HALI YA MJADALA WA BUNGE LA BAJETI 
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP, tumekuwa tukifuatilia kwa karibu sana mjadala wa
bajeti ya serikali ya mwaka wa Fedha 2012/2013 katika Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, tumestushwa na kusikitishwa jinsi ambavyo baadhi ya
wabunge wanaonesha  tabia ya kutumia nafasi na dhamana waliopewa na wananchi vibaya, kinyume na matarajio.
Bajeti
ya mwaka 2012/2013 imekuja wakati ambapo wananchi walio wengi wanashuhudia  hali ngumu ya maisha kutokana na mfumko wa
bei, ukosefu wa ajira, ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake, wazee na watoto
na kudorora kwa hduma zote muhimu kwa wananchi ikiwemo , maji, afya, nishati,
elimu na huduma za kijamii hususani kwa walioko pembezoni. Kwa mantiki hii
wananchi wanamategemeo makubwa kwa Bunge na wabunge katika mjadala huo. 
Kinyume
na matarajio hayo, tumesikitishwa na tabia ya baadhi ya wabunge kutumia Bunge
kama sehemu ya malumbano ya kisiasa na kutambiana elimu, vyeti na sifa binafsi
badala ya kujadili na kufanya maamuzi yenye manufaa kwa nchi yetu.
Tumesikia
matumizi ya lugha chafu ndani ya Bunge zikitolewa na baadhi ya wabunge, dharau,
jeuri, na kejeli badala ya kujadili bajeti kwa misingi ya mahitaji ya  wananchi ambao wanateseka kwa ugumu wa maisha. 
TGNP
tunakemea na kukataa matumizi mabaya ya muda  na nafasi adimu waliopewa wabunge kwa gharama kubwa za wananchi kutumika
vibaya, kujadili maisha ya watu binafsi, kushambulia vyama vya siasa, kufanya
utani badala ya kujadili jinsi ya kusaidia na kuboresha maisha ya Watanzania waliowengi. 
Sisi
kama wanaharakati na watetezi wa ukombozi wa wanawake, haki za bindamu,
demokrasia, na usawa wa kijinsia  tunawataka wabunge na ofisi ya Spika kufanya yafuatayo:
        * Kuheshimu kwa dhati muda na gharama za walipa kodi  zinazowafanya wawepo Dodoma, mijadala ilenge kuleta tija, mageuzi ya  kiuchumi na kubadilisha hali duni  na umasikini wa Mtanzania ambaye  amebaki kupata mlo mmoja kwa siku na wengine hawana kabisa. 
        * Wabunge wajikite kuchambua, kujadili bajeti  na kuishauri  serikali namna ya kuboresha na kutekeleza ahadi , mipango yake ya  kiuchumi hasa ule wa Miaka mitano (FYDP),MKUKUTA11, Mpango wa  Maendeleo(Vision 2025), kwa kurejea Hali halisi ya uchumi wa wananchi  kwa sasa iliyosomwa na Waziri wa Nchi (Uhusiano). 
        * Wabunge kuacha mara moja lugha chafu za matusi, kejeli,  dhararu, vurugu na kuchana nyaraka za mijadala Bungeni kwani hiyo ni  kuwatusi wananchi walalahoi, ambao ni wapiga kura. 
        * Spika asiruhusu ushabiki wa  maoni ya mtu binafsi au kikundi  bali  hoja za bajeti ya serikali ambayo inawagusa wananchi  wa Tanzania.  
Kwa
kushirikiana  na wananchi  tutaendelea kufuatilia na kudai
uwajibikaji  wa wabunge na viongozi  wa serikali katika nagzi zote kwa maendeleo
ya Taifa letu. . 
Imetolewa
na:
…………………
Usu Mallya
Mkurugenzi
Mtendaji wa TGNP
                      -