Pages

Monday, August 6, 2012

TAFRIJA YA KUMUAGA MKURUGENZI MTENDAJI WA SBL MJINI MOSHI

Mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda (wapili kushoto) akiwa katika Picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti, Steve Gannon (wapili kulia) na Mkurugenzi aliyemaliza muda wake Richard Wells (kushoto) na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa SBL Teddy Mapunda wakati wa tafrija maalum ya kumuaga Wells, iliyofanyika Kiwanda cha SBL mjini Moshi hivi karibuni.
Mama Tundu Pinda, akipeana mkono na Mkurugenzi Mtendaji wa SBL aliyemaliza muda wake, Richard Wells, wakati wa tafrija ya kumuaga iliyofanyika kiwanda cha SBL mjini Moshio hivi karibuni.
Mama Tunu Pinda, akisalimiana na Mkurugenzi mpya wa SBL, Steven Gannon.
Richard Wells (kushoto) akiwa katika vazi la jadi la jamii ya Wamasai pamoja na Kisu cha sime baada ya kukabidhiwa na Wafanyakazi wa SBL mjini Moshi wakati walipomuaga rasmi baada ya kumaliza muda wake na kumkaribisha Mkurugenzi Mpya Steven Gannon.
Baadhi ya Maofisa wa Kampuni ya Bia Serengeti Mjini Moshi wakipiga picha na viongozi wao.
Mke wa Waziri Mkuu Mama Tunu Pinda (wapili kushoto) akiwa katika Picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti, Steve Gannon (kulia) na Mkurugenzi aliyemaliza muda wake Richard Wells (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Moshi Dkt. Msengi
Mkurugemzi wa Mawasiliano wa SBL, Teddy Mapunda, akitunzwa na Meneja Miradi Endelevu na Uwajibikaji wa SBL, Nandi Mwiyombela, kwa kutoa burudani ya aina yake wakati wa tafrija hiyo ya kumuga Richard Wells.
Vijana wa Kalunde Band wakiwa kazini kutoa burudani.
Hapa kazi tu.....Mkurugenzi wa Mawasiliano wa SBL, Teddy Mapunda, na Mkurugenzi wa Masoko, Ephraim Mafuru, wakiimba wakati wa tafrija hiyo ya kumuaga Richard Wells.
Richard Wells, akicheza muziki na Wafanyakazi wa Kiwanda cha SBL mjini Moshi wakati wa tafrija ya kumuaga.
Mkurugenzi Mtendaji Mpya wa SBL, Steven Gannon, akisakata rumba na wafanyakazi wa SBL Kiwanda cha Moshi.
Wafanyakazi wakiwa wanaendelea na vitu vya hapa na pale wakati wa tafrija hiyo ya kumuaga Mkurugenzi Mtendaji aliyemaliza muda wake, Richard Wells, mjini Moshi.

Popular Posts