Pages

Monday, June 4, 2012

USIKU WA SUGU ULIVYOFANA DARLIVE

Danny Msimamo akiwarusha wapenzi wa burudani.
Sugu akiwarusha mashabiki waliofurika ndani ya Dar Live usiku wa kuamkia leo.
Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari nae akitoa 'verse' kuupamba usiku wa Sugu ndani ya Dar Live.
Sugu na Mkoloni wakizidi kuwadatisha mashabiki.
Profesa Jay akiwapa burudani mashabiki wa Dar Live.
...Akiwasabahi mashabiki wake.
Mapacha kutoka kundi la Vinega wakiiteka steji ya Dar Live.
Suma G nae alikuwepo kuupamba usiku huo.
Juma Nature na kundi lake la Wanaume Halisi likifanya makamuzi stejini.
....Wanaume kazini.
Kundi la Naukala Ndima likifanya vitu vyake stejini.
Bendi ya Chuchu Sound nayo ilifanya makamuzi katika tamasha hilo la Usiku wa Sugu.
Mbunge wa Kinondoni (CCM), Idd Azzan akiwasalimia mashabiki wa Dar Live.
Nyomi iliyohudhuria Usiku wa Sugu.
Baadhi ya mashabiki wakiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Sugu.
-
Msanii mahiri wa HIP HOP ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi 'Mr II' a.k.a Sugu, jana alizikonga nyoyo za mashabiki wake waliofurika ndani ya ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam kwa kufanya makamuzi ya hatari katika tamasha la Usiku wa Sugu. Sugu alisindikizwa na Juma Nature, Profesa Jay, Vinega, Mkoloni na wengineo wengi kwenye shoo hiyo iliyokuwa ya aina yake.

Popular Posts