Pages

Wednesday, August 8, 2012

TBL YASAIDIA VIJIJI VISIMA VYA MAJI 15 WILAYANI LUDEWA

Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo, akinywa maji kuashiria kuwa ni safi na salama kwa matumizi ya binadamu wakati wa hafla ya kukabidhi mradi wa visima 15 wilayani Ludewa, Mkoa wa Njombe hivi karibuni. Mradi huo umefadhiliwa na TBL.
Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo (kushoto) akimtwisha ndoo ya maji Mkazi wa Ngelenge, Kata ya Manda,wakati wa uzinduzi wa visima 15 vilifadhiwa na TBL, wilayani Ludewa, Mkoa wa Njombe hivi karibuni.
Katibu Tarafa wa Ngelenge, Januari Mwambeleko, akifunua kitambaa ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa visima 15 vilivyojengwa kwa ufadhili wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), katika baadhi ya vijiji wilayani Ludewa, Mkoa mpya wa Njombe. Kulia ni Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa TBL, Steve Kilindo. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni wilayani humo.


Mwambeleko, akipampu amaji kwenye moja ya visima hivyo.
Steve Kindo (wa pili kulia) akiwa na baadhi ya maofisa wa TBL pamoja na viongozi wa vijiji wilayani Ludewa walionufaika na mradi huo.

Popular Posts