Pages

Wednesday, June 27, 2012

SHEREHE ZA MIAKA 35 ZA UHURU WA DJIBOUTI


Pichani juu na chini ni Balozi wa Jamhuri ya Djibouti-Tanzania, Saidi Amin Shamo akiongea machache kwenye hafla fupi ya kutimiza miaka 35,mbele ya wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo mabalozi kutoka sehemu mbalimbali,hafla hiyo imefanyika jioni ya jana nyumbani kwa balozi huyo,jijini Dar.
Sehemu ya baadhi ya wageni waalikwa wakisikiliza hotuba fupi iliyokuwa ikitolewa na Balozi wa Jamhuri ya Djibouti, Saidi Amin Shamo,kwenye hafla fupi ya kutimiza miaka 35 ya jamhuri ya Djibout iliyofanyika jioni ya jana jijini Dar.
Wageni waalikwa wakijadiliana jambo,Pichani kati ni Mkurugenzi wa Clouds Media Group,Bw.Joseph Kusaga.
Wageni waalikwa mbalimbali wakiwa wamekusanyika nyumbani kwa Balozi wa Jamhuri ya Djibouti-Tanzania, Saidi Amin Shamo,wakisherehekea hafla fupi ya kutimiza miaka 35 ya jamhuri ya Djibout iliyofanyika jioni ya jana jijini Dar.
Burudani kama hivi ilikuwepo kwa wageni waalikwa waliofika kwenye hafla hiyo.
Balozi wa Jamhuri ya Djibouti-Tanzania, Saidi Amin Shamo akimpokea mgeni rasmi wa hafla hiyo,Rais mstaafu wa awamu ya pili,Mh.Ally Hassan Mwinyi alipokuwa akiwasili nyumbani kwa balozi huyo.
Balozi wa Jamhuri ya Djibouti, Saidi Amin Shamo akimkaribisha Sir Andy Chande (Mtanzania wa kwanza kukiri kuwa Mwanachama wa Freemasons) mara alipokuwa akiwasili kwenye hafla hiyo.
Sir Andy Chande (Mtanzania wa kwanza kukiri kuwa Mwanachama wa Freemasons) akisalimiana na Rais mstaafu wa awamu ya pili,Mh.Ally Hassan Mwinyi jioni ya jana kwenye viunga vya balozi wa Jamhuri ya Djibouti, Saidi Amin Shamo
Balozi wa Jamhuri ya Djibouti-Tanzania, Saidi Amin Shamo akizungumza machache na machache na Rais mstaafu wa awamu ya pili,Mh.Ally Hassan Mwinyi ,shoto ni Sir Andy Chande (Mtanzania wa kwanza kukiri kuwa Mwanachama wa Freemasons)
Balozi wa Jamhuri ya Djibouti-Tanzania, Saidi Amin Shamo sambamba na Mkewe Mariam Shamo wakiwa na mmoja wa wageni wao,Mwamvita Makamba kutoka kampuni ya simu za mikononi ya Vodacom.
Balozi Shamo na Mkewe wakiwa na wageni wao waalikwa waliofika kujumuika nao kwenye hafla hiyo.
Mke wa Balozi,Mariam Shamo (wa nne shoto) akiwa katika picha ya pamoja na wageni waalikwa.
Mkurugenzi wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga akiwa na Mkewe Juhayna Kusaga wakifurahia jambo kwenye hafla hiyo
Rais mstaafu wa awamu ya pili,Mh.Ally Hassan Mwinyi akizungumza jambo na Sir Andy Chande (Mtanzania wa kwanza kukiri kuwa Mwanachama wa Freemasons).
Rais mstaafu wa awamu ya pili,Mh.Ally Hassan Mwinyi akizungumza machache kuhusiana na hafla hiyo kwa baadhi ya wanahabari waliohudhuria ,shoto ni Sir Andy Chande.

Popular Posts