Pages

Tuesday, July 24, 2012

Prime Time Promotions Ltd Yatoa Rambirambi ya Million Moja Kwa Serikali ya Zanzibar Kufuatia Ajali ya Kuzama Kwa Meli ya MV Skagik

Mratibu wa Coconut Fm Ali Khatib Dai (kushoto) akimkabidhi rambirambi makamu wa pili wa raisi wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kiasi cha shilingi milioni moja (1,000,000/-) ofisini kwake Vuga mapema leo

Meneja wa Coconut Fm Husna Abdul akisalimiana na Makamu wa pili wa Raisi wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ofisini kwake Vuga mjini Zanzibar walipokwenda kukabidhi rambirambi kufuatia ajali ya meli ya MV Skagik.
Makamu wa pili wa Raisi wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akitoa maelezo kwa mratibu wa Coconut Fm Ali Khatib Dai kuhusiana na hali inayoendelea kuhusiana na ajali ya kuzama kwa meli ya MV Skagik Prime Time Promotion kupitia kituo chake cha redio Coconut Fm kimekabidhi rambirambi ya kiasi cha shilingi milioni moja (1,000,000/-) kwa makamu wa pili wa raisi wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kufuatia na kuguswa kwake ajali ya kuzama kwa meli ya MV Skagik.

Popular Posts