Pages

Thursday, July 5, 2012

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR BALOZI SEIF ALLY IDDI AKABIDHI VIFAA ZAHANATI YA KIMARA

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Iddi akimkabidhi vifaa vya huduma na tiba, Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Kata ya Kimara, Dk. Alphoncina Mbinda katika hafla maalum iliyofanyika jana, kwenye Zahanati hiyo, Kimara, Dar es Salaam. Vifaa hivyo vya sh. milioni 5.1, vimepatikana kutokana na michango ya wanachama na viongozi wa Jumuia ya Wazazi Tanzania. Wengine katika picha ni baadhi ya viongozi wa Jumuia ya Wazazi, Katibu Mkuu Hamis Dadi (kulia) Katibu Wilaya ya Kinondoni, Stanley Mkandawile (wapili kulia), na katikati ya Makamu na Mganga Mfawidhi ni Kaimu Mwenyekiti wa Jumuia hiyo, Dogo Mabrouk.
Wana-CCM Kata ya Kimara wakishangilia wakati wa hafla hiyo.
Wana-CCM na wananchi kwa jumla wakijimwaya mwaya kucheza muziki wa taarab, kushangilia makabidhiano ya vifaa hivyo vya huduma na tiba kwa Zahanati yao.
Baadhi ya wanachama wa Jumuia ya Wazazi waliohudhuria sherehe hiyo.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa kwenye sherehe hiyo ya makabidhiano ya vifaa vya huduma na tiba kwa Zahanati ya Kimara. Kulia (Mwenye koti) ni Diwani wa Kata hiyo ya Kimara kwa tiketi ya Chadema. Picha na na Bashir Nkoromo

Popular Posts