Pages

Friday, July 27, 2012

Rais wa zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein Afungua Msikiti wa Ijumaa Masjid Hudda wa Kiboje Mwembeshauri

Rais wa zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dkt. Ali Mohamed Shein,(wa pili kulia) akikata utepe kama ishara ya kuufungua Msikiti wa Ijumaa Masjid Lhudda wa Kiboje Mwembeshauri,Wilaya ya Kati Unguja leo, (wa kwanza kulia) Mufti wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi. Picha na Ramadhan Othman,ORZ
Rais wa zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dkt.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Mufti wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi,pamoja na viongozi wengine alipowasili katika Msikiti wa Ijumaa Masjid Hudda wa Kiboje Mwembeshauri Wilaya ya Kati Unguja leo kwa ajili ya kuuzindua rasmi msikiti huo.
Miongoni mwa Viongozi waliohudhuria katika hafla ya Ufunguzi wa Msikiti wa Ijumaa Masjid Lhudda,wa Kiboje Mwembeshauri,Wilaya ya Kati Unguja uliofunguliwa na Rais wa zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein leo.
Rais wa zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,akitoa nasaha zake mbele ya waumini wa Dini ya Kiislamu wakati wa sherehe ya ufunguzi wa Msikiti wa Ijumaa Masjid lhudda wa Kiboje Mwembeshauri Wilaya ya Kati Unguja leo.

Baadhi ya waislamu wa Kijiji cha Kiboje Mwembeshauri,pamoja na vitongoji vyake wakimsikiliza Rais wa zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein,alipokuwa akitoa nasaha zake baada ya kuufungua Msikiti wa Ijumaa Masjid Hudda wa Kiboje Mwembeshauri Wilaya ya Kati Unguja leo.

Popular Posts