Pages

Sunday, July 29, 2012

YANGA YA TANZANIA NDIO BINGWA WA KOMBE LA KAGAME 2012

Wachezaji wa Yanga ya Jijini Dar es Salaam, wakishangilia ubingwa wao wakiwa na Kombe la Kagame baada ya kukabidhiwa rasmi walipoibanjua timu ya Azam Fc kwa mabao 2-0, katika mchezo wa Fainali uliozikutanisha timu hizo katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa leo jioni.
*****************************

TIMU ya Yanga ya jijini ya Dar es Salaam, leo imewadhihirishia mashabiki wa soka kwa kutetea ubingwa wake na kutwaa Kombe la Klabu Bingwa ya soka Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame 2012,katika mchezo wa Fainali za Kombe hilo dhidi yake na timu ya wauza Lambalamba Azam Fc, na kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika Uwanja wa Taifa.

Yanga sasa imebakiza mara moja kufikisha idadi sawa na wapinzani wao wa jadi, Simba kutwaa Kombe hilo, mara tano kwa sita. Yanga ilibeba taji hilo 1975, 1993, 1999, 2011 na 2012.

Mabao ya Yanga yalifungwa na Hamisi Kiiza aliyefunga bao la kwanza katika dakika ya 44 na Said Bahanuzi aliyefunga la pili dakika ya 90+ katika dakika tatu za nyongeza.

Kiiza alifunga bao lake, baada ya kuuwahi mpira uliookolewa na kipa Deo Munishi ‘Dida’ na kumpiga chenga kipa huyo kisha kuusukuma mpira nyavuni.

Bahanuzi aliuwahi mpira mrefu uliopigwa na beki Oscar Joshua na kuwazidi ujanja mabeki wa Azam kabla ya kumtungua Dida.

Niyonzima, akichanja Mbuga.
Niyonzima, akimtoka beki wa Azam kwa spidi ya ajab na kumimina majalo.
Kipa wa Azm, Dida, akiokoa moha ya hatari langoni kwake.
Niyonzima, akiendelea kuwatesa mabeki wa Azam.
Beki wa Azam, Mouris akimdhibiti mshambuliaji wa Yanga, Said Bahanuzi na kumpa nafasi kipa wake Dida kudaka mpira huo.
Mashabiki wa Azam waliochanganyika na wa Simba, wakiwa wamebeba Jeneza kuwakejeli mashabiki wa Yanga, kabla ya kuanza kwa mchezo huo.lakini hadi mwisho wa mchezo huo Jeneza hilo halikujulikana lilikopitia.
Katika mchezo uliotangulia wa kusaka mshindi wa tatu, AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) iliifunga APR ya Rwanda mabao 2-1, mabao ya As Vita yakifungwa na Magola Mapanda dakika ya 18 na Mutombo Kazadi, dakika ya 67, wakati la kufutia machozi la timu ya APR ya Rwanda, lilifungwa na Jean Mugiraneza dakika ya 89 na kufanya mshindi wa tatu katika michuano hiyo kuwa ni AS Vita.
Mashabiki wa Yanga, wakishangilia bao la kwanza.
Wachezaji wa Yanga wakishangilia na Kombe lao.
Kasuku nao walikuwapo kushuhudia mtanange huo huku wakiwa na rangi ya Yanga na Bendera ya Yanga.
Mashabiki wa Azam wakiwa Tuliiiiii, wakiwa kama wamemwagiwa maji baada ya timu yao kupokea kichapo kitakatifu jioni ya leo.
Said Bahanuz, akishangilia mbele ya mashabiki wake baada ya mchezo huo kumalizika.
Mashabiki wa Yanga....... Ebwana eeeeh!!!! ushindi mtamu bwanaaaaaa!!!!
Bahanuzi kama Kawa.......
Mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Manji akipita katikati ya Uwanja kuwapongeza wachezaji wake baada ya mchezo huo kumalizika.
Niyonzima (kushoto) akimfariji Ngasa, baada ya mchezo huo.

2012 CECAFA KAGAME CLUB CUP
Dar es Salaam, July 14-28
(Yellow cards after end of preliminary round)
2:
20. Derrick Walulya (Suspended Match No. 12)
4. Yusuf Makame Juma [Mafunzo]
5. Kadar Abaneh [AS Port]
1:
2. Edward Simon Jovan [El Salaam, Wau]
28. Maxime Sekamana [APR ]
11. Emery Ndikumana [Atletico Olympique]
7. Didier Kavumbagu [Atletico Olympique]
17. Amir Maftah [Simba]
15. Allan Munabu [URA]
21. Ahmed Mohdi [AS Port]
5. Ismail Khamis [Mafunzo]
25. Johnson Bagoole [APR]
17. Christopher Ndayishimiye [Atletico]
4. Hassan Hakizimana [Atletico]
13. Ismail Musa Juma [El Salaam, Wau]
13. Lema Mubidi [AS Vita]
17. Thiery Kasereka [AS Vita]
16. Vincent Agbor [AS Port]
1. Khalid Moursal [AS Port]
4. Jean Paul Niyibaraba [AS Port]
3. Francis Nongwe [Atletico]
15. Frederick Nsabiyumwa [Atletico]
15. Santino Makuei [El Salaam, Wau]
24. Jerry Santos [Tusker]
18. Said Musa Shaaban [Mafunzo]
14. Sula Bagala [URA]
22. Osman Wejuli [URA]
12. Suleman Ndikumana [APR]
4. Donatien Tuyizere [APR]
18. Joseph Shikokoti [Tusker]
13. Aggrey Morris [Azam]
19. John Bocco [Azam]
TOTAL: 29
QURTER FINALS
2:
21. Issa Mpeko [AS Vita Club] (2) R
4. Ibrahim Mwaipopo [Azam] (2) R
1:
15. Mohamed Abdoulrahman [Mafunzo]
20. Derrick Walulya [URA]
16. Augustine Nsumba [URA]
22. Jean Claude Iranzi [APR]
3. Albert Ngaboyisibo [APR]
16. Nelson Lukong [Vita]
23. Pierre Kwizera [Atletico]
3. Simbi Ebunga [AS Vita Club]
14. Mutombo Kazadi [AS Vita Club]
10. Felix Sunzu [Simba]
6. Erasto Nyoni [Azam]
26. Haruna Shamte [Simba]
25. Jabir Aziz [Azam]
TOTAL (from Quarter final stage only): 17 - Up to Match No. 20 (Yanga v APR semifinal)
OVERALL TOTAL: 36
Gishinga Njoroge
Managing Editor
www.kpl.co.ke
Brookside Grove
Westlands
P.O Box 5350, Nairobi, 00506 Kenya
Office Tel: +254 020 444 20 70
+254 020 444 20 72
email: gishinga@kenyanpremierleague.com
Personal cel phone: +254 722 79 77 49

Popular Posts