Mwananchi wa kijiji cha Mzuri Makunduchi Bakari Ubwa, akitoa maoni yake  mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ametaka kuwe na Serekali mbili  ya Zanzibar na Tanzania Bara na kila Serekali iwe na uwezo wake na Rais  wa Zanzibar awe na uwezo wa kuamua mambo yake kwa ajili ya Zanzibar,Rais  wa Zanzibar awe na uwezo wa kuchagua Mabalozi kwa ajili ya Zanzibar na  Rais wa Tanzania pia na yeye achaguwe mabalozi wa Tanzania. 
   Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Balozi Salim Ahmed Salim,  akizungumza kuhusiana na utoaji wa maoni ya Mabadiliko ya Katiba ya  Tanzania katika mkutano huo uliofanyika viwanja vya Mtende. 
    Mwenyekiti wa Mkutano wa kutowa maoni ya Mabadiliko ya Katiba ya  Tanzania Mohammed Yussuf Mshamba, akisoma vipengele wakati wa kutowa  maoni ya mabadiliko ya katiba katika viwanja vya Mtende Makunduchi. 
    Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania Dk Mvungi, akitowa  maelezo  kwa Wananchi wa Kijiji cha Mtende waliofika kutoa maoni yao  katika viwanja vya Skuli ya Mtende. 
   Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania wakifuatilia maoni ya  Wananchi wa Kijiji cha Mzuri wakiyatowa mbele ya Tume hiyo ilioanza kazi  yake jana katika Wilaya ya Kusini Unguja Makunduchi Mkoa wa Kusini  Unguja.
   Mwananchi wa Kijiji cha Mzuri Makunduchi akikabidhi barua yenye maoni  yake kuhusu Mabadiliko ya Katiba, mkutano huo umefanyika katika viwanja  vya mpira timu ya Mwenge Mzuri, 
    Mwananchi wa Kijiji cha Mtende Makunduchi Aziza Mcha, akikabidhi barua  yake yenye maoni yake kwa Mwenyekiti wa Mkutano wa kutowa maoni ya  mabadiliko ya Katiba ya Tanzania Mohammed Yussuf Mshamba, wakati tume  hiyo ilipofika katika Wilaya ya Kusini Unguja kukusanya maoni ya  Wananchi kuhusu Katiba, mkutano huo umefanyika katika viwanja vya Skuli  ya Mtende.
   Mwananchi wa Kijiji cha Mtende Ali Khamis Ali, akichangia maoni yake kwa  kuanza kwa historia kuhusu Mzee Karume, ambaye amesema Unguja itakuwa  kama peponi na kweli ilikuwa hivyo kwa kujenga Nyumba za Wazee Sebleni  na kuanzisha Viwanda mbalimbali katika Zanzibar.Amesema kuwepo kwa serikali mbili ya Zanzibar na Tanganyika na kutaka  kuwe na Muungano wa Mkataba na kugawana sawa kwa sawa misaada  inayopatikana.  na mambo ya muungano kugaiwa sawa. 
   Mwananchi wa Kijiji cha Mzuri Makunduchi Duli Ali Duli, akichangia maoni  yake kwa Tume iliofika kukusanya maoni ya Wananchi kuhusu Mabadiliko ya  Katiba ya Tanzania, amesema kuwe na Serikali mbili ya Zanzibar na  Tanganyika, na kuondoa kasoro zilioko katika Muungano huu.
   Mwananchi wa Mtende Abuu Kombo Ramadhani, ametowa maoni yake kuwe na  serekali mbili na kuwe na uwiano katika nafasi za Muungano kwa pande  mbili hizi na Zanzibar iwe na rasilimali zake wenyewe bila kuingiliwa na  upande mwengine. na bara iwe hivyohivyo.  
    Mwnchi wa Kijiji cha Mtende Mohammed Shaka Mussa, amesema nashukuru  kuitwa Tanzania na pia Umoja ni Nguvu,Utengano ni Udhaifu. Amesema  kuwepo na serikali mbili ya Zanzibar na Tanganyika na kila upande uwe na  uwezo wa kuamua mambo yake na kuondoa kasoro za Muungano zilizopo ili  kuimarisha umoja wetu. 
    Wananchi wa Kijiji cha Mzuri Makunduchi wakiwa katika viwanja vya  Mwenge wakishiriki kutowa maoni yao wakisikiliza maoni ya Wananchi   mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania.iliyofika katika kijiji  hicho kukusanya maoni ya Wananchi. 
   Wananchi wa Kijiji cha Mtende wakisikiliza maoni yanayotolewa na  Wananchi wa Mtende mbele ya Tume ya Marekebisho ya Katiba katika viwanja  vya skuli ya Mtende 
  Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania Balozi Salim Ahmed  Salim. akibadilishana mawazo na Wazee wa Kijiji cha Mzuri  Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja, baada ya kumalizika kwa utowaji wa  maoni kwa Wananchi wa Kijiji hicho.Picha Zote na Mdau Mapara Othman-Kusini Unguja