Pages

Tuesday, July 3, 2012

Madaktari warejea kazini

Tathimini iliyofanyika kuanzia asubuhi saa mbili hadi saa 11 jioni
inaonyesha kuwa katika Idara ya Tiba, Madaktari Bingwa 19 kati ya 21
wamefika kazini ambapo watatu wako likizo. Aidha Registrars wote 12
walikuja kazini. Kliniki zote za tiba zimefanyika kama kawaida.

Katika Idara ya watoto, yenye Madakatari Bingwa 16, kati yao 14 walikuja
kazini wengine wawili wako likizo na Registrar watatu kati ya sita walikuja
kazini ambapo watatu wako likizo.

Upande wa OPD yenye Registrars saba, sita kati yao walikuja kazini na mmoja
yuko likizo. Aidha Madaktari Bingwa wote walikuja kazini.

Idara ya Magonjwa ya Afya ya Akili yenye Madakatri Bingwa 10, tisa
walikuja kazini na mmoja wao yuko masomoni.

Upande wa Emergency Medicine, Registrars wote 10 walikuja kazini.

Kuhusu huduma za upasuaji, wagonjwa wote waliolazwa wodini wameonwa, na
baadhi ya kliniki za huduma ya upasuaji zilifanyika. Hata hivyo, upasuaji
haukufanyika kwani hakukuwa na orodha ya wagonjwa waliopangwa kufanyiwa
upasuaji..

KWA UJUMLA, MADAKTARI WAMEREJEA KAZINI.

Imetolewa na;

Aminiel Buberwa Aligaesha
Afisa Uhusiano Mwandamizi
Julai 2, 2012

Popular Posts