Pages

Saturday, June 30, 2012

UZINDUZI WA KINYWAJI CHA KIBO GOLD WAFANA

Kinywaji cha Kibo Gold kilichopotea kwa wanywaji wake takribani miaka kumi,kimerejeshwa tena kampuni ya bia ya Serengeti.
Meneja wa kinywaji cha bia ya Serengeti,Allan Chonjo akizungumza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo wafanyakazi wa kampuni hiyo wakati wa utambulisho mpya wa kinywaji cha Kibo Gold.Akizungumza na wageni waalikwa na waandishi wa habari waliohudhuria katika uzinduzi huo uliofanyika katika kiwanda cha Serengeti tawi la moshi mkoani Kilimanjaro, Bw.Allan Chonjo amesema kuwa kampuni yao imeamua kukizalisha kinywaji hicho na kukirejesha tena kwa wanywaji wake ambao walikikosa kwa muda wa miaka kumi tangu kilipoachwa kuzalishwa.
Meneja wa Kampuni ya Sbl,tawi la Moshi,Bw.Gerald Mandala akitoa historia fupi kuhusiana na na kinywaji cha Kibo Gold,kwa wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo wanahabari (hawapo pichani),wakati wa utambulisho mpya wa kinywaji hicho uliofanyika kwenye viunga vya kiwanda hicho cha SBL Moshi.kuliwa kwake ni Operesheni Meneja wa Kiwanda,Bi.Alice Kilembe.
Mpishi wa bia ya Kibo Gold,Bw.Julius Nyaki akifafanua jambo kuhusiana na upishi wa kinywaji cha Kibo Gold bia.
Baadhi ya Wafanayakazi wa kampuni ya bia ya SBL wakishangweka vilivyo jioni ya leo na kinywaji chao kipya aina ya Kibo Gold,mara baada ya kukizindua tena kwa wakazi wa mji wa Moshi na kwingineko,mara baada ya kupotea kabisa kabisa katiko soko kwa muda wa miaka kumi.
Sehemu ya wageni waalikwa wa wakiwemo Wanhabari wakishuhudia utambulisho mpya wa kinywaji cha Kigo Gold uliofanyika leo jioni kwenye viunga vya kiwanda hicho,mjini Moshi.
Meneja wa bia ya Serengeti,Bwa.Allan Chonjo akimsikiliza mmoja wa wanyaji wa bia ya Kibo Gold kwa miaka miaka,akitoa ushuhuda wa urejesho mpya wa kinywaji hicho kwa wanywaji wake,ambapo anakiri wazi kuwa waliokuwa wanywaji wa bia hiyo wamefarijika sana kurejeshewa kinywaji chao walichokikosa kwa miaka mingi,takribani miaka kumi mpaka sasa.
Baadhi ya wafanyakazi wa SBL wakifurahi jambo kwa pamoja.
Wafanyakazi,wadau mbalimbali wakiwemo na wahahabari wakiw kwenye moja ya ukumbi wa kampuni ya SBL,mjini Moshi jioni ya leo kushuhudia utambulisho mpya wa kinyaji cha Kibo Gold.
Baadhi ya wadau wa kampuni ya Bia ya SBL,wakiwa kwenye utambulishao mpya wa kinywaji cha Kibo Gold,uliofanyika jioni ya leo kwanye viunga vya kampuni hiyo,mjini Moshi.

Popular Posts