Pages

Tuesday, July 24, 2012

MRADI WA KUHIFADHI MAZINGIRA WA TWIGA CEMENT WAZINDULIWA

Muasisi wa Taasisi ya Jane Goodall, Dkt Jane Goodall (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Saruji ya Twiga Cement (TPCC), Pascal Lesoinne, wakitembelea kitalu cha miti wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa mradi wa miti wa kukarabati na kuasilisha machimbo ya saruji ya kampuni hiyo uliofanyika Wazo Hill, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya Twiga Cement (TPCC) wakimwangalia mwanaserere sokwe wa Dkt.Jane Goodall, wakati wa uzinduzi rasmi wa mradi huo. Dkt. Jane Goodall ni Bingwa wa Utafiti wa maisha ya Masokwe Duniani.
Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Boko na ambaye pia ni mwanachama wa Roots and Shoots akipanda mti wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi wa mradi wa miti.

Muasisi wa Taasisi ya Jane Goodall, Dk Jane Goodall (wa nne kushoto, waliosimama), Mkurugenzi Mtendaji wa Twiga Cement, Pascal Lesoinne (kushoto kwake) na Meneja Mazingira wa kampuni hiyo, Juliet Mboneko (wa sita kushoto) wakipozi kwa picha na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Twiga Cement katika halfa ya uzinduzi wa mradi huo.

Popular Posts