI NA kulaumu SERIKALI peke yake ili UMMA ueleweshwe jambo hili linavyopotoshwa na wanaojiita NGULI wa habari, matatizo ya tasnia ya Habari Nchini imevamiwa na watu wasio Wataalamu wa Fani hii na wengine hawana hata Diploma tu za fani ya Uandishi wa habari au Mawasiliano ya UMMA lakini wamejipa majina ya NGULI (expert- kawaida mtu expert anategemewa kuwa angalau na M.A kama si PhD na kadhalika kwani tulio nao hawana hata Diploma zinazotambulika katika fani),ndio wanatupa taabu katika kuharibuTasnia hii Nchini kwa kujifanya kwamba wanafahamu sana UHURU WA VYOMBO VYA HABARI,KUMBE WANACHOFAHAMU NI KINYUME.

2) Tunaomba wale wote wanaojitokeza na kujitambulisha kuifahamu fani ya habari na dhana ya uhuru wa habari wasiwe wanazungumza kiholela hii ni fani yenye wasomi, hivyo pia watutajie C.V zao ili tujiridhishe na maoni yao tujue ya kitaalamu au ya aina ya kijiweni?

“MWANAHABARI MSOMI HAWEZI HATA KIDOGO KUTETEA “UNETHICAL WRITTEN NEWS PAPER”


TAJA TUNARUDIA KULAANI WOTE, MWANAHALISI NA SERIKALI KWA MATENDO YAO YA UKANDAMIZAJI MKUBWA WA UHURU WA KUPATA HABARI NA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI TANZANIA.


NI MATEGEMEO YA TAJA KWAMBA,MAADUI HAWA WAWILI WALIOJITAMB ULISHA WAZI WAZI WATAJIREKEBISHA KWA SERIKALI KUPELEKA SHERIA YA UHURU WA VYOMBO YA HABARI BUNGENI NA KUANCHANA NA AHADI ZISIZOTEKELEZEKA(HEWA) KILA MWAKA NA MWANAHALISI NAO WAJIENDELEZE KITAALUMA ILI WAJUE DUNIANI HAKUNA POPOTE KWENYE UHURU WA HABARI USIO MIPAKA.
MWISHO. TAJA tunampongeza Mhe. Saed Kubenea Mkurugenzi wa MWANAHALISI, kwa kuongeza elimu yake Nje na kurudi nchini.Tunamshauri atumie elimu hiyo aliyoipata kuweka heshima ya TASNIA yetu badala ya kuidhalilisha kwa kuandika habari zisizo, ATTRIBUTIO, BALANCE,TRUTH –Sisi tunadhani anaweza kulisaidia gazeti lake ambalo KITAALUMA kwa sasa linajitambilisha kwa pwaya halizingatii MAADILI .
(YEYOTE YULE MWENYE HOJA NASI TUNAYOSEMA AITE JOPO TUYACHAMBUE KISOMI KWA FAIDA YA WATANZANIA)


HAMZA KONDO

RAIS CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI TANZANIA (TAJA)

MWANACHUO WA SHAHADA YA UZAMIVU MAWASILIANO YA UMMA(PhD in Mass Communication) OUT.-mwaka wa tatu.
Mob: 0786450000.

CC-Mitandao ya Jamii na vyuo vikuu.

Popular Posts