Pages

Wednesday, June 6, 2012

TBL YATOA MSAADA WA VIFAA VYA USAFI ILALA

Mfanyakazi wa TBL, akimvisha Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi kifaa cha kuzuia vumbi kabla ya kuanza kufanya usafi.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mushi (kushoto) na Steve Kilindo wa TBL wakifagia ikiwa ni ishara ya kuzindua rfasmi maadhimisho hayo karibu na Soko la Mchikichini, Ilala, Dar es Salaam.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) wakiungana na watumishi wa Manispaa ya Ilala kufanya usafi wa mazingira katika makutano Barabara ya Uhuru na Mtaa wa Muheza, Karikaoo, Dar es Salaam jana. TBL ilitoa msaada wa vifaa vya usafi vyenye thamani ya sh. mil. 12 kwa Manispaa ya Ilala wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Mazingira, Dar es Salaam jana.
Meneja Uhusiano Mambo ya Nje wa TBL, Emma Oriyo (katikati), akizoa taka wakati wa kampeni hiyo ya usafi wa mazingira
Watumishi wa Manispaa ya Ilala na Wafanyakazi wa TBL, wakifanya usafi kwenye Mtaa wa Muheza, Kariakoo.
Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo (kulia) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi, msaada wa vifaa vya usafi vyenye thamani ya sh. milioni 12 kwa ajili ya Manispaa ya Ilala, wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Mazingira Duniani, Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi, akiendesha moja kati ya matolori yaliyotolewa msaada na TBL kwa Manispaa ya Ilala. Kulia ni Steve Kilindo wa TBL.
Mtaa wa Muheza, Kariakoo ukipendeza baada ya kufanyiwa usafi.

Popular Posts