| ...Mkuu wa wilaya ya Kilwa mkoani Lindi,Abdallah Ulega akihutubia wananchi wa Tarafa ya Kipatimu wilayani humo.  | 
Wananchi  wa wilaya ya Kilwa mkoani Lindi wametakiwa kushiriki ipasavyo katika  vikao mbalimbali vya serikali za mitaa ili kurahisisha Upangaji wa  Mipango ya Maendeleo kufuatia hatua ya serikali kurudisha madaraka kwa  ushirikiswaji kutoka ngazi ya vijiji hadi Taifa
Akihutubia katika kilele cha maadhimisho ya nane ya siku ya Serikali za mitaa yaliyofanyika kiwilaya katika kijiji cha Mtongo Kimwaga Kata ya kipatimu wilayani humo,Mkuu wa wilaya ya Kilwa ,Bw Abdallah Ulega alieleza kuwa kushiriki vema kutasaidia wilaya hiyo kupanga mipango yake shirikishi na pia jamii itatumia ipasavyo haki ya msingi kufanikisha kujenga Demokrasia.
Akihutubia katika kilele cha maadhimisho ya nane ya siku ya Serikali za mitaa yaliyofanyika kiwilaya katika kijiji cha Mtongo Kimwaga Kata ya kipatimu wilayani humo,Mkuu wa wilaya ya Kilwa ,Bw Abdallah Ulega alieleza kuwa kushiriki vema kutasaidia wilaya hiyo kupanga mipango yake shirikishi na pia jamii itatumia ipasavyo haki ya msingi kufanikisha kujenga Demokrasia.
    Awali   kaimu mkugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Bw Peter Malekela  akimkaribisha mkuu wa wilaya hiyo kuhutubia hadhara hiyo baada ya kuweka  jiwe la msingi la Ujenzi wa Zahanati ya kijiji hicho alieleza  changamoto kubwa wilayani humo ipo kwa wananchi kutoshiriki kwa asilimia  kubwa katika vikao mbalimbali hali inayotoa ugumu katika utekelezaji wa  maamuzi yaliyoazimiwa.
Serikali za mitaa ni chombo kilichoundwa na kuwa na mamlaka ya kisheria huundwa na halmashauri za vijiji wilaya,Miji na mamlaka ya miji midogo Huadhimishwa kila tarehe 01 ya mwezi wa saba ambapo pia kunawepo Burudani mbalimbali ikiwa pamoja na kutembelea na kufungua miradi mbali mbali ya jamii.