Pages

Thursday, July 26, 2012

MIKUTANO YA KUKUSANYA MAONI YA KATIBA - TSEGERA, ANGA, KYERWA, KARAGWE, MISENYI

Wiliam Wilbard Ishengoma, mkazi wa Kata ya Bwanjai, Wilaya ya Misenyi mkoani Kageraakitoa maoni yake kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilipofanya mkutano wake wilayani hapo hivi karibuni.
Mzee Idrisa Omary (70),mkazi wa kijiji cha Michungwani, Kata ya Segera, Wilaya ya Handeni mkoani Tanga akitoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya Mpya katika mkutano wa kukusanya maoni kijijini hapo hivi karibuni.
Abdallah Mohamedi (31) mkazi wa kijiji cha Michungwani, Kata ya Segera, Wilaya ya Handeni mkoani Tanga akitoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya katika mkutano wa kukusanya maoni kijijini hapo hivi karibuni.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Michungwani iliyopo kijiji cha michungwani, Kata ya Segera wilayani Handeni mkoani Tanga wakijisomea kitabu kuhusu Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka1977 katika mkutano kukusanyaji maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya uliofanyika kijijini hapo hivi karibuni.
Bi.Teodezea John, ambaye ni mlemavu, mkazi wa Kata ya Kilimikile, Wilaya ya Misenyi,mkoani Kagera akitoa maoni yake kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilipofanya mkutano wake wilayani hapo. hivi karibuni.
Wananchi wa Kata ya Nkwenda, Wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera wakiwa katika mkutano wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wa kukusanya maoni yao kuhusu KatibaMpya.Picha -Tume ya Mabadiliko ya Katiba (CRC))

Popular Posts